Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,677
Ni nadra sana kumkuta Mtanzania wa visiwa vya Zanzibar akijitambulisha kwamba yeye ni Mtanzania.
Nimefanya utafiti wangu usio rasmi kuhusu hili suala. Ukimkuta Mzanzibari nje ya nchi, halafu ukamuuliza ikiwa yeye ni mtanzania, mara nyingi utapokea jibu kwamba 'Mimi ni Mzanzibari'.
Yaani ni kwamba wazanzibari wengi huwa wanajaribu kwa namna yeyote, kuukwepa utanzania na wengi hawapendi kuitwa watanzania. Kwa waliotembea uarabuni mtathibitisha hili. Yaani ukitaka ukosane na mzanzibari huko arabuni, basi we muite mtanzania.
Inaonekana ni kama wazanzibari wanahisi tayari wapo daraja fulani hivi la juu, hivo kitu utanzania ni kuwashusha hadhi.
Hili jambo ni moja ya mambo ambayo nahisi yanahitaji uwepo wa serikali tatu, maana huko tunapoenda, itafika mahali hata sisi wa bara tutatamani kuitwa watanganyika.
Mi binafsi naanza kuchukia jina Tanzania. Maana yake sioni faida ya huu muungano ambao, kuna upande unautweza wazi wazi.
Nimefanya utafiti wangu usio rasmi kuhusu hili suala. Ukimkuta Mzanzibari nje ya nchi, halafu ukamuuliza ikiwa yeye ni mtanzania, mara nyingi utapokea jibu kwamba 'Mimi ni Mzanzibari'.
Yaani ni kwamba wazanzibari wengi huwa wanajaribu kwa namna yeyote, kuukwepa utanzania na wengi hawapendi kuitwa watanzania. Kwa waliotembea uarabuni mtathibitisha hili. Yaani ukitaka ukosane na mzanzibari huko arabuni, basi we muite mtanzania.
Inaonekana ni kama wazanzibari wanahisi tayari wapo daraja fulani hivi la juu, hivo kitu utanzania ni kuwashusha hadhi.
Hili jambo ni moja ya mambo ambayo nahisi yanahitaji uwepo wa serikali tatu, maana huko tunapoenda, itafika mahali hata sisi wa bara tutatamani kuitwa watanganyika.
Mi binafsi naanza kuchukia jina Tanzania. Maana yake sioni faida ya huu muungano ambao, kuna upande unautweza wazi wazi.