mkalamo
JF-Expert Member
- Sep 7, 2013
- 340
- 359
Ikiwa kesho tarehe 25 ndiyo siku ya Tume ya Uchaguzi kuwathibitisha wagombea wa nafasi ya Urais, Ubunge na Udiwani kwa vyama mbali mbali nchini, hali ya ajira ya watumishi wa Umma waliojitosa katika kinyang'anyiro hicho imebaki kuwa ni kitendawili kisichokuwa na mteguaji.
Kwa mujibu wa taarifa zilizowasilishwa kwa maafisa utumishi katika halmashauri mbali mbali nchini, pamoja na taasisi za umma, wale wote waliogombea pasipo kujali kama waliteuliwa na vyama vyao au la wanatakiwa waandike barua upya ya kuomba kurejea kazini huku wakisubiri majibu kama wataruhusiwa kuendelea na kazi au ndiyo mwisho wa ajira zao.
Agizo hilo linawahusu wote waliogombea kwa nafasi ya kata, jimbo na viti maalum ambayo mpaka sasa vyama kwa asilimia 90 zimeshawatambulisha wagombea wao wa nafasi hizo pamoja na wale wa Viti Maalum.
Mpaka sasa wengi wa wagombea walioshindwa kupitishwa na vyama vyao wameshindwa kurejea kazini wakisubiri hatma ya Agost 25
Kwa mujibu wa taarifa zilizowasilishwa kwa maafisa utumishi katika halmashauri mbali mbali nchini, pamoja na taasisi za umma, wale wote waliogombea pasipo kujali kama waliteuliwa na vyama vyao au la wanatakiwa waandike barua upya ya kuomba kurejea kazini huku wakisubiri majibu kama wataruhusiwa kuendelea na kazi au ndiyo mwisho wa ajira zao.
Agizo hilo linawahusu wote waliogombea kwa nafasi ya kata, jimbo na viti maalum ambayo mpaka sasa vyama kwa asilimia 90 zimeshawatambulisha wagombea wao wa nafasi hizo pamoja na wale wa Viti Maalum.
Mpaka sasa wengi wa wagombea walioshindwa kupitishwa na vyama vyao wameshindwa kurejea kazini wakisubiri hatma ya Agost 25