Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Wazazi msipowafuatilia watoto wenu chuo mtajutia mwishoni

Unataka tuwawekee makufuli kwenye vikojoleo?

Mambo mengine yaachwe kama yalivyo!

Huna la kufanya.
 
Duh!
Kwa hili naomba niungane na monde arabe kusema, "noma sana".
But if we are being serious kungwi Sexless , reason kubwa ni nini? Je ni hao watoto kukosa misingi imara kwenye makuzi yao au ni njaa?
MAana asilimia kubwa tumeenda chuo, tumeona mabinti ambao wanaanza mpka wanamaliza bila hizi drama, na wengine ambao dishi linasoma 890.
Kabla ya kuitishana wazazi kila kona, tujibu swali kwanza, sababu ya haya yote n nini???
 
Hayo mambo yalikuwepo toka kitambo, kikubwa wazazi wawape darasa na kufuatilia watoto wao.
Kadri miaka inasonga hali inazidi kuwa mbaya. Kuna issue ya kiroho na kimwili kutokana na majira na nyakati hizi. Tuwaombee sana watoto wetu zidi ya mikono miuvu, pia tujenge misingi ya makuzi yao katika hofu ya Mungu nasi wazazi tutimize majukumu yetu ipasavyo kwenye kuhudumia watoto
 
reason kubwa ni nini? Je ni hao watoto kukosa misingi imara kwenye makuzi yao au ni njaa?
Sababu kubwa ni mbili:-
1. Mmomonyoko wa maadili. Ngono inaongelewa, ngono inaimbwa na ngono imefanywa kuwa biashara kila kona ya nchi hii.
2. Tamaa. Vibinti vidogo vinataka kuwa na mambo makubwa. Kibinti kinataka kuwa na simu ya gharama ama kutembelea gari kali.
 
Sababu kubwa ni mbili:-
1. Mmomonyoko wa maadili. Ngono inaongelewa, ngono unaimbwa na ngono imefanywa kuwa biashara kila kona ya nchi hii.
2. Tamaa. Vibinti vidogo vinataka kuwa na mambo makubwa. Kibinti kinataka kuwa na simu ya gharama ama kutembelea gari kali.
1. Sasa binti ambae hakuwekewa misingi ya kimaadili moka anafika hatua ya kuingia chuo, leo mzazi akienda huko akakuta kawekwa kinyumba atambadilishaje ghafla? Simple example, mzazi yuko mtwara, mtoto anasoma mwanza, haya amefuata ujumbe huu akaja akamkuta mtoto anapembua mchele kwa ajili ya ze mubaba, wat wil he/she do? Atamuachisha shule? Hata akimkaripia, kwan akisepa dogo hatarudi kwenye hogo la jang'ombe?
2. Tamaa haikwepeki kwa sababu huyo binti bado n mdogo kwenda kumchanganya na waliokubuhu.
Kwaio mimi naendelea kusisitiza, the problem iko kwa hao wazazi kwanza then watoto baadae
 
Kadri miaka inasonga hali inazidi kuwa mbaya. Kuna issue ya kiroho na kimwili kutokana na majira na nyakati hizi. Tuwaombee sana watoto wetu zidi ya mikono miuvu, pia tujenge misingi ya makuzi yao katika hofu ya Mungu nasi wazazi tutimize majukumu yetu ipasavyo kwenye kuhudumia watoto
Mikono miovu ni hii ya kwako wewe National Anthem, bila kusahau mikono ya yule ibilisi mwenzio wa kuitwa @Wa kupambania , bila kusahau mikono ya shetani wa kuitwa mzabzab
 
Mm nadhani wazazi hawana uwezo wa kubadilisha lolote hasa walio mbali na vyuo, mfano mtu uko singida na mtoto wako anasomea chuo Dar hata ufanyeje huna uwezo wa kumdhibiti.

Mwenye uwezo wa kukomesha huu upuuzi ni serikali kwa kufuta huu upuuzi unao itwa uhuru ulio pitiliza vyuoni ,kwa sababu wenye busara walisha sema ya kuwa demokrasia ipo kwa ajili ya watu wenye akili na si kwa ajili ya wapumbavu.

