Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Niliogopa ulipoanza kusema ila baada ya kuona hiyo CV nikaona ni kitu cha kawaida sana braza. Wewe kama mtumishi, ni muhimu sana mwajiri wako akajua hizo taarifa ikiwemo dini yako, kabila lako, wazazi wako, kwenu ni wapi na taarifa nyingine. Hizo ulizoziainisha ni sawa na zile ulizoandika wakati unajaza kwenye NIDA. Kwa sasa wana establish mifumo ambayo inakuwa na taarifa zako sahihi kote za kikazi na kiraia.

Kwa wewe kama mtumishi, unaweza ukafa kazini, je wakuhudumie kwa imani gani ya dini? Je wakupeleke wapi? Je taratibu za kabila lako zikoje? Haya ni mambo ambayo hayahitaji kubahatisha. Kwa sababu kuna watu walishawahi zikwa kwa imani tofauti maiti ikaja fukuliwa kuzikwa upya. Hapa nimetolea mfano tu braza lakini kunaweza kuwa na sababu zingine muhimu tu zaidi. Kwa hiyo hupaswi kuwa na hofu ya namna hiyo. By the way, wewe kutakiwa kujaza dini haitakuwa mara yako ya kwanza, naamini kuna sehemu nyingi tu wewe na mimi tumeandika ikiwemo kwenye kupata kitamburisho cha Nida, Lesseni za udereva n.k. Relax
 
Kelvin...
Inategemea ni dini gani uliyokusudia.
Nakuwekea hapa Uislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika:

Soma makala hii hapo chini inaweza kuwa msaada kwako kuielewa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na pia kuelewa jinsi Uislam ulivyotumika kuleta umoja wa wananchi katika kupambana na ukoloni:

DINI ILIVYOWAUNGANISHA WATANGANYIKA DHIDI YA UKOLONI: NAFASI YA DUA NDANI YA TANU VISOMO VYA QUR'AN NA DUA ZILIZOFANYIKA WAKATI WA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA: SEHEMU YA NNE

Inategemea watu watakavyoitumia dini.

Dini inaweza kutumika kuwaunganisha watu na pia inaweza kutumika kuwagawa.

Mikutano ya mwanzo ya TANU pale Mnazi Mmoja ilifunguliwa kwa dua na watu wakisoma Surat Fatha na kutikia dua hiyo kwa pamoja.

Aliyekuwa akiongoza dua hii alikuwa Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Leo ni tabu sana kwa mtu kuamini kuwa hali ilikuwa hivi kuwa hata mikutano ya ndani ya TANU pale New Street ilikuwa ikifunguliwa na kufungwa kwa dua na Nyerere akiwapo.

Mwalimu Nyerere katika hotuba yake maarufu kwa Wazee wa Dar es Salaam Ukumbi wa Diamond wakati wa kustaafu urais mwaka wa 1985 alieleza kuhusu dua aliyofanyiwa na akashiriki nyumbani kwa Mzee Jumbe Tambaza.

Hotuba hii imekuwa maarufu sana khasa kipande hiki anachoeleza jinsi yeye Mkristo alivyopokelewa na Waislam wa Dar es Salaam akiwa na vijana wenzake Abdul Sykes na Dossa Aziz.

Hawa vijana wawili Abdul Sykes na Dossa Aziz, marafiki wa Baba wa Taifa ndiyo waliompeleka Mwalimu Nyerere kwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir kumtambulisha na kutaka msaada wake akubalike kwa Waislam na kuanzia siku ile Sheikh Hassan bin Ameir na Nyerere walikuwa wazalendo wawili wakisaidiana katika kudai uhuru wa Tanganyika Sheikh Hassan akiuza kadi za TANU ndani ya misikiti ya Dar es Salaam alikokuwa akidarsisha.

Turejee kwenye visomo na dua wakati wa kudai uhuru.

Lilikuwa jambo la kawaida sana wakati ule kwa Waislam waliokuwa katika mapambano na ukoloni kutanguliza mambo yao yote kutaka msaada wa Allah.

Hili lilikuwa jambo lililokuwa linakuja hata bila ya kufikiri.

Mwaka wa 1949 kabla ya mgomo wa makuli wa Bandari ya Dar es Salaam, walifanya kisoma na dua kubwa na baada ya hapo ndipo walipoingia barabarani kwa maandamano kama ishara ya kuanza mgomo.

