Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Inashangaza hadi polisi wanatangazaga dini na kabila la mtuhumiwa sielewi zina umuhim gani
 
Huu ni muendelezo wa zile tulizojaza kipindi cha JPM, tukaambiwa ni few selected ndo tumechaguliwa kujaza au ni mpya?

Watu tlikuwa tunasubiria uteuzi!
 
Anataka ajue mkifa iwe rahisi kuwatambikia ... just kidding..
 
Inapendeza sana kuona Sukuma GANG na Mataga ndio mnaishi katika mashaka na hofu kubwa.. Mungu Ametenda..!
 
Acha haya maneno yako. Mfumo Kristo ni upi? Serikali haina dini ila watu wake wana dini.
 
ila wachaga mnapata tabu sana, anyway logeni ccm itoke madarakani ndio itakua nafuu kwenu
Toka nchi ipate uhuru, TANU na CCM ndiyo watawala na Wachagga hatukuwahi kupungukiwa. Bado huko nje ya Tanzania amabapo hamna CCM kuna Wachagga pia.
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.
Mbona kwenye hospital na vitambulisho au polisi na kweti vya kuzaliwa yote hayo yanafanyika ,jipya ni nini?
 
Hii haiko sawa mfano kuna kasi kubwa vijana wengi kuoa au kuolea na makabila mengine. Ni vema tutengeneze kabila liitwalo mtanzania.
Na hii dini ya nini bora wailize magrupu ya damu
Tulitakiwa kama Taifa kuondoa kabisa haya maswali yanayoulizwa kuleta matabaka. Kabila la mtumishi wanalifanyia nini?
 
Sure kitu Cha kawaida Hadi polisi ama hospital unaulizwa.
Sasa si ni katika kukufahamu hauoni hapa mpaka wageni waoiojipachika uraia tutawajua mkuu.
Ila yeye analipigia kelele utadhani watu wake tz hawana ivyo vitambulisho.
Kama kabila linakuonyesha unatokea sehemu gani hapa Tanzania.
Mfano mtu amefariki tunasemaje ama kutangazaje Sasa.
Kuwa mtanzania mwenye jina Nyanungu mangucha amefariki ama ameiba.
Nadhani hata huyu hajasoma fomu wani bailoji Ile classification.
We classify living things up to family or scientific name.
Anza na human being sijui class animalia.
Identification ni muhimu sana.
 
Unawaza kujua Kabila na Dini ya mtu Kwa ajili ya maziko??? Kweli...
You are so myopic. Una upeo mfupi sana.
 
Unawaza kujua Kabila na Dini ya mtu Kwa ajili ya maziko??? Kweli...
You are so myopic. Una upeo mfupi sana.
Yaani unachosema ni just your perception. Sasa kwaniw watanzania hatuna makabila mkuu ama mbona unaogopa Sana kujulikana.
Ni ishu ya kawaida mbona.
Kwani Kuna hatari gani' ya kujulikana kabila lako.
Hauoni cheti Cha kuzaliwa kiasi kikubwa kimekaa katika kukufahamu ama haunacho.
Mbona hujaona suala la mamluki wanaozamia hapa nchini lakini.
Ama umevutiwa na hapo tu kwenye maziko.
Ama mengine yako sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…