Wazazi, acheni kuwapotezea muda watoto wa kiume kuwafundisha kupika!

Mwanangu nitamfundisha kupika hakuna namna.
 
How did you ditect that's a weak while you are the weakest? Remember that, " the one who knows he knows not he knows"
 
Wanaopika kwenye mahoteli ni akina nani?
 
Mwanangu nitamfundisha kupika hakuna namna.
Humu kuna wachangiaji wengi ni kula kulala tena wengine wanaishi kwa shemeji zao hamna walijuwalo.

Kwa mfano mimi binafsi hawa tunaowaita wadada wa kazi wamenisumbuwa sana achilia mbali kuwabadirisha au anakuja huyu anakaa wiki anataka kuondoka kumbe ulitumioa tu kumleta mjini na saa nyingine unatuma nauli unaliwa vilevile, sasa nimeamuwa hivi.

Watoto wakubwa wako boarding, mtoto mdogo yupo day lakini anashinda shuleni anarudi jioni kabisa kwahiyo nyumbani tunapika usiku tu au nanunuwa take away hakuna kupika.

Sihitaji wala sifikilii kuleta house girl, usafi ni mara moja kwa wiki anakuja dada anafuwa anaosha vyombo anapiga deki nyumba namlipa cash yake anatambaa, siku za kawaida kufagia nyumba hakunishindi nafagia mimi au wife yeyote atakayehisi kuna michanga ndani.

Kwahiyo kwangu wala hatuhitaji mpishi na wakubwa wakirudi likizo wanapika wenyewe mchana au mama yao kabla ya kwenda job akiamka mapema awapikie ubwabwa full suti, binafsi kama nakuwa home vyakula vyangu ni michemsho tu wala havina mambo mengi ni nyama au samaki viazi ndizi na viungo unachanganya pamoja unakadiria maji, unaweka chumvi unatia na mafuta machache unawasha gesi ngoma inajipika yenyewe, hivi hapo shida iko wapi? Ukiona mimi nanunuwa chips ujuwe ni dharura tena ni usiku inanibidu tu.
 
!!!.Napita
 
Mwanaume mtu mzima anaweza kupika bila mafundisho ya utotoni, hapo ndo utajua kuwa kumfundisha nyumbani mtoto wa kiume Ni kupoteza muda
Me too nilijikuta napika tu na sikuwahi funzwa.
 
Safi sana. Kuna watu hawapa wanaona kujifunza kupika ni kama itawaondolea uanaume wao kitu ambacho naona si kweli. Nawaza kijana wa kiume leo hii akianza kujitegemea na hajui kupika ina mana atakua anakula migahawan siku zote? Anyways tunaambiwa kila mtu na chaguo lake.
 
Si kila chakula unaweza kupata kwenye migahawa yetu ya mitaani.

Kuna muda una choice zako unataka ule nini, tena hawa wajinga wanaotaka kupotosha dhana hii unaweza kukuta jitu limeshinda njaa, kwenye fliji kuna kuku mbichi au nyama mbichi, tangawizi ipo, vitunguu swaumu vipo, limao lipo jiko lagesi na umeme lenye oven chini lipo lakini hajui hata kuhoka nyama au kuku kwenye oven wakati inajiivisha yenyewe tu, unachemsha ndizi pembeni bonge la msosi. Sasa vitu rahisi kama hivi hawa watoto hawataki wafundishwe ni msiba kwakweli.

Sasa wazungu wametengeza mpaka rice cooker sufuria la umeme wali unajipika wenyewe, yani kukadiria maji tu na chumvi na mafuta kisha baada ya dakika kadhaa kugeuzageuza hapo shida iko wapi?

Basi watoto wa hivi hata kuandaa matunda hawatoweza, italeta tikiti maji na avocado na bado mtu atashindwa kuandaa kwenye sahani, mimi mtoto wa hivyo labda atumie ubini wa mama yake lakini siyo jina langu.
 
Wengi wanaokushambulia labda ni kwa sababu umewaita shosti, of which has nothing to dilute the truth…. hoja yako ni ya msingi na inahitaji watu timamu tu [sio wingi] kukuunga mkono.

Mwanamme huwezi kusimama popote ukajivunia ujuzi wa kupika, labda kama ni kazi yako rasmi inayokupa maisha…. sasa ya nini kukomalia?

Ukiwa na akili timamu tu, suala la kupika ni kitu kidogo mno ambacho haipaswi kuwa ishu ya kufundishwa tangu utotoni…. kuna mambo mengi ya msingi kwa mtoto wa kiume kujifunza lakini sio UPISHI.
 
Twende taratibu nione kama hizo akili unazo kweli, unaelewa mshahara wa Chef hotelini ni kiasi gani?

Kwamba unataka kutuaminisha wanaosomea hotel management ni wapuuzi watupu na wanatowa huduma za catering hamnazo?
 
Wenye akili kama zako chuo hulazimika kuishi na mademu, akiachana na huyu leo kesho ana mwingine ili apikiwe na kufuliwa. Kushiriki kutoa mimba ndio wanaongoza, kuoa ile sogea tukae wote ni wao, kuteswa na mapenzi ni wao.

Mimi sikufundishwa kupika ila kuna muda house maid aliondoka nikawa narudi siku nyingine sikuti chakula. Bites huwa sioni kama ni mlo nikajifunza kupika kwa siri nikajua na siku moja ndio nikapika cha watu wengi wakashangaa.

Kila kiumbe hai kina sifa kuu 7 (characteristics) ambazo ni lazima uzitimize kuishi. Nutrition, respiration, movement, reproduction, sensitivity, growth na excretion. Hizo zote bila kufundishwa unaweza jua ila ukifundishwa si vibaya. Wanyama hufundisha watoto wao skills za kuwinda ambazo tiyari zishaonekana ni sahihi.

Usiseme ni advantage ya mwanamke kujua kupika labda useme ukoo wenu wanaume huwa wanakula mawe. Kujua kupika hakupunguzi wala kuondoa lolote kwa mwanaume, sio jambo la ajabu maana hata kula sio ajabu wala siri. Viungo vinavyotumika kupika viko jinsia zote, hatutumii ovaries kubandika sufuria. Wewe unachukulia kupika kama kunyonyesha
 
Humu JF kuna kila aina ya watu usikute mtoa mada sasa hivi yupo anasugua masufuria
 
Kwani kuna kufundishwa kupika ndio kutakufanya usiwe mwanaume???mbona wapishi wengi kwenye ma hoteli ni wanaume mimi mwenyewe ni mpishi na nnalipwa laki 9 kwa kazi hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…