Abdul Sykes alihusika sana katika mgomo huu.

Mwalimu Nyerere kwa hiyo hakuwa kiongozi wa kwanza katika harakati kufanyiwa kisomo na Waislam.

Mwalimu Nyerere yeye haya hakuyajua kwani alizikuta harakati katikati.

Abdul Sykes alikuwa Market Master Kariakoo Market nafasi kubwa sana wakati wa ukoloni na yenye wasaa na fursa za kutosha.

TANU ilipoanza Abdul Sykes akawa anauza kadi za TANU pale sokoni na Nyerere alikuwa hapungui ofisini kwake.

Special Branch wakiwafuatilia na siku moja Abdul Sykes akavamiwa na mkubwa wake Mzungu, Town Clerk ambae soko lilikuwa chini yake.

Abdul na huyu Mzungu walipambana kwa maneno makali Abdul akidai kuwa TANU kilikuwa chama halali na si kosa kuwa na kadi zake.

Hofu iliyotanda pale sokoni ilikuwa Abdul atafukuzwa kazi.
Abdul wakati ule Abdul alikuwa kijana wa miaka 30.

Wazee wafanyabiashara pale sokoni akina Sharif Mbaya Mtu, Mshume Kiyate, Shariff Abdallah Attas, huyu alikuwa mfanyakazi wa soko, mkusanyaji ushuru wa nafaka pale sokoni walijikusanya na pakafanyika dua kubwa ya kisomo na wakachinja mnyama.

Hii ilikuwa ndiyo dua ya kwanza kwa TANU kufanya kisha zikafuata dua aliyofanyiwa Rashid Ali Meli na ile ya Nyerere.

Rashid Ali Meli yeye alikuwa mweka fedha wa Dar es Salaam Municipal Council.

Rashid Ali Meli alifungua safe yake ofisini akatoa fedha kuikopesha TANU akamkabidhi Iddi Faiz Mafungo aliyekuwa Mweka Hazina wa TANU ili aziingize katika mfuko wa safari ya Nyerere UNO.

Siku ya pili wakaguzi wakaja ofisini kwake kufanya ukaguzi bahati nzuri hawakuanza na kukagua fedha taslimu.

Ilikuwa wazi kuwa endapo wakaguzi watagundua kuwa kuna upungufu wa fedha Rashid Ali Meli atashtakiwa kwa wizi na atafungwa.

Taarifa hizi ziliipofika ofisi ya TANU kitu cha kwanza kabisa ikawa pafanywe dua.

Baada ya kisomo hiki cha Rashid Ali Meli kikafuatia kisomo cha Lindi alichofanyiwa Baba wa Taifa na Sheikh Mohamed Yusuf Badi mwaka wa 1956 kisha ikafuatia dua ya Mnyanjani, Tanga kabla ya kwenda Tabora kwenye mkutano wa Kura Tatu uliotishia kuigawa TANU katika mapande mawili.

Picha hizo hapo chini ni Mkutano wa TANU Mnazi Mmoja miaka ya mwanzo ya TANU, picha ya pili ni kushoto Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia na Julius Nyerere.

Picha ya tatu ni Soko la Kariakoo kama lilivyokuwa katika miaka ya 1950 na picha ya nne ni Shariff Abdallah Atttas.

Picha ya mwisho kulia ni Lawi Sijaona, Abdul Sykes, Julius Nyerere na Dossa Aziz katika hafla Ukumbi wa Arnatouglo kumuaga Nyerere safari ya pili UNO 1957.

Namaliza kwa kusema kuwa hivi ndivyo Waislam walivyoitumia dini yao katika kuleta umoja wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika umoja ambao hivi sasa haupo tena kwani uhuru ulikuja na changamoto zake na moja ya changanoto kubwa ikawa kuzuka kwa uadui dhidi ya Uislam ikawa chochote kinachowahusu Waislam hakiangaliwi kwa jicho la kheri na wale walioshika madaraka ya serikali.

Taratibu hata historia hii ya wazalendo hawa waliopigania uhuru ikawa haitakiwi na zikafanyika juhudi kubwa na za makusudi kuwafuta mashujaa hawa katika historia ya Tanganyika.

