Watu wanaolalamikia internet kufosi Starlink mbona Voda, airtel wana unlimited nzuri kwa 120,000 tu kwa mwezi

Je Starlink inakaa ndani? Ni Dishi linakaa juu ya bati, so kusema Router inakaa nje ndio upate network sio Excuse ya kuhalalisha.
 
1. Labda kama walibadilisha tena kuna mnaija mmoja alitoa uthibitisho wa kuvuka, alifika 6TB, ila sjajua sana.

2.Kwa video niliyoiona youtube channel ya Nigeria pia walikua wanapata 230mbps kwa 43$, kama wanepandisha pia sijafatilia sana.

3. Mengine inaweza kua kweli ila nimeskia kuna mijadala mahala kwamba ana ongeza satellite so wenda kwa issue ya kenya na ukanda wetu mambo yaka kaa sawa soon.
 
tatizo ni ubora wa huduma
 
Nimejitahidi sanaa kuelimisha wa tanzania ila hawaelewiii wabishi satellite sio kwa watqnzania masikini .....pia hutumika mbugani au vitani tanzania full coverage za mitandao ya simu hivyo hatuwezi pia gharama ziko juu sanaa hakuna wa tz wataweza watu wanaropoka tu dola 70 hadi 100 kila mwezi wataweza ??
 
Mkuu TTCL yangu ya copper 4mbps in theory kwa mwezi 1.2-1.3TB. so kama speed inashuka after 1TB still it's possible kufikisha 6TB, assume unapata 10mbps after speed kudrop kwa mtu mmoja ama wawili watatu sio mbaya ila watu 6 kuendelea itakua speed ndogo sana.

Hio 230mbps ni pale inaanza unakuta Satellite nzima upo mwenyewe, hii internet ni shared the more mnavyoongezeka the more speed inashuka, unlike fiber ambayo waya mmoja unaenda Hadi 10Gbps. Mfano hii Airtel wqliyozindua juzi 5G unlimited backbone yake ni 180 Terabyte per second, kuijaza hio ni kama watu Milioni 10 Kila mtu awe online kwa speed ya 10-20mbps.

Kwa Kenya kifurushi Cha kawaida ni 25-100mbps download na 10mbps upload ila most of time unacheza around hio 40mbps. Ukitaka speed ya 200mbps kupanda ni business package.

Yes hata Mimi nimesikia Wana mpango wa kuongeza satellite satellite Ukanda wetu by mwezi wa 6 mwaka huu.
 
Kwa hiyo kama Voda na Airtel na hao watu wengine wanazo basi haitakiwi taasisi nyingine kuingia? Huwezi jua fupi, kama kila siku wapita njia ileile.
 
Nimekupata loud and clear mkuu.
 
Tofaut kati ya star lnk na hao ulowataja ni moja tu star lnk ni ukwel na uhakika wakat hao wengne speed yao hailewek na ukitumia sana inaanza kua slow sana
Mi natumia iyo ya airtel ttzo lao ni speed mchana ad jion speed ni 126kb/500 kb per second ila usiku kwanzai saa 7 saa8 ndo unapata speed ya 1mb /2mb per scnd
 
Msaada wakuu mimi niko na shida ya kuangalia mpira ligi ya bongo nina smartphone ina bando mchawi ni account ya azamTv max yangu kifurushi kimeisha sasa hapa usawa haukabi kwa mwenyewe azamTv decoder ambae hatumii kweny cm au hata anaetumia anisaidie ni angalie hata kwa leo tu wajameni.. Au aje tubadilishane anipe ya azamTv mimi nimpe ya Dstv.. Asante, Dm tafadhari.
 
Jinsi ya kujiunga unlimited please
 
Kama umeelewa Voda ni wewe aise
Kama nafasi ipo acha waje hao starLink na wengine km wapo waje tu
 
Mbona kuna app nyingi play store za kusngalia mpira azam tv?? Au unatumia High Phone
 
Watu wanaongelea unlimited internet, hayo ya buku 1 buku mbili yanakujaje tena.
 
Jinsi ya kujiunga unlimited please
Angalia location Yako kwanza kama ina fiber iwe priority ni fiber, katikati ya jiji na Maeneo kama mbezi Makampuni kama Zuku yapo, Maeneo kama Sinza nasikia Kuna Fiber ya Vodacom na Kuna provider wengine local maeneo tofauti. Kama fiber ipo ukiwapigia wanakuja, kama umehakiki fiber ya Kampuni Fulani ipo ukipost hapa utapewa contact za kupiga.

Ukikosa fiber ni 4G/5G hizi unaenda mTandao husika,
-Airtel wanahitaji 270,000 ambayo laki 2 ni Bei ya router na 70,000 mwezi wa kwanza, Ama kama una Tin na leseni zipo package za biashara ambazo wanakupa Router Bure na unalipia kwa mwezi 110,000.

-Tigo wanataka 650,000 ya router na Kila mwezi unalipa 70,000

-voda wanaanzia 120,000 ila wanahitaji Tin na kitambulisho.

TTCL wao wanaanzia 25,000 tu kwa copper na 55,000 kwa fiber ila ni pasua kichwa.
 
Kuna halotel special wanaoption ya 15K Kwa Gb 18. Kwa sisi uchumi wa kati

Starlink ni gharama zaidi kulinganisha na hizi unlimited za voda tigo ttcl and halotel
 
Watu wanataka speed, hiyo mitandao uliyoitaja speed sio kubwa na hata ikiwa kubwa ni baadhi ya maeneo tu..!
 
Yaani ni aheri starlink iwepo walioithinisha starlink sio kwamba hawana akili. Binafsi hata wangesema kwa mwezi laki 5. Tunaweza kuji-adjust kuendana na uchumi huo na kizuri zaidi ni non-contract business ukiwa nayo sawa isipokuwepo sawa.
Kuna vijana katika clubs zao wanaweza wakajiunga na wakawa wanafanya business zao na maisha yanaenda.
Masuala ya kusema ni ghali, jua umezeeka na upo nje ya mfumo wa uchumi wa sasa.
Makampuni yaliyopo 100Mbps ni karibu laki nne kwa mwezi. TTCL ndio ingekuwa mkombozi wetu lakini wamejifungia wanakula mishahara hawawazi mfumo bora wa kiushindani na kutanua biashara.
Binafsi niliomba ninunue mimi cable za fiber ndio waniunge waligoma katakata wanataka ununue kwao afu km 5 milion 20
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…