Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.

Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!

Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.

Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......

Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.

Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.

Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?

KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!

Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.

Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,

Huna hoja za msingi sasa CV ni taarifa za mtu binafsi kwanini ufiche taarifa zako kama dini na kabila jambo ambalo ni muhimu sana., acheni ujinga nyi majinga mafomu mangapi tunajaza Online nchi kibao duniani zinataka kujua dini yako? mbona hukuhoji kuhusu Umri na tarehe za kuzaliwa? maana nao kwa mujibu hoja zako pia unaweza kuleta ubaguzi wa Kiumri.

Polisi wakitukamata mabarabarani zile bondi zao zinakuuliza dini yako na kabila pia kwanini humuulizi kamanda Siro kwanini bondi zenu zina masuala ya makabila?

Nadhani ni hoja dhaifu sana tupa kule kwa dustbin., Kengee

Mbona hoja hii waislamu huwa hawaileti siku zote zinaletwa na wakiristo tu? hofu yenu ni nini hasa nyie wakiristo na dini yenu?

Mimi naiomba Serikali pia kwenye sensa inayokuja pia kuwe na hili suali kuhusu dini ili Nchi ijuwe waislamu wangapi na wakiristo wangapi lakini kama kuna ambao hawana dini pia ni wangapi

Si lazima kila wakati uje hapa na kuandika tu chochote.,
 
Wakristo Wana chuki Sana na Waislamu,Cha ajabu Waislamu Wala hawawachukii wakristo!

Magufuli kweli alikuwa mdini na mkabila wakutisha,lakini Hawa kenge hatukusikia wakiliongelea humu mitandaoni,

Cha ajabu hizo chuki zao kwa viongozi wenye utu wa kiislamu,inawaongezea umri mrefu na afya tele
Acha ujinga wako! Wakristo ulishawahi kuwakuta wanahangaika na kujadili waislam? Nyingi ndo kila siku mnafundishwa chuki juu ya wakristo!
 
Moja,
Kazi hazijawahi kusimama Kwa sababu ya watu kwenda kuabudu.

Pili,
Hakuna packages za kidini, ktk utumishi wa Umma, Hapa mnataka kujenga kaburi ambalo hata urefu wake hamlijui.

Tatu,
Serikali haihusiki na mirathi na mambo ya maziko ya watumishi, haihusiki kabisa na hizo taratibu. Nakupa elimu kwa sababu inaonekana huna ufahamu na ofisi za umma.

Nne,
Hilo la malalamiko mbalimbali, aangalie ni wapi wanalalamika na aende huko kuhoji. Sio utumishi nchi nzima kujazishwa hivi. Na haielezi lengo ni nini
Kwani wewe unapata shida gani hizo taarifa zikichukuliwa? - Kwa nini huoni ajabu taarifa za jinsia kuchukuliwa, wewe unadhani jinsia yako inaisadia nini serikali?

Lengo la Taarifa hizi ni ili serikali iweze kuondoa ubaguzi katika utumishi wa umma, au hujui kuwa rais ameapa kutimiza majukumu yake bila upendeleo wa dini, kabila au jinsia? —Hizi data zinasaidia serikali kusolve ishu ya inequalities katika utumishi wa umma, ili keki ya Taifa isiliwe na watu wa mrengo mmoja, ni hatarisana kama inaonekana watu wa dini moja ndo wana fursa halafu wengine hola
 
Ndugu yangu, jamaa anasema tuache kazi apate kazi, sijui anamaanisha nini .

Leo Kila sehemu tukianza kuulizana Dini na Kabila, tutakuwa na Taifa kweli.!
Kuna wengine wanasema et, unaweza ukaweka Dash, kwa maana ukaacha wazi sehmu ya kabila na dini. Hawajui kwamba huyu mtu anayetaka kuwatambua waatu kwa makabila na dini zao, hiyo dash au usipojaza uakuwa unaongezea ama kupunguza nini upande upi. Na hujui hiyo dash ina maanisha nini katika kutimiza agenda zake za kidini na kikabila anazotaka kuzisimika.
 
Kwani wewe unapata shida gani hizo taarifa zikichukuliwa? - Kwa nini huoni ajabu taarifa za jinsia kuchukuliwa, wewe unadhani jinsia yako inaisadia nini serikali?

Lengo la Taarifa hizi ni ili serikali iweze kuondoa ubaguzi katika utumishi wa umma, au hujui kuwa rais ameapa kutimiza majukumu yake bila upendeleo wa dini, kabila au jinsia? —Hizi data zinasaidia serikali kusolve ishu ya inequalities katika utumishi wa umma, ili keki ya Taifa isiliwe na watu wa mrengo mmoja, ni hatarisana kama inaonekana watu wa dini moja ndo wana fursa halafu wengine hola
Dini au kabila ni maumbile kwamba mtu hawezi kujibadilisha na hvyo anahitaji kuzingatiwa kwa jinsi alivyo? Huo ndio upumbavu tunaousema wa kuwa na watu wasio na eliimu sahihi wala exposure. Magari ya ukabila na udini yalishaondolewa barabarani. Tuko kwenye globalization error halafu ninyi maaanza kutafuta ujinga wa kuturudisha kule dunia ilishaatoka. Pumbavu sana.
 