Wazee wetu wameonyesha kuwa dini inaweza kutumika kuwaunganisha watu.
Bahati mbaya sana leo dini inatumika kuwabagua watu.

MWISHO

View attachment 2099044
Asante. Nime jifunza
 
Shinge2,
Zipo na data zinazopingana na data za CIA na kama ninavyokueleza nimezijibu takwimu za CIA kwa jicho lililoshuhudia harakati za uhuru 1950s.

Pia kuna mjadala wa sensa ya 1967 na yaliyojiri na nimeandika niliyokutananayo katika kitabu cha Abdul Sykes.

Siku zote mimi nimekuwa nikikwepa kuzungumza suala hili kwa kutambua linavyogonga nyoyo za watu.

Ninazo taarifa nyingi tu ambazo zinaonyesha tatizo katika utoaji wa nafasi za elimu.

Kuna utafiti wa Warsha (1981), Barua ya Prof. Kighoma Malima kwa Rais Ali Hassan Mwinyi kuhusu aliyogundua Wizara ya Elimu (1987) na Hotuba ya Kitwana Kondo Bungeni 1999.

Utafiti wa Warsha ulighabisha sana serikali na wako waliofukuzwa nchini na wengine kuigwa marufuku kutokuwa viongozi katika taasisi yeyote ya Kiislam, Prof. Malima akatolewa Wizara ya Elimu na Kitwana Kondo hakuweza tena kutetea kiti chake.

Nadhani unaweza kukisia kwa nini ilikuwa hivi.

Ukisoma taarifa hizi utaogopa na utajiuliza kweli haya wanafanyiwa Waislam nchi hii?
Je, serikali inayajua haya?

Hapa sina haja ya kueleza tuhuma za Waislam dhidi ya NECTA zilizopelekea Waislam kufanya maandamano mwaka wa 2012.

Ndugu yangu nina mengi niyajuayo katika miaka yangu ya utafiti wa historia ya Waislam wa Tanganyika.
Mkuu ninakupata. Ila usisahau kuwa ktk swala la elimu uliloligusia, ukiangalia kwa makini na kufanya utafiti hata LEO ni kuwa Wakristo na Taasisi zao za Dini walipoingia Tanganyika walijikita zaidi ktk kujenga Taasisi za Elimu, Hospitali nk. Wakati huo huo Taasisi za Kiislamu zilijikita sana ktk kiwafundisha WATOTO wao elimu ya Madrassa wakisema Elimu dunia ni upuuzi. Hata hivyo baadhi ya Wazazi waliojaliwa uelewa hawakukubaliana na hilo. Baada ya Madrassa waliwaingiza watoto wao katika shule za MISHENI/KIKRISTO ili wasome. Miongoni mwao ni kina Jakaya Kikwete na wengine wengi. Sasa ukiangalia hiyo ratio inajieleza yenyewe. Wakristo wakasoma hasa. Waislamu wengi wakakataa hata kuwaingiza watoto wao ktk shule za Kikristo ndo kushuka kwa idadi ya WASOMI miongoni mwa Waislamu. Jaribu kuchukua Data za IDADI ya Taasisi za ELIMU, Hospitali, Nyumba za Wazee nk utakuta ni NYINGI sana sana. Ukilinganisha za Kiislamu utakuta zile KIDOGO zilizopo zimeanzishwa miaka ya hivi karibuni kama vile chuo cha UMMA huko Morogoro. Kwa hiyo basi Wakristo walihudumia mioyo na pia walijaribu sana ktk kubadilisha MAISHA ya Wenyeji waliokuwa wakiwapa dini.
Hii ni kusema nini? Wengi wa wasomi ni Wakristo kutokana na sababu nilizozieleza hapo juu. Nafikiri inajieleza yenyewe. Shukrani.
 
mnarefusha mjadala buree, historia imeeleweka vyema.
sasa tuangalie wakati uliopo je? bado kuna tatizo na kama lipo linasababishwa na nini kwa sasa?
nini kifanyike ili sasa tuijenge Nchi yetu kwa nguvu ya pamoja?
maana kama wasomi wa dini zote sasa wapo wengi tu, hakuna tena kisingizio..
 
mnarefusha mjadala buree, historia imeeleweka vyema.
sasa tuangalie wakati uliopo je? bado kuna tatizo na kama lipo linasababishwa na nini kwa sasa?
nini kifanyike ili sasa tuijenge Nchi yetu kwa nguvu ya pamoja?
maana kama wasomi wa dini zote sasa wapo wengi tu, hakuna tena kisingizio..


