Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Lupamba's grandson

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2015
Posts
1,232
Reaction score
1,196
Wazazi na walezi,

Tembelea watoto wako wanaosoma vyuo!

Hasa hawa walioenda ngazi ya cheti baada ya kumaliza kidato cha nne, wengine wameoa na kuolewa!
Binti haingii darasani, anafua na kupika kwa kijana waliyekutana naye chuoni.

Kuna ambao pesa ya ada hajalipa anahudumia "mke"! Unaweza fikiri yupo masomoni kumbe analea mke na mtoto.

Kuna ambao wamefukuzwa vyuo au kuacha masomo kwasababu mbalimbali, mzazi usipofuatilia hautajua.

Wengi wanaoenda vyuo vya kati au vyuo vikuu baada ya kidato cha nne wana umri mdogo sana, hawajafundishwa namna ya kutumia "uhuru" wa chuo, huko hakuna mwalimu wa darasa au mwalimu wa nidhamu. Haulizwi kwanini hajaingia darasani, au hajafanya mtihani, ni matokeo ya mwisho yatakayoamua.

Sasa mzazi usipoyajua haya unaweza kushangazwa na hayo matokeo ya mwisho, na inaweza kuwa tayari umeshachelewa.

Siku hizi wahitimu wengi wa kidato cha nne hawataki kwenda kidato cha tano, wanataka kwenda vyuo, ukiacha sababu ya kutaka kupata ujuzi na ajira kwa haraka, wengi wanataka kuwa huru. Wanasema vyuoni hakuna mambo ya kuvaa sare wala kupangiwa vitu vya kufanya, na kingine wanafurahia pesa ya matumizi anayopewa chuo ni kubwa kuliko akienda sekondari.

Sasa huu uhuru na pesa ya matumizi ukivichanganya na usipokuwa na akili njema, kuna kitu kinaitwa "majuto ni mjukuu"!

MZAZI TIMIZA WAJIBU WAKO!

Mwl.Doris Mboma!
 
Yaani mkuu nikweli hapa nilipo naona vijana wameona kabisaaa Hadi najiuliza wazazi wanayajua haya yanayoendelea kwa vijana wao. Dah hali inatisha
Nilipomaliza chuo ndio nikaja shangaa ile lifestyle nilikuwa naishi. Sahivi naenda nawatazama vilevile wanavyofanya nashangaa ilikuwaje nilikuwa hivi. Unakuta vidada na jumpsuits vinatembea vimeshikana na boyfriends zao mitaani.

Niko na girlfriend nilipokuwa Advance yeye alikuwa O level yuko mkoa ila huwa anakuja tunakaa bila wasiwasi, muda anapigia mama au baba yake natulia bila kelele. Tunapanga safari, namtembelea ananitembelea tunazurua hadi mikoani. Akifunga anapitia kwangu na akifungua chuo anapitia kwangu.

Kitu kingine mzazi ogopa mfano wewe unaishi Moshi, mwanao anakwambia amepata field Mwanza wakati anasomea Dar, uongo mtupu.
 
Huwaga nashauri Binti afike Kidato cha sita hata kama akifeli ndio Aende chuo.

Ila aking'ang'ana kuwa aende college Baada ya kumaliza Kidato cha nne basi akae hosteli za chuoni, tena awe anaangaliwa mara Kwa mara.

Au atokee nyumbani kwa Ndugu au wazazi wanaojua Kulea.

Vinginevyo mimba haziepukiki hapo
 
Huwaga nashauri Binti afike Kidato cha sita hata kama akifeli ndio Aende chuo.
Ila aking'ang'ana kuwa aende college Baada ya kumaliza Kidato cha nne basi akae hosteli za chuoni, tena awe anaangaliwa mara Kwa mara.
Au atokee nyumbani kwa Ndugu au wazazi wanaojua Kulea.

Vinginevyo mimba haziepukiki hapo
Siku hizi mimba havikamati ila kupelekewa moto ndio sana. Nilishawahi kukaa karibu na chuo cha Tumain aisee kwa siku unaweza kuvusha hata viwili

Kama wewe ni mtombaji lazima ukimbie mwenyewe
 
Mm nadhani wazazi hawana uwezo wa kubadilisha lolote hasa walio mbali na vyuo, mfano mtu uko singida na mtoto wako anasomea chuo Dar hata ufanyeje huna uwezo wa kumdhibiti.

