Watu wakimya (introverts) mnapataje marafiki wa kawaida ukubwani?

Watu wakimya (introverts) mnapataje marafiki wa kawaida ukubwani?

Duksi

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2019
Posts
229
Reaction score
576
Hulka moja wapo ya watu wakimya (introverts) ni ugumu wa kujichanganya na kuzoeana na watu wapya. Hii inapelekea wengi wanajikuta hawana marafiki ukitoa watu wachache wale waliofahamiana wakati wa chuo/sekondari, biashara/kazini. Siku zinavyosonga na wanavyozidi kukukua kimaisha "cycle" ya marafiki alionao inazidi kupungua. Anabakiwa na zaidi familia tu na rafiki mmoja au wawili.

Anajikuta imefika weekend mtu anatamani kujiachia kidogo na kubadili mawazo ila akiangalia hana watu wa kujumuika nao. Akiingia bar/mgahawa anakuta majamaa wamekaa kwenye meza kwa vikundi, inabidi aidha akae meza yake mwenyewe au akae counter...lakini anakosa ile ladha ya urafiki na uhusiano walionayo wengine kwenye maisha ambapo hubadilishana mawazo na kupeana changamoto chanya za kimaisha.

Kwa upande mwingine wanakuwa ni watu wanaojitegemea (independent) kifikra na kwa mambo mengi hufanya maamuzi na kuendesha maisha bila kutegemea ushauri au mawazo ya wengine. Pia kutokana na kutokuwa na watu wengi huwa hawana zile drama/changamoto za marafiki.

Faida za marafiki ni nyingi kuliko hasara, hebu introverts toeni mbinu za kupata marafiki wapya ukubwani.
 
Kama umeniona siku hiz pozi langu ni kaunta tu, mbaya zaidi zaidi hata wale niliosoma nao wote urafiki uliisha..
Sina marafiki wapya na mtu hawez kunizoea kirahisi.. Ila ndo hivyo tunaishi humo humo.
 
.

Kwa upande mwingine wanakuwa ni watu wanaojitegemea (independent) kifikra na kwa mambo mengi hufanya maamuzi na kuendesha maisha bila kutegemea ushauri au mawazo ya wengine. Pia kutokana na kutokuwa na watu wengi huwa hawana zile drama/changamoto za marafiki.

.

And this is what makes them so strong and intelligent!!

Shout out to all introverts out there!!
 
Nakumbuka nilikaa kwa muda wa miaka mitatu zanzibar sijawahi kwenda forodhani.

Sikuenda kwa sababu sikua na mtu wa kwenda nae kuenjoy nae.

Kuna kipindi nilijiona sipo sawa nikahisi nna tatizo ila nikajisemea mbona kama hili sio tatizo baadae nikagundua kumbe kuna aina hii ya watu,hapo ndipo nikaanza kurelax juu ya tabia yangu hii maana watu walinitisha sana kwamba napenda kujitenga,sipendi watu n.k

Mziki unakua nikiumwa ghafla tu,kuna safari niliumwa niliisoma namba mbona.
Faida za marafiki ni nyingi kuliko hasara, hebu introverts toeni mbinu za kupata marafiki wapya ukubwani.
Rafiki wa kweli ni yule ambae hamkuzoeana haraka.

Ukiona umezoeana na mtu haraka basi jua mtakorofishana tu,sio MARA ZOTE.

Mimi binafsi mpaka sasa sina rafiki wa mtaani ambae nashare nae mambo yangu,nina rafiki angu ambae hayupo tanzania tunapiga stori sana na kushare mambo yetu
 
Sina marafiki wapya na mtu hawez kunizoea kirahisi.. Ila ndo hivyo tunaishi humo humo.
Kuna mpuuzi mmoja alinizoea ghafla mimi nikawa namchukulia kawaida kama watu wengine tu.

Akanikopa pesa hajarudisha nikasema wewe ndo kwa heri nakutoa katika list,ajabu sijapunguza mazoea nae kwa sababu sikuwahi kuzoweana nae,naishi nae kama mwanzo.

Akinikopa ni mwendo wa sina kaka,sina kaka,daaah niko vibaya kaka,dah ningekuwezesha
Hapo nabadili misemo tuu.

Uzuri ni kuwa usipomzowea mtu ukaishi nao katika standard level watu wote ni ngumu mtu kukuosoma
 
Back
Top Bottom