Tetesi: Watumishi waliogombea Ubunge roho mkononi

Tetesi: Watumishi waliogombea Ubunge roho mkononi

Leo tukifuata hiki wanachofanyiwa hawa watumishi, nadhani hatutakuwa na mwanasiasa hata mmoja.

Tutaanza kumfuta Magufuli kwenye hii nafasi yake, maana ilitokana na yeye kuwa mtumishi wa umma. Majaliwa naye hatabaki salama.
 
mkalamo,

Watumishi wa Umma waliokosa kuteuliwa na ccm wamekosa mishahara miezi miwili,wamekosa nafasi zao za kazi waliokuwa, wako majumbani hawajui hatima Yao, Sasa wale waliopitishwa kugombea wanawaomba Wasaidie Tena kufanya kampeni ili waweze kushinda Oct,28. Watumishi hai Ni zaidi ya 7,000 na wanaogopa hata kuvaa kofia na mashati ya CCM. Na Bila kuwatumia waliokosa Kura za maoni Hali za walioteuliwa kisiasa Ni mbaya kwani waliokosa mishahara wameonekana wasaliti ndani ya jamii na wafanyakazi wenzao.

Kwa mantiki hiyo tunaomba wale wote waliokosa utumishi na mishahara Yao waachane na kuwafanyia kampeni na waonane kwenye box la Kura October 28.
 
Nawapa pole zao. Baada ya kukosa mishahara miezi miwili bado hawajui hatima yao. Sikuona kosa lao kujaribu bahati zao kisiasa kama Watanzania wengine waliotia nia mwaka huu. Kama kungekuwa na waraka wa kuwakumbushia / kuwaonya wasijitumbukize huko (Endapo wangekuwa wanavunja sheria) , wengi wao wasingethubutu kutia nia ila kwa sababu ilizoeleka chaguzi zilizopita hakukuwa na tatizo baada ya kuomba ruhusa, nao wakajaribu bahati zao.

Siasa inalipa nchi hii kuliko taaluma yeyote ile ndiyo maana mwamko wa watendaji wa Serikali kwa ngazi mbalimbali kutimkia huko ni mkubwa sana.

Lakini kwanini haya yamejitokeza mwaka huu? Sheria ya Utumishi wa Umma inasemaje? Je watumishi wa Umma waliotia nia walifuata sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma? Mbona wanasiasa wengi wenye majina makubwa walikuwa watumishi wa umma na wakabadili mwelekeo na kujiunga na siasa, waliwezeshwa na sheria gani?

Naomba nisaidiwe na wataalamu wa sheria za kazi ili kukuza ufahamu wangu.

Walionywa na waraka!
 
Hakuna kitu kibaya kama kuwa maskini wa akili, unashangilia wenzako kufukuzwa kazi badala ya kusikitika na kushauri, sisi maskini huwa tunaombea aliyenacho akose tukose wote badala ya kuomba uwe kama yeye.
Wakati wengine wanasota na yeye pia alikuwa anashangilia
 
Back
Top Bottom