Taasisi ya elimu ya juu ni taasisi nyeti sana ndani ya nchi ambayo inaandaa watu watakao amuwa msitakabili wa nchi lakini cha kushangaza serikali ni kama imefumba macho utadhani haioni kinacho endelea alafu kesho tukipata viongozi na watumishi wa hovyo tuanze kulalamika.

Tatizo waafrika tuna razimisha kuishi wa kufuata demokrasia ya kamagharibi hali ya kuwa sisi ni watu wawili tofauti kabisa, kuanzia upeo wa kiakili na mfumo wetu wa maisha
Mfano binti wa kijerumani mwenye umri wa 16 tiyari anakuwa amesha jiwekea malengo ya anahitaji kuwa nani na atafanya nn pale atapo maliza masomo, wakati binti wa kiafrika mwenye miaka 25 anacho waza ni kumiliki iPhone ili awalingishie mashoga zake na jinsi ya kuwapanga mabwana zake 10 anao tembea nao wasijuane, sasa watu wa namna hii huwezi ukawaongoza kwa mtindo mmoja ni lazima ufeli tu.

Huu upuuzi unao itwa uhuru vyuoni ukienda nchi nyingi za Asia na mashariki ya kati haupo na ndio maana wanazalisha wasomi wa maana wenye msaada kwa mataifa yao wakati huku Africa wanao jiita wasomi wamegeuka mizigo ndani ya matifa yao.
100%
 
Kidada kimeishi kinyumba huko chuoni for 4 or 3 good damn years halafu mimi ndo nimwokote nimuoe..hell no.

Kampeni yetu iendelee mpaka pale bikra watakapopatikana kwa wingi.
 
Lakini wazazi wengi siku hizi wana-opt mtoto kwenda chuo badala ya form five.
 
Huwaga nashauri Binti afike Kidato cha sita hata kama akifeli ndio Aende chuo.

Ila aking'ang'ana kuwa aende college Baada ya kumaliza Kidato cha nne basi akae hosteli za chuoni, tena awe anaangaliwa mara Kwa mara.

Au atokee nyumbani kwa Ndugu au wazazi wanaojua Kulea.

Vinginevyo mimba haziepukiki hapo
Nafikiri our parenting skills ndio zina tatizo. Kwenye familia zetu tunaona zinaa kama kitu cha kawaida. Unakuta baba ana nyumba ndogo mtaani na watoto wanajua. Mama nae anachepuka na jirani au mfanyakazi mwenzake. Yaani hakuna hata wa kulea na kushauri watoto. Jamani tubadilike la sivyo tutaendelea kulaumu watoto kumbe tatizo ni sisi.
 
Kila kitu kinachotokea kwenye jamii huwa kinaanzia kwenye familia Yani baba na mama ,baba kazi yake huwa ni kutimiza mahitaji ya familia kama chakula,mavazi na makazi na mama kazi yake huwa ni kulea familia. Sasa wazazi wengi huwa hatuna utaratibu wa kukaa na watto wetu na kuwauliza changamoto wanazokumbanazo wakati wa masomo yao si huwa tunajaluli kutimiza mahitaji muhimu ya familia na mambo ya kulea huwa tumewaachia wakina mama
 
Tulimkataza binti wa dada yangu kwenda mwanza eti akakae hostel wakati anasoma certificate. Yuko kwangu anaenda na kurudi. Mwaka huu anamaliza diploma. Alianza degree ndio ataweza kukaa huko chuo.
Hata chuo atakaa nyumbani tu jamani naogopa mimi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mimi haya yamenikuta kuna mdogo wangu nilijitolea kumusomesha chuo fulani hivi diploma na nikahakikisha nalipa kila kitu kwa wakati ili baadaye asije kunilaumu sasa kilichotokea dogo kala ada baada ya kupata demu huko chuoni sasa nimeamua kumutimua home akapambane mwenyewe
 
Back
Top Bottom