Huna hoja za msingi sasa CV ni taarifa za mtu binafsi kwanini ufiche taarifa zako kama dini na kabila jambo ambalo ni muhimu sana., acheni ujinga nyi majinga mafomu mangapi tunajaza Online nchi kibao duniani zinataka kujua dini yako? mbona hukuhoji kuhusu Umri na tarehe za kuzaliwa? maana nao kwa mujibu hoja zako pia unaweza kuleta ubaguzi wa Kiumri.Habari wana JF ..
Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.
Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.
Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!
Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.
Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......
Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.
Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.
Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?
KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!
Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.
Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.
Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,
Polisi wakitukamata mabarabarani zile bondi zao zinakuuliza dini yako na kabila pia kwanini humuulizi kamanda Siro kwanini bondi zenu zina masuala ya makabila?
Nadhani ni hoja dhaifu sana tupa kule kwa dustbin., Kengee
Mbona hoja hii waislamu huwa hawaileti siku zote zinaletwa na wakiristo tu? hofu yenu ni nini hasa nyie wakiristo na dini yenu?
Mimi naiomba Serikali pia kwenye sensa inayokuja pia kuwe na hili suali kuhusu dini ili Nchi ijuwe waislamu wangapi na wakiristo wangapi lakini kama kuna ambao hawana dini pia ni wangapi
Si lazima kila wakati uje hapa na kuandika tu chochote.,