Umeandika vizuri lakini hapo itabaki swala la kimahesabu tu ya uwiano na uchambuzi (ratio analysis , interpretation and application ).

Kule kwenye wasomi wengi zaidi zikitangazwa nafasi za kazi chances ya wao kujitokeza kuomba hizo nafasi ni kubwa na obviously chances za idadi yao kuweza kupata hizo nafasi zikawa kubwa pia.

Na kinyume chake kitakuwa sahihi pia .

Swala hapo ni kuweka kanuni thabiti na uwazi katika usaili.

Kuwepo na ushindani huru na siyo kutafuta hisani kwa visingizio ambavyo ha ipo.

Haki ionekane kutendeka kwa uwazi.

Udini usiwepo kabisa.
 
Nilichomaanisha ni kwamba kuwe na 50/50 kwenye hizi fursa,ukizungumzia usomi hata waislamu wanasoma na wamesoma after that

Sasa hoja ya kusema kwamba Christians wako wengi kwenye nyadhifa mbalimbali eti kwa sababu wao wana wasomi wengi kuliko waislamu hiyo ni rubbish
Siyo 50/50 kwa wakristo na waislamu. Hi nchi siyo ya wakristo na waislamu peke yao.

Kila mtu ana kwa imani yake awe Rastafarian, budha, mpagani, Hindu n.k haki ya 50 kwa 50
 
Mkuu ninakupata. Ila usisahau kuwa ktk swala la elimu uliloligusia, ukiangalia kwa makini na kufanya utafiti hata LEO ni kuwa Wakristo na Taasisi zao za Dini walipoingia Tanganyika walijikita zaidi ktk kujenga Taasisi za Elimu, Hospitali nk. Wakati huo huo Taasisi za Kiislamu zilijikita sana ktk kiwafundisha WATOTO wao elimu ya Madrassa wakisema Elimu dunia ni upuuzi. Hata hivyo baadhi ya Wazazi waliojaliwa uelewa hawakukubaliana na hilo. Baada ya Madrassa waliwaingiza watoto wao katika shule za MISHENI/KIKRISTO ili wasome. Miongoni mwao ni kina Jakaya Kikwete na wengine wengi. Sasa ukiangalia hiyo ratio inajieleza yenyewe. Wakristo wakasoma hasa. Waislamu wengi wakakataa hata kuwaingiza watoto wao ktk shule za Kikristo ndo kushuka kwa idadi ya WASOMI miongoni mwa Waislamu. Jaribu kuchukua Data za IDADI ya Taasisi za ELIMU, Hospitali, Nyumba za Wazee nk utakuta ni NYINGI sana sana. Ukilinganisha za Kiislamu utakuta zile KIDOGO zilizopo zimeanzishwa miaka ya hivi karibuni kama vile chuo cha UMMA huko Morogoro. Kwa hiyo basi Wakristo walihudumia mioyo na pia walijaribu sana ktk kubadilisha MAISHA ya Wenyeji waliokuwa wakiwapa dini.
Hii ni kusema nini? Wengi wa wasomi ni Wakristo kutokana na sababu nilizozieleza hapo juu. Nafikiri inajieleza yenyewe. Shukrani.
Shinge2,
Unajadili somo usilolijua.

Unaijua historia ya kuvunjwa kwa EAMWS 1968?

Unajua kwa nini ilivunjwa na serikali kuunda BAKWATA?

EAMWS 1968 ilikuwa inajenga shule nchi nzima na jiwe la msingi la Chuo Kikuu liliwekwa na Julius Nyerere.

Waislam wanajenga Chuo Kikuu?
Hili halikubaliki.

Waislam wanajenga shule na wanajenga Chuo Kikuu sisi hatuna Chuo Kikuu!

Hii EAMWS lazima tuivunje kabla haijajenga Chuo Kikuu.

Unaijua historia hii?

EAMWS ikavunjwa na miradi yake yote ya elimu ikaenda na maji.

Je, unawajua waliotenda haya ndani ya serikali ya Tanzania?

Hii ndiyo hatari ya kutaka kujadili mambo usiyoyajua.