Hakuna kitu kinachoitwa 'mfumo kristu' kwenye hili taifa........hizo ni kampeni za kueneza chuki, fitina na hila ovu dhidi ya kundi fulani la ki-imani.
Tena
Hii acting smart ya baadhi ya watu ni hatari sana. Kama mtakumbuka malumbano haya yalianza wakati wa sensa ya 2012 mpaka, then kipengele hicho kikaondolewa.

Mambo kama haya huanzishwa kwa akili na kwa utaratibu ili kuleta division na kuwadi wa haya yote huwa external people. Africa imeshindwa kujiendeleza kipengele kikubwa kikiwa hicho, Tanzania imekuwa tofauti na mara kadhaa wameshindwa kutuviruga kwasababu ya integration iliyofanya na baba wa taifa na makatazo fulani. Miaka ya nyuma ilikuwa ni kosa hata kutaja kabila publicly nakumbuka nilikemewa nilipotaja kabila la wafugaji kwenye workshop fulani. So sad to see haya yanaanza kuwa introduced slowly and carefully....Mungu isaidie nchi yangu
Huyu 2025 inabidi aende likizo. Atatuharibia undugu wetu tuliojiwekea kwa ujinga wa siasa za kishamba.
 
Dini au kabila ni maumbile kwamba mtu hawezi kujibadilisha na hvyo anahitaji kuzingatiwa kwa jinsi alivyo? Huo ndio upumbavu tunaousema wa kuwa na watu wasio na eliimu sahihi wala exposure. Magari ya ukabila na udini yalishaondolewa barabarani. Tuko kwenye globalization error halafu ninyi maaanza kutafuta ujinga wa kuturudisha kule dunia ilishaatoka. Pumbavu sana.
Data na information yoyote ya mambo ya kijamii ni muhimu kwa serikali. Inasaidia serikali kwenye mambo mengi ikiwemo affirmative action ikibidi au kwenye kuzuia udini na ukabila kwenye ajira.
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.

Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!

Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.

Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......

Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.

Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.

Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?

KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!

Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.

Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,

Du hata kwenye sensa kipengele cha dini na kabila halipo,kwa kuamini Tanzania haina udini na ukabila, hata ukitaka kufanya tafiti mojawapo ya masharti ya kupitishwa kwa dodoso la utafiti ni kutokuweka kipengele cha dini na kabila.
 
Waandishi wa habari nchi hii hopeless kabisa zingekuwa nchi zingine zilizoendelea wangekuwa wangemshukia kama mwewe kuhoji waziri wa fedha au Raisi

Naomba BBC wamhoji raisi ukabila na udini wa mini na motive ya hii kitu ni nini?

BBC hojini Rais hilo
 
Nadhani hili sio jipya na ni usumbufu tu kwani mtu anapoajiriwa, taarifa hizo karibu zote hutakiwa kuzijaza sasa sijui kwanini wanaziomba upya.

Hata Polisi wanapochukua taarifa za wahalifu, huchukua taarifa zikiwemo za kabila la mtu na sijui ni kwanini.
Labda wanahisi wengine wamebadiri DINI
 
Zamani walikuwa wanawaondoa watu wanaotaka kuivuruga ccm, kwa kuwaita dodoma, sasa hawa wanaoplan mazito kuliko kuigusa ccm nadhani ni kuwashughulikia fasta zaidi, kwa wale TISS wazalendo maana hata TISS imeshavamiwa bila shaka sasa mwisho wa siku nahisi kila eneo litatekwa na hawa wavuruga nchi,
Nahisi kama kuna kundi linatakiwa kuwa eliminated kabisa ndani ya nchi. Kwa kuwa nia ya kukusanya tawkimu kwa majina binafsi haijawekwa wazi, ninahisi kama sasa wasiotakiwa wataanza kuwa replaced, frustrated ama sidelined na kuawa kabisa ili agenda inayofukuziwa ifikiwe.

Huu ni wasiwasi mkubwa unaosababishwa na haya mambo ya ajabu yanayotokea katika kipindi cha uharifu ufiohojiwa wala kutolewa maelezo.
Ninapata wasiwasi na usalama wa hao kundi lililo kwenye black list.
 
Hiyo statement na maelezo yote ya chini yanazidi kubainisha kuwa kabila is no longer and shouldn't be a means to determine a ruling in any dimensions. Niliuelewa vizuri na given nilipo nimeamka masaa mengi sana yaliyopita. Kimsingi hiyo statement haina msingi wowote wa kutetea swali la kutaka kujua kabila la mtu katika mfumo wa kufanya maamuzi (mahakamani) kwa sababu nilizoeleza. Kama inafanyika ni kutokana na udhaifu wetu wa mifumo ya haki, uchumi, Siasa na uongozi. Period.
Huku kwenye taaluma yetu hiyo ni criteria ingawa it is qualified not absolute. Na imeisaidia sana Mahakama kufikia maamuzi ya haki mara kadhaa.

