Satoh Hirosh
JF-Expert Member
- Mar 30, 2021
- 6,432
- 25,646
- Thread starter
- #161
Naaaaaaaaaaaaammm!! 🤣Kuna yule wa Igoma Mwanza wakuitwa Muhili Obale muite sasa jina lake uone nalaa lake. Anaitika robo saa nzima. Hiyo ilikua Radio Free Africa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naaaaaaaaaaaaammm!! 🤣Kuna yule wa Igoma Mwanza wakuitwa Muhili Obale muite sasa jina lake uone nalaa lake. Anaitika robo saa nzima. Hiyo ilikua Radio Free Africa.
Nasikia ni hayati huyu Kwa sasa..R.i.p
Ooh..asante Kwa taarifa mkuuYupo hai
Masumbuko lamwai shombeKuna yule wa Makongorosi Chunya namkumbuka kwa jina 1 tu la Masumbuko,halafu kuna bingwa wa kuning'inia kwenye tawi la mchicha,nafikiri huyu atakuwa wa Dodoma.
Hailimwi ileMing'oko ambayo alikula mpwayungu village alipokuwa Lindi? Kwani Ile mizizi inalimwa Mzee Baba? Naionaga Kwa wingi nikienda mbagala
kuna MWALIMU KENNEDY MPEMBA nae ni mdau balaa
Aise namm nimepamiss San sumbawangaPale pale mjini na ndio maana ikawa ni rahisi kumpata.....ni watu maarufu kwenye mji ule,tena kwasasa huyo Paul ana duka la jumla la retail shop
Nitarudi tena kwenye ule mji muda si mrefu nimepakumbuka ni almost miaka 2 sijafika
Umesahau Matumla s Matumla wa kirombero kidatu MorogoroMiaka imesonga sana, maisha yamebadilika Kwa kiasi kikubwa.Tofauti na sasa ambapo ukiwa na simu janja au tarakirishi unapata taarifa zote zilizotokea na zilizovunjika 'breaking news', Zamani redio ilikuwa chombo muhimu ktk kupata taarifa na burudani.
Leo nimewakumbuka wale watuma salamu maarufu enzi zile,ingawa hata sasa wapo baadhi ya watu ambao ni maarufu ktk vipindi mbalimbali ukisikiliza redio km Clouds mfano kuna heri dereva babaji, shangwe dereva babaji, Daudi wakota n.k
Enzi hizo ukisikiliza kipindi cha mirindimo asilia na Malima Nderema au salamu Kwa wagonjwa, kuna majina maarufu huwezi kuacha kuyasikia wakati wa kutuma salamu.
Kuna huyu jamaa wa kuitwa Wajadi fundi Wajadi binadamu mashaka, yeye kila siku yupo safarini kuelekea mahuta shimoni, fundi Khamisi full migebuka wa mwandiga fashion sokoni Kigoma.
Lawena Msonda Baba mzazi kutoka chunya Mbeya.
Ally Mrangi Gigiri Mresa yeye mar kila siku yupo safarini kuelekea mabibo Dar es Salaam.
Zakaria Ndemfoo, Issa Mzee wa urembo kutoka Moshi. Lupa tingatinga "mdau asiyechuja" ndiyo ilikuwa slogan yake bila kumsahau Chesko Mzee wa matunda kutoka Africa Sana.
Kuna mdau akiitwa Limonga Justine Limonga na kuna huyu mama Abuu wa majani mapana. Kuna jamaa aliitwa Fikiri Dario Gakala wa GGM Geita na Filbert Kyenshambi kutoka Muleba-Nshambi, wapo wengi sn na tulikuwa tunaenjoy sana Enzi hizo
Unawakumbuka baadhi? Unazikumbuka kauli mbiu zao maarufu zilizotamba?