Mwenye uwezo wa kukomesha huu upuuzi ni serikali kwa kufuta huu upuuzi unao itwa uhuru ulio pitiliza vyuoni ,kwa sababu wenye busara walisha sema ya kuwa demokrasia ipo kwa ajili ya watu wenye akili na si kwa ajili ya wapumbavu.

Taasisi ya elimu ya juu ni taasisi nyeti sana ndani ya nchi ambayo inaandaa watu watakao amuwa msitakabili wa nchi lakini cha kushangaza serikali ni kama imefumba macho utadhani haioni kinacho endelea alafu kesho tukipata viongozi na watumishi wa hovyo tuanze kulalamika.

Tatizo waafrika tuna razimisha kuishi wa kufuata demokrasia ya kamagharibi hali ya kuwa sisi ni watu wawili tofauti kabisa, kuanzia upeo wa kiakili na mfumo wetu wa maisha
Mfano binti wa kijerumani mwenye umri wa 16 tiyari anakuwa amesha jiwekea malengo ya anahitaji kuwa nani na atafanya nn pale atapo maliza masomo, wakati binti wa kiafrika mwenye miaka 25 anacho waza ni kumiliki iPhone ili awalingishie mashoga zake na jinsi ya kuwapanga mabwana zake 10 anao tembea nao wasijuane, sasa watu wa namna hii huwezi ukawaongoza kwa mtindo mmoja ni lazima ufeli tu.

Huu upuuzi unao itwa uhuru vyuoni ukienda nchi nyingi za Asia na mashariki ya kati haupo na ndio maana wanazalisha wasomi wa maana wenye msaada kwa mataifa yao wakati huku Africa wanao jiita wasomi wamegeuka mizigo ndani ya matifa yao.
 
Wazazi na walezi,

Tembelea watoto wako wanaosoma vyuo!

Hasa hawa walioenda ngazi ya cheti baada ya kumaliza kidato cha nne, wengine wameoa na kuolewa!
Binti haingii darasani, anafua na kupika kwa kijana waliyekutana naye chuoni.

Kuna ambao pesa ya ada hajalipa anahudumia "mke"! Unaweza fikiri yupo masomoni kumbe analea mke na mtoto.

Kuna ambao wamefukuzwa vyuo au kuacha masomo kwasababu mbalimbali, mzazi usipofuatilia hautajua.

Wengi wanaoenda vyuo vya kati au vyuo vikuu baada ya kidato cha nne wana umri mdogo sana, hawajafundishwa namna ya kutumia "uhuru" wa chuo, huko hakuna mwalimu wa darasa au mwalimu wa nidhamu. Haulizwi kwanini hajaingia darasani, au hajafanya mtihani, ni matokeo ya mwisho yatakayoamua.

Sasa mzazi usipoyajua haya unaweza kushangazwa na hayo matokeo ya mwisho, na inaweza kuwa tayari umeshachelewa.

Siku hizi wahitimu wengi wa kidato cha nne hawataki kwenda kidato cha tano, wanataka kwenda vyuo, ukiacha sababu ya kutaka kupata ujuzi na ajira kwa haraka, wengi wanataka kuwa huru. Wanasema vyuoni hakuna mambo ya kuvaa sare wala kupangiwa vitu vya kufanya, na kingine wanafurahia pesa ya matumizi anayopewa chuo ni kubwa kuliko akienda sekondari.

Sasa huu uhuru na pesa ya matumizi ukivichanganya na usipokuwa na akili njema, kuna kitu kinaitwa "majuto ni mjukuu"!

MZAZI TIMIZA WAJIBU WAKO!

Mwl.Doris Mboma!
Ww kama Mzazi omba akaunti yake ya chuo na password yake huko ndo utaona maendeleo ya mwanao chuoni
Hii Akaunti ya mwanafunzi haidanganyi yni akifanya test utaona tu
 
Back
Top Bottom