Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Kwa hiyo unaamini huu ni mkakati maalumu?
Mfano mkigundua Wakristo ni wengi, mnaanza kubana wao wasiingie kazini, muweke Dini zingine?
Au kama waislamu ni wengi, wazuiwe kuajiriwa, hata kama wao ndio wana sifa zaidi za kielimu, kimafunzo, kiutendaji. Unawaza hivyo?!
 
Unawaza kujua Kabila na Dini ya mtu Kwa ajili ya maziko??? Kweli...
You are so myopic. Una upeo mfupi sana.
Kama vipi tuondoe hata majina ya mikoa wilaya tarafa kata Kijiji mtaa kitongoji uwe inaandikwa kuwa unaishi na umezaliwa Tanzania inatosha ama shida ni Nini lakini.mbona unaogopa.
Hata usipoandika unajulikana
 
Sio lazima kujaza dini kwenye hiyo CV, hauwezi kufanywa chochote kwa kutokua na dini. Pia watu wengi tu wanaishi pamoja na wakiwa na familia bila kuoana na zipo ndoa za kiserikali ambazo sio lazima kuwa na dini.
Hizo ni nadharia tu za ndoa za boma lakini sababu ya uwepo wa ndoa za serikali ni kwa sababu tu wazazi wa Amina wamekataa kufungisha ndoa ya binti yao kwa Peter na hivyo amina peter kuhalalisha ufuska na ukaidi wao kwa wazazi wameamua kwenda kwa baraza la wilaya ili kuruhusiwa waishi kama mama na baba kwa wanao.
Hizi dini na makabila yapo kikanda na wilaya. Mfano Ruvuma Mbinga wakristo na wamatengo, Songea wakristo na wangoni, Namtumbo waisilamu na wandendeule, Tunduru Waisilamu na wayao. Umkute mmatengo muisilamu lazima akupe sababu kwa nn yeye muisilamu hivyo hivyo ukikutana na Myao mkristo lazima akupe sababu ya yy kuwa mkristo. Leo hii ukienda Mbeya wanyakyusa waisilamu wapo ila wachache sana na wanasababu za kuwa huko ila 98% wakristo.
Sababu hizo zinazotolewa kwa sababu tu sio athiri yao kuwa dini hizo. Tanzania dini zipo na makabila yapo na ukitaka idadi nitakupa
 
Mimi nasubiri nione 'dodoso' ya sensa kama itakuwa na kipengele.

Nacheka lakini naopgopa.
 
Ukiteua huku unafikiria dini badala ya uwezo na utayari wa mtu ni hatari sana. Maana badae watu wataenda mbali zaidi hadi kwenye madhejebu. Utwaridhisha watu kweli kwa jinsi hii?
 
Kwani serikali inafanya matambiko? Serikali inaswalisha? Kuna kitu gani cha kiimani au kikabila serikali inafanya kwenye hizo dharula?
Hii acting smart ya baadhi ya watu ni hatari sana. Kama mtakumbuka malumbano haya yalianza wakati wa sensa ya 2012 mpaka, then kipengele hicho kikaondolewa.

Mambo kama haya huanzishwa kwa akili na kwa utaratibu ili kuleta division na kuwadi wa haya yote huwa external people. Africa imeshindwa kujiendeleza kipengele kikubwa kikiwa hicho, Tanzania imekuwa tofauti na mara kadhaa wameshindwa kutuviruga kwasababu ya integration iliyofanya na baba wa taifa na makatazo fulani. Miaka ya nyuma ilikuwa ni kosa hata kutaja kabila publicly nakumbuka nilikemewa nilipotaja kabila la wafugaji kwenye workshop fulani. So sad to see haya yanaanza kuwa introduced slowly and carefully....Mungu isaidie nchi yangu
 
Rais anahusika vipi hapo?
 
Mbona hizi taarifa za dini na kabila hazijaanza leo, labda kama ww ndio umeanza kuziona awamu hii ya sita ila toka muda ukienda polisi au hosipital walikua wanauliza kabila na dini yako
Mtumishi aliyepo kazini, Kabila linakusadia nini? Kupandisha mshahara, au cheo?
 

Ina maana hujui umuhimu wa sherehe za Kichifu na Makabila zinazopigiwa chapuo kila uchao? Mbona kwenye nyumba za wageni unaulizwa Kabila lako na huhoji!
 
Ina maana hujui umuhimu wa sherehe za Kichifu na Makabila zinazopigiwa chapuo kila uchao? Mbona kwenye nyumba za wageni unaulizwa Kabila lako na huhoji!
Tunatakiwa kuondoa haya maswali. Hayana tija, yanatumika isivyopaswa.
 
Mambo mengine ni ya kipumbavu kwa wajinga
Mimi ni mimi niulize mimi na kosa nikifanya ni mimi
Hiyo sheria ya kuuliza majina matatu ya mzazi ipo wapi duniani kama sio kwetu tu

Hawajui kuwa wengine hawawajui wazazi wao?
Wengine hata kabila hawajui unataka adanganye?
Acheni kabisa ujinga huu
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Eti " Trible " sic ni ujinga tu 😡 😡 😡
 
Ninaweza nikakuwekea Waraka wa ndani wa Taasisi moja ya Umma, hiki ni kiambatanisho tu.
Nimeacha hizo nyaraka za Taasisi, zilizosainiwa. Na deadline ya kuwasilisha taarifa hizi ni tarehe 07 February 2022.
Nasita kuweka hizo nyaraka, kulinda watoa taarifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…