Nani kakufunza kuwa Waislam hatukuwa na mipango ya elimu?

Tupiganie uhuru hadi upatikane tusijue tutafanya nini tukishapata uhuru?

Soma historia ya Muslim Congress 1962 na 1963 utajifunza historia ya Waislam wa Tanganyika.

Kiongozi wa Waislam alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Unaujua mchango wa Sheikh Hassan bin Ameir katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Umepata kusoma popote!
Hujiulizi kwa nini?

Baada ya uamuzi kupitishwa kuwa EAMWS ivunjwe Sheikh Hassan bin Ameir alikamatwa usiku wa manane akarudishwa Zanzibar na akapigwa marufuku asitie mguu wake Tanganyika.

Soma historia ya Waislam wa Tanganyika utajifunza mengi na sababu kwa nini mimi niliamua lazima historia hii niiandike ijulikane na vizazi vitajavyokuja baadae.
 
Siyo 50/50 kwa wakristo na waislamu. Hi nchi siyo ya wakristo na waislamu peke yao.

Kila mtu ana kwa imani yake awe Rastafarian, budha, mpagani, Hindu n.k haki ya 50 kwa 50
Ndio maana sio sahihi kwa Christians kuhodhi nafasi nyingi kwa 80%,what about the rest?
 
Shinge2,
Unajadili somo usilolijua.

Unaijua historia ya kuvunjwa kwa EAMWS 1968?

Unajua kwa nini ilivunjwa na serikali kuunda BAKWATA?

EAMWS 1968 ilikuwa inajenga shule nchi nzima na jiwe la msingi la Chuo Kikuu liliwekwa na Julius Nyerere.

Waislam wanajenga Chuo Kikuu?
Hili halikubaliki.

Waislam wanajenga shule na wanajenga Chuo Kikuu sisi hatuna Chuo Kikuu!

Hii EAMWS lazima tuivunje kabla haijajenga Chuo Kikuu.

Unaijua historia hii?

EAMWS ikavunjwa na miradi yake yote ya elimu ikaenda na maji.

Je, unawajua waliotenda haya ndani ya serikali ya Tanzania?

Hii ndiyo hatari ya kutaka kujadili mambo usiyoyajua.

Nani kakufunza kuwa Waislam hatukuwa na mipango ya elimu?

Tupiganie uhuru hadi upatikane tusijue tutafanya nini tukishapata uhuru?

Soma historia ya Muslim Congress 1962 na 1963 utajifunza historia ya Waislam wa Tanganyika.

Kiongozi wa Waislam alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Unaujua mchango wa Sheikh Hassan bin Ameir katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Umepata kusoma popote!
Hujiulizi kwa nini?

Baada ya uamuzi kupitishwa kuwa EAMWS ivunjwe Sheikh Hassan bin Ameir alikamatwa usiku wa manane akarudishwa Zanzibar na akapigwa marufuku asitie mguu wake Tanganyika.

Soma historia ya Waislam wa Tanganyika utajifunza mengi na sababu kwa nini mimi niliamua lazima historia hii niiandike ijulikane na vizazi vitajavyokuja baadae.
Naelewa sana. Swali? Kwa hiyo unataka kusema nini mkuu? Pointi yako ni ipi?
 
Shinge2,
Unajadili somo usilolijua.

Unaijua historia ya kuvunjwa kwa EAMWS 1968?

Unajua kwa nini ilivunjwa na serikali kuunda BAKWATA?

EAMWS 1968 ilikuwa inajenga shule nchi nzima na jiwe la msingi la Chuo Kikuu liliwekwa na Julius Nyerere.

Waislam wanajenga Chuo Kikuu?
Hili halikubaliki.

Waislam wanajenga shule na wanajenga Chuo Kikuu sisi hatuna Chuo Kikuu!

Hii EAMWS lazima tuivunje kabla haijajenga Chuo Kikuu.

Unaijua historia hii?

EAMWS ikavunjwa na miradi yake yote ya elimu ikaenda na maji.

Je, unawajua waliotenda haya ndani ya serikali ya Tanzania?

Hii ndiyo hatari ya kutaka kujadili mambo usiyoyajua.

Nani kakufunza kuwa Waislam hatukuwa na mipango ya elimu?

Tupiganie uhuru hadi upatikane tusijue tutafanya nini tukishapata uhuru?

