Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Wakati wa ajira nilijaza kila kitu. Nachozungumza ni hii inafayika kwa watumishi (watu waliopo kazini tayari).
Unaelewa?!
 
Acha uzwazwa.
Nioneshe kifungu chochote cha Katiba, kinachosema Kabila?!
Upambe usikutoe akili.
 
Japo hatujui wanapanga nini lakini kabila na dini sio vitu vya kutukuzwa hata kidogo.
 
Huo uwiano unaoupigania bara mbona huupiganii uwepo Zanzibar?
 
Asiyeona hatari ya kupalilia ukabila, udini,. Hivyo viwili vikimea, hakuna Taifa moja. Hata kidogo!
 
Huo uwiano unaoupigania bara mbona huupiganii uwepo Zanzibar?
Na watu wakianza kuchokonoa haya. Tunajikuta pabaya sana.
Mfano kama mnapigania usawa wa kidini makazini. Huko Zanzibar mnaweza kuuweka huo usawa? Na ukabila je?
Acheni kupalilia mgawanyiko.
 
Hao wakristo waliosoma mwanzo bado tu wako hai? Hawajakufa?

Nyerere alitaifisha shule ili watoto wote wasome, pia alilazimisha wazazi wapeleke watoti shule, tatu alijenga shule kila kijiji na hatua zote hizo tangu zichukuliwe ni takribani miaka 60 - 45 sasa maana yake hata wanufaika wa mwanzo mwanzo wamestaafu au wanakaribia kustaafu. Sasa mtu bado analaumu ukristo na ukoloni? Mimi binafsi nilikulia hapa DSM uswahilini ambako watoto wengi niliocheza nao walikuwa waislamu na wazazi wao hawakuona kabisa umuhimu wa kuhimiza elimu kwa watoto wao, wengine waliwapeleka shule watoto wao kuogopa kufungwa lakini hawakujali kuwahimiza kuzingatia masomo na mara kwa mara waliendekeza utoro, lakini watoto hao hao walikuwa wanasoma madrasa na walikuwa wanabanwa sana kusoma madrasa na walipigwa mno huko madrasa ili waelewe. Kuna watoto kadhaa hawakusoma kabisa primary mfano mmojawapo watoto wa mjumbe wetu wa shina wote hawakugusa darasa hata vidudu ila madrasa walisoma, baadae aliwafundisha kuvua samaki kwani naye alikuwa mvuvi.
 
Wewe ndio huna hoja kabisa yaani mtoto azuiwe kusoma kisa kuna watu wa dini yake huko nyuma walisoma!

Kwanza uelewe kuna koo kibao tena za kikristo hata leo hii hazina mtu aliyefika University . Sio makabila yote yaliyonufaika kwanza shule zilikuwa chache sana enzi hizo. Pili makabila ya wafugaji yote hayakuona umuhimu wa kupeleka watoto shule na makabila hayo baadhi walikuwa wapagani wala sio waislamu.

Inasikitisha sana kila kunapokuwa na rais muislamu chokochoko za kidini zinaibuka.
 
Swali kubwa ni: Inakuwaje hoja za Dini na Kabila zinahusika na mambo ya ajira?
 


Werevu wamenielewa vizuri sana.

Ili kunielewa ni mpaka uzingatie flow of facts tangu Mwanzo lakini ukijakusoma kipande tu cha mchango wa hoja hautaweza kuelewa itabaki kujichoresha tu wewe mwenyewe kwa kuvaba kwako!
 
Ikumbukwe watu hawajazwi tu, unaangaliwa uwezo. Kwa waislamu wengi elimu ya madrasa ni bora kuliko nyingine unategemea nini hapo? Na ni kwa nini tuanze kulinganisha uwiano kwa mizania ya kidini? Tukianza na ukristo na uislam hata waki balance 50/50 kwenye wakristo wataanza kuangalia wa RC, wasabato, walutheri etc kwa waislamu hali napo itakua hivyo hivyo mwisho wa siku tunatengeneza taifa lenye mpasuko kwa misingi ya kidini, Hizi dini sio bora kuliko u raia/uTanzania wetu.
 
Makafiri mna tabu Sana
 
Misaada ya kipesa tunaomba Marekani, Mikopo- Marekani (IMF), Jamani hata hizi Takwimu za kwetu tuvuke masafa mpaka Marekani kujua idadi ya wakristo/waislam wangapi nchini kwetu. Ni aibu!!!!!!!!!!! Kwanini tusijipange na kupata Takwimu zetu wenyewe katika SENSA tunazofanya humu nchini?

Yaani mmarekani akifanya Takwimu juu ya idadi ya waislam na wakristo ni sahihi, Lakini Tanzania kufanya takwimu hizo ni marufuku. Na Takwimu unazihitaji ila hutaki kufanya - Kweli tupo pabaya. Sasa nitafanya kila lililo katika uwezo wangu kuhakikisha kuwa kipengele cha KABILA na DINI kiwepo katika sensa ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…