Watu wengi wa Pwani hawajui kuzungumza kiswahili Fasaha

Watu wengi wa Pwani hawajui kuzungumza kiswahili Fasaha

ZANZIBAR SWAHILI WORDS

wewe - weye

majukumu - kazi mkononi

funga mlango - tia Pete

usiniudhi - nitolee hashuo

nyanya - tungule

bubble gum - ubani

wali - ubwabwa

mjomba - ammy

sokoni - marikiti
Ami au hio uloandika ammy ni baba mkubwa au baba mdogo. Mjomba ni hio hio mjomba yaani ndugu wa mama
Funga mlango pia unaweza kusema komea mlango. Na hio Korlmea au tia pete yaani ni ku lock. Lkn funga ya ku shut tunatumia hio hio funga mlango.
Hapo nilitegemea ungeongelea tunavyokata maneno
Usinikere usin'kere
Nakwenda-naenda n.k
 
Kiswahala fasaha kinazungumzwa Unguja mjini, Na miji iliyokaribu na Unguja Mjini nayo pia ndio inazungumza kisawahili lizuri. Sasa mkuu ukihisi wewe upo tofauti nao basi ujijue kuwa wewe ndio hujui
 
Zanzibar ni pwani lakini kiswahili chao kuna maeneo kina Shida sana,Niliwahi kukaa na mzazibari sehemu alikuwa akiongea simuelewi kabisa anaongea nini. Nimezaliwa pwani,nimekulia pwani,hakuna sehemu utapata kiswahili sahihi kama pwani. Pwani ndio kwa waswahili. Mfano mmoja wa mpemba ndio uje ukosoe watu wote wa pwani?

MKuu Kiswahili sahihi kipo Zanzibar
 
Back
Top Bottom