Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wewe ni mjinga kabisa! nimesema mwanzoni kabisa kuwa jamaa mauzo yake sio chini ya 1.5 million nikasema ukitoa gharama ya manunuzi ya vitu vyote faida anapata zaidi ya hiyo pesa laki 2 yenu.Kifupi wahi tu mirembe hospitali ya vichaa Kwa kuandika vitu vya kuota .Eti nipige hesabu uchwara.Nitapigaje hesabu wakati huhaweka bei za vitu .Kuwa mfano hizo boda boda zinatumia mafuta shilingi ngapi? Mkaa bei Gani na anatumia kiasi Gani Kwa siku,Hao kuku na viazi, ,kabichi nk ananunua shilingi ngapi na kuuza anauza shilingi ngapi Kwa sahani Kwa wateja wangapi Kwa siku?
Hujaweka hizo bei kwenye maelezo Yako uchwara
Kifupi wahi hospitali ya mirembe kichaa Huwa kinaanza hivyo hivyo mtu unaanza kuwaza vitu hewa visivyokuwepo
Hawa hawajui kinachoendelea huko MitaaniEndeleeni kushangaa tu watu wanapiga pesa! kuna jamaa pale Mwanza Uhuru dampo anauza chips mauzo ya million 1.5 kwa siku day and night sasa kwa mauzo hayo anakosaje hiyo faida kwa mfano.
Kwa maandilizi hayo na hizo pilikapilika jamaa anapiga pesa zaidi ya wakuu wa mikoa.Acha ubishi wa kijinga wewe! unapajua Uhuru dampo kwanza? yule mwamba chips haziishi pale unazikuta kwenye kabati kama chapati.
1.Anawafanyakazi wanashift mchana na usiku.
2.kuna watu kazi yao ni kumenya viazi tu.
3.kuna watu kazi yao ni kuandaa Mishikaki tu.
4.kuna watu kazi yao ni kuandaa kuku tu.
5.kuna watu kazi yao ni kukaanga viazi tu.
6.kuna watu kazi yao ni kuchoma chips tu.
7.kuna mtu kazi yake ni kuhudumia vinywaji tu.
8.Ana watu 3 kazi yao ni kupokea pesa tu.
9.Anabajaji 2 zimepaki kwaajili ya kufata mkaa stoo ukiisha.
Tembea uone acha ubishi wa hovyo! yule jamaa ananyumba 3 amejenga, watu wanachukua take away pale kama hawana akili nzuri.
Pesa gani wanazotumia hovyo wakati wengi wanaishi kwa madeniKwa sababu mnatumia pesa hovyo Kwa kuona zipo tuu mwisho wa mwezi.
Sawa na wavuvi au wachimbaji.
Sio kweli, hizi ni fikra za kiswahili.Kwenye maisha Cha muhimu mtu apatacho na maisha yake kuridhika upate elfu hamsini Kwa mwezi au bilioni Kwa mwezi
Kwani wazungu wote ni wajasiriamali hakuna walioajiriwa?Sio kweli, hizi ni fikra za kiswahili.
Elimu yake haijamsaidia, tungepata mamilionea wa kutosha kwa kuuza ugali nyama mtaani.Weeee bwana! Unajua faida ya laki 2 hadi 3 kwa siku? Nenda ukalale!
Hizo hizo wanazolipwaPesa gani wanazotumia hovyo wakati wengi wanaishi kwa madeni
Jamaa anachukulia mauzo yote kwa siku ndio faida, bila shaka madeni ya vikoba yanamchanganya hivyo anaona kila biashara ina faida lukukiNimeshanga hata mimi
Ova
Tatizo wanajiingiza kwenye ujasiliamali kifarafara..,Kuna mwalimu mmoja hapa kafungua duka la spare parts za pikipiki karibu kabisa na duka langu linalouza hizohizo spare parts.., huyu anachofanya ni kuharibu biashara kwa sababu Bei za spare zinashuka sana na ninauza kwa panick,Tena mbaya zaidi mtumishi ukijitahidi kuwa mjasiriamali unarudishwa nyuma hatua buku moja hata kwa uchawi mpaka uchakae
Mpaka imekuwa masihara Sasa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Kuna jamaa anauza miguu ya kuku na vichwa huku mbagala anaingiza laki sita kwa siku