Nikuongezee mfano mwingine wa kwenye kesi za udhalilishaji (defamation). Kuna kabila mtu akikutamkia neno flani linakuwa ni udhalilishaji kwa kabila hilo, lakini kwa kabila lingine ni utani. Kwahiyo wafanya maamuzi wa Mahakama wanapaswa kulizingatia hili kabla ya kufanya maamuzi, vinginevyo watu watawajibishwa/kutowajibishwa kimakosa halafu mrudi humu kulalamika.

Hivyo ni lazima uelewe kwamba kwenye baadhi ya maeneo ni lazima ubainishe kabila lako kwa dhumuni jema kabisa ambalo huenda likakusaidia wewe mwenyewe.
 
kuna kale ka msemo ukielimisha mwanamke, umeelimisha jamii...nadhani kwa tz inatakiwa kafutwe
 
Kwenye rekodi za serikali huwa hakuna dini wala kabila la mtu. Nyerere aliondoa hiyo zamani sana wakati taifa bado ni changa, na hata marais waislamu Mwinyi na Kikwete hawakuirudisha. Sasa tumepata mwislamu kamili ndiye anayeyaleta. Katika teuzi wake naona kipengele cha dini kimekuwa ni cha muhimu sana kwake; na ili kukihalalisha ndiyo maana ameunganisha na ukabila akianzia na kurudisha uchifu.

View attachment 2095774



Kama tuvoyapinga huko serikali tuyapinge vile vile kwenye sekta binafsi...
Taarifa nyeti kama umri, jinsia, dini, kabila, makazi, pakuzaliwa, hali ya ndoa, taarifa za wazazi, mtu wa karibu... zote hizo zinatakiwa kuwa hiyari na siri.
Na ukizitoa ni vizuri kujiridhisha zitatumikaje...
 
Nahisi kama kuna kundi linatakiwa kuwa eliminated kabisa ndani ya nchi. Kwa kuwa nia ya kukusanya tawkimu kwa majina binafsi haijawekwa wazi, ninahisi kama sasa wasiotakiwa wataanza kuwa replaced, frustrated ama sidelined na kuawa kabisa ili agenda inayofukuziwa ifikiwe.

Huu ni wasiwasi mkubwa unaosababishwa na haya mambo ya ajabu yanayotokea katika kipindi cha uharifu ufiohojiwa wala kutolewa maelezo.
Ninapata wasiwasi na usalama wa hao kundi lililo kwenye black list.
Angalia baraza la mawaziri juzi, waliopigwa chini wote ni wakristu na replacement yake utapata jibu
 
Kwenye rekodi za serikali huwa hakuna dini wala kabila la mtu. Nyerere aliondoa hiyo zamani sana wakati taifa bado ni changa, na hata marais waislamu Mwinyi na Kikwete hawakuirudisha. Sasa tumepata mwislamu kamili ndiye anayeyaleta. Katika teuzi wake naona kipengele cha dini kimekuwa ni cha muhimu sana kwake; na ili kukihalalisha ndiyo maana ameunganisha na ukabila akianzia na kurudisha uchifu.

View attachment 2095774


Kwa uzoefu wangu hizi taarifa sio mpya kwenye utumishi wa umma, unapoajiriwa kwa mara ya kwanza taarifa hizo huwa zinachukuliwa kupitia fomu flani ambayo mtumishi huwa anajaza. Pia, kama upo Wizarani na umefanyiwa vetting, taarifa za ajabu ajabu kama hizo huhitajika ikiwemo hadi details za wakwe zako na dada na kaka wa mkeo. Mimi kwangu cha kushangaza, kwanini wanazitaka hivi sasa wakati tayari taarifa hizo zote wanazo? Ni uvivu wa kupekua nyaraka au?
 
Wakristo mbona mna hofu Sana,au kwakuwa mmejazana kwenye maofisi mnajishtukia, muacheni Rais apige kazi,hizi kelele mngezipiga kipindi kile Cha dikteta
Waislamu akishika uraisi muislamu mwenzao wanamsumbua sana Raisi kwa hoja za kuokoteza

Mfano angalia Mwinyi alipokuwa Raisi akamuweka Kighoma Malima mwislamu mwenzie kuwa waziri wa Elimu Malima akasema ohhh waislamu shule zao zinafeli sana sababu wasahihishaji mfumo kristu wakiona mtoto jina LA kiislamu wanamfelisha kwa makusudi zitumike namba tu za mitihani sio majina .Wakristo wakakubali Leo hii shule za kiislamu bado zinashika mkia wanafeli hasa Likiwemo somo lao LA Islam Knowledge linalofundishwa na ma ustaadhi na kusahihishwa na maustaadhi wenyewe

Leo wanataka Dini na kabila viwekwe wazi isiwe siri !!!
 
Back
Top Bottom