Soma historia ya Muslim Congress 1962 na 1963 utajifunza historia ya Waislam wa Tanganyika.

Kiongozi wa Waislam alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Unaujua mchango wa Sheikh Hassan bin Ameir katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Umepata kusoma popote!
Hujiulizi kwa nini?

Baada ya uamuzi kupitishwa kuwa EAMWS ivunjwe Sheikh Hassan bin Ameir alikamatwa usiku wa manane akarudishwa Zanzibar na akapigwa marufuku asitie mguu wake Tanganyika.

Soma historia ya Waislam wa Tanganyika utajifunza mengi na sababu kwa nini mimi niliamua lazima historia hii niiandike ijulikane na vizazi vitajavyokuja baadae.
Elimu ipi unaongelea mzee?

Hi Boko Haram ya mzungu???
 
Ndio maana sio sahihi kwa Christians kuhodhi nafasi nyingi kwa 80%,what about the rest?
Mkuu hiyo EAMWS baada ya kuhamia Tanganyika ikitokea Mombasa, thumuni lao kuu ilikua ni kueneza Uislam. Na tangu liliopoundwa 1945 pamoja ma kuwa lilikuwa na mawazo ama nia ya kuinua Waislam ndani yake kulikuwa na kitu kilichojificha ambacho hakikuwa wazi. Nyerere akashituka. Si kwa sababu walikuwa na UWEZO wa kufanya uliyoyasema bali ilikuwa ni cover tu ya sinister motive. Mbona huko Mombasa walikoanzia bado Waislamu wengi hawakutaka shule? Tukubaliane kuwa tusitupe lawama kuwa kutosoma kwa Waislam wengi kulisababishwa na Wakristo ama viongozi watawala wa Kikristo. Kwa kuwa umekuwa Marekani kama ulivyosema, najua umekuwa na wamarekani weusi. Lawama zao zote ni kulaumu watu weupe kwa kila matatizo yao. Na ukiangalia kwa makini wengi hawataki kusoma wanataka waishi ktk social Welfare. Nafasi wanapewa nyingi tu ni wavivu. Ndo ilivyo wenzetu hapa Tanzania.
 
Nashukuru sana kwa kueleza kwa kirefu kuhusu uhalali wa CIA Factbook ya idadi ya hizi dini mbili kubwa. Ni kweli kule Kusini wakati wa vita vya Majimaji wengi walikuwa ni Waislam. Lakini unajua ni kwa nini?
Sehemu ya ukanda wa PWANI yote ambako Waarabu walianzia kufanya biashara zao na wenyeji, hilo liliwafanya wengi kuikumbatia dini hii mpya kwao. Ndo hapo mpaka leo wengi ni Waislamu.Hivyo basi Wakristo hawakuwa wengi vile. U kristo uliongezeka baada ya Wamissionary wa CMS na Katoliki kuingia na kuanza kazi yao. Ndo hapo hapo tunakuta Peramiho nk.
Kama nilivyosema Waislamu wengi walikuwa na wako mwambao wa Pwani. Ila Bara Wakristo ni wengi sana. Na hivyo no kusema kuwa CIA Factbook wanatumia data zilizo Factual kulingana na utafiti wao. Hili halina mjadala. Ratio ni 64.1 % Wakristo vs 34.1% Waislam. Kando ya hizo data za Wa Marekani, bado kuna data zingine zinazokubaliana na hizo za Wa Marekani. Maana dunia ni kijiji kwa Karne hii. Nashukuru mkuu.
Kwa nini sasa kipengele cha dini kwenye sensa hamkitaki?.
 
Ndio maana sio sahihi kwa Christians kuhodhi nafasi nyingi kwa 80%,what about the rest?
kama kweli takwimu zako ziko sahihi, nakubaliana nawe, Mimi ni mkristu safi huwa sipendi unafiki wala uzandiki, ni ukweli usiopingika kuwa ndugu zetu waisilamu walikuwa "marginalized" ktk nafasi mbalimbali za Serikalini, iwe na sababu za kihistoria au vyovyote vile kwa sasa sio sio hoja bali jambo la msingi kwa zama hizi za sasa ni kuwepo uwiano ili kujenga Taifa lenye Umoja na Nguvu zaidi.
I

Sisi sote tutakufa lkn Nchi yetu bado itaendelea kuwapo miaka zaidi ya 100 ijayo, hivyo viongozi wetu hawana budi walitambue hilo, tusione aibu wala tusiogope, tuweke uwiano ktk nafasi mbalimbali za Serikalini ili kuimarisha umoja wa Taifa letu, vinginevyo kama tutaendelea kuficha ukweli tutatengeneza tatizo kubwa huko mbele ya safari.
 
Kwa hiyo saivi watu wataajiriwa kwa vigezo pia vya dini na sio uwezo wa mtu? Haya yatakuwa maajabu.

Tukumbuke kuna wasio na dini kabisa. Sasa hawa sijui placement yao itakuwaje.

Ni hatari kuingiza udini kwenye mambo kama ajira.

Dini tuwaachie maaskofu, mashehe na marabi.
 
Kwa hiyo saivi watu wataajiriwa kwa vigezo pia vya dini na sio uwezo wa mtu? Haya yatakuwa maajabu.

Tukumbuke kuna wasio na dini kabisa. Sasa hawa sijui placement yao itakuwaje.

Ni hatari kuingiza udini kwenye mambo kama ajira.

Dini tuwaachie maaskofu, mashehe na marabi.
Hapana wala sio sahihi kuajiri kwa kigezo cha dini isipo kuwa sifa/uwezo na uzoefu,

nadhani kinacho lalamikiwa hapa ni dini moja kuhodhi kwa asilimia kubwa ktk kila taasisi za Serikali...hilo halina ubishi ni kweli sisi wakristu tumehodhi, sasa kifanyike nini? Badala ya kuendelea kujaza watu wa dini moja ni muhimu kuzingatia uwiano ili kubalance vinginevyo italeta shida kama sio sasa baadae.
ni vyema kuuziba huu ufa badala ya kujidanganya na kuendelea kujenga tabaka ambalo litaleta shinda mbeleni.
Tuipende nchi yetu tuijenge sisi sote ndipo kila mmoja atajua thamani ya Nchi yake.
Taifa imara litajengwa na watanzania wote kwa pamoja sio baadhi.
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.

Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!

Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.

Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......

Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.

Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.

Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?

KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!

Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.

Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,

Hivi wewe ulipitia michakato ya ajira au kuna mtu alifanya hiyo michakato kwa niaba yako?

Hetu tuletee mtu humu na taasisi aliyopo ambayo katika mchakato wa ajira/ utumishi hakujaza ni Dini au Kabila gani.

Kama wewe ni kijana wa juzi basi uliza hata Wazee wako.

AU KUNA KITU UNAHOFIA HAPO ULIVYOONA DETAILS ZA UTUMISHI ZINAHITAJIKA
 
Hapana wala sio sahihi kuajiri kwa kigezo cha dini isipo kuwa sifa/uwezo na uzoefu,

nadhani kinacho lalamikiwa hapa ni dini moja kuhodhi kwa asilimia kubwa ktk kila taasisi za Serikali...hilo halina ubishi ni kweli sisi wakristu tumehodhi, sasa kifanyike nini? Badala ya kuendelea kujaza watu wa dini moja ni muhimu kuzingatia uwiano ili kubalance vinginevyo italeta shida kama sio sasa baadae.
ni vyema kuuziba huu ufa badala ya kujidanganya na kuendelea kujenga tabaka ambalo litaleta shinda mbeleni.
Tuipende nchi yetu tuijenge sisi sote ndipo kila mmoja atajua thamani ya Nchi yake.
Taifa imara litajengwa na watanzania wote kwa pamoja sio baadhi.
Je hiyo asilimia kubwa kwa dini moja ulikuwa ni mkakati wa makusudi au imetokea hivyo tu. Hivi mfano unaitangaza nafasi za kazi halafu wanaoomba 80% ni dini moja na ndio wenye sifa zaidi ya wenzake,utasema ngoja ni balance Dini!!!

Tusiipeleke nchi huko. Kuna ambao Kipaumbele Chao sio Elimu Dunia na ndio maana ktk shule za Msingi kuko balanced, lakini unapoanza kwenda juu kundi moja linaanza kupungua na ukifika vyuoni ndio kabisa. Na sio kama hawana uwezo wa kufika huko laa hasha Bali background ktk familia zao inakuwa haichukuliwi kwa uzito Mkubwa.
 
Back
Top Bottom