Watu zaidi ya 15 wafariki kwa ugonjwa usiofahamika, Chunya

Watu zaidi ya 15 wafariki kwa ugonjwa usiofahamika, Chunya

Status
Not open for further replies.

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Wananchi wa kata ya Ifumbo wilayani Chunya wameripotiwa kuugua ugonjwa usiofamika ambao mtu akiugua anatapika damu mpaka anapoteza maisha, na mpaka sasa tayari watu zaidi ya 15 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 50 wanaendelea kuugua, hali ambayo imesababisha halmashauri hiyo kuomba msaada wa kitaalam katika ngazi za juu ili kuubaini na hatimaye kupata tiba yake.
vlcsnap-2021-02-06-14h20m37s582.png

Taarifa ya kuwepo kwa ugonjwa huo usiofahamika imeibuliwa na diwani wa kata ya Ifumbo Mhe.Weston Mpyila mbele ya kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Chunya huku akiomba msaada wa kuwanusuru wananchi wake.

Mganga mkuu wa wilaya ya Chunya, Dk.Felister Kisandu amethibitisha kuwepo kwa ugonjwa huo ambao wameshindwa kuutambua na kudai kuwa ofisi yake imeomba msaada katika ngazi za juu ili wasaidiwe kuutambua na kukabiliana nao.

Chanzo: ITV

---

KANUSHO: Serikali kupitia Wizara ya Afya imekanusha taarifa za mlipuko wa ugonjwa huo. Zaidi soma Serikali yakanusha kuwepo mlipuko wa Ugonjwa wowote kata ya Ifumbo, Mbeya. Wizara ya Afya kuichukulia hatua ITV
 
Wataalamu wa afya wafanye uchunguzi haraka kubaini chanzo ili kudhibiti.
pole kwa watanzania wenzetu walio ifiwa, Mungu azipokee roho zao

lakini kwa nini mnazusha wakati vifo hivi vimetokea kwa nyakati tofauti tofauti?! tangu mwaka juzi tena kwa idadi ya mtu mmojammoja! leo hii mnataka kuaminisha kuwa watu 15 wamekufa kwa mkupuo!!

mnapata faida gani mnapo potosha taarifa?!
na kuaminisha watu kama vile vifo vimetokea kwa wakati mmoja kumbe sio!
 
Tanzania inatakiwa kuwepo na kikosi maalumu kwa ajili ya magonjwa ya milipuko na ikiwezekana wanakua na chopa yao kabisaa ya emergency bila kutegemea usafiri wa magari hapo tutakua tumeweza maana hii ya watu kutoa taarifa mpaka kwenye kikao cha madiwani na ishu ya kuzima Moto Mungu atusaidie kwa kweli...
 
Tanzania inatakiwa kuwepo na kikosi maalumu kwa ajili ya magonjwa ya milipuko na ikiwezekana wanakua na chopa yao kabisaa ya emergency bila kutegemea usafiri wa magari hapo tutakua tumeweza maana hii ya watu kutoa taarifa mpaka kwenye kikao cha madiwani na ishu ya kuzima Moto Mungu atusaidie kwa kweli...
Nani kakuambia hakipo? Ubaya wa nyakati hizi ni kwamba sirikali yetu haitaki kuwa wazi.

Au umesahau Mwele alifanywaje baada ya kusema Tanzania kuna Zika virus? Sasa huyo Mwele ndiyo alikuwa hiko kitengo.
 
TUWE MAKINI SANA NA HAWA MABEBERU.TENA MBAYA ZAIDI TUMEKATAA CHANJO NA BILL GATES ALISEMA KUNA JANGA LITAKUJA BAYA ZAIDI HATUJUI LITAANZIA NCHI GANI.
 
Duh! Mamlaka husika zichukue hatua muhimu kufanya uchunguzi na hatimaye kudhibiti taharuki hiyo. Isije ikawa ni choko choko za mabeberu.
 
Tanzania inatakiwa kuwepo na kikosi maalumu kwa ajili ya magonjwa ya milipuko na ikiwezekana wanakua na chopa yao kabisaa ya emergency bila kutegemea usafiri wa magari hapo tutakua tumeweza maana hii ya watu kutoa taarifa mpaka kwenye kikao cha madiwani na ishu ya kuzima Moto Mungu atusaidie kwa kweli...

Haya mafuta tu, mpaka docs za manunuzi zikamilike washakufa 20
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom