Magidu
Member
- Oct 18, 2022
- 52
- 86
Nawasalimu nyote,
Jana ni siku ambayo sitaisahau kutokana na story yakusikitisha niliyosimuliwa na binti wa miaka18. Binti huyu ni mwanafunzi wa mwaka wakwanza katika moja kati ya vyuo vikuu maarufu hapa nchini. Aliripoti chuoni Mwezi October Mwaka jana akionekana mtoto mtulivu na mwenye heshima zake.
Kama mjuavyo, vyuoni kuna mchanganyiko wa wanafunzi waliotoka sekondari moja kwa moja na wale ambao wametoka makazini waliokuja kwa lengo lakujiendeleza(In-service).
Sasa kumbe haka kabinti kalikutana na mwanaume mtu mzima(in-service) ambaye alikarubuni wakapanga chumba na kuishi pamoja kama mtu na mwenza wake.Kwa maelezo yabinti nikwamba huyu mwanaume ana zaidi ya miaka48.
Baada ya likizo fupi ya kumaliza semester ya kwanza, wapenzi hawa walitawanyika kila mmoja akienda nyumbani, binti alirudi kwa wazazi huku mwanaume akienda kwa mke nawatoto wake.
Shida imeanza baada ya likizo ambapo binti alitangulia kurudi huku jamaa akiahidi kurudi siku za mbeleni kidogo. Muda umeenda jamaa harudi huku binti akiishi maisha yashida kwani alikuwa anamtegemea yule mwanaume kwa kila kitu ikiwemo kodi ya chumba.
Jana nimemkuta mahali analia anadai baada yakuona anaumwa mara kwa mara ilibidi aende hospital ambapo amekutwa na magonjwa ya ngono ikiwemo VVU/UKIMWI.
Taarifa zauhakika kutoka kwa wanaomfahamu huyo mzee nikwamba ni mgonjwa wa miaka mingi na kutokana na sababu zakifamilia amesitisha masomo hatarudi tena chuoni.
Kilichoniuma binafsi nikwamba naamini mzee kama huyu hakosi binti wa umri kama huyo aliyemharibia kesho yake kwa makusudi. Alishindwaje kuvaa viatu vya mzazi mwenzake ambaye alitumaini kuwa elimu anayompa binti yake itaenda kumfaidisha siku zijazo? Ni vipi angejisikia endapo binti yake angefanyiwa unyama kama huo na mzee mwenzake?
Mwisho; Watoto wa kike mkienda vyuoni kumbukeni yale maneno mnaoambiwa na wazazi/walezi wenu.
Jana ni siku ambayo sitaisahau kutokana na story yakusikitisha niliyosimuliwa na binti wa miaka18. Binti huyu ni mwanafunzi wa mwaka wakwanza katika moja kati ya vyuo vikuu maarufu hapa nchini. Aliripoti chuoni Mwezi October Mwaka jana akionekana mtoto mtulivu na mwenye heshima zake.
Kama mjuavyo, vyuoni kuna mchanganyiko wa wanafunzi waliotoka sekondari moja kwa moja na wale ambao wametoka makazini waliokuja kwa lengo lakujiendeleza(In-service).
Sasa kumbe haka kabinti kalikutana na mwanaume mtu mzima(in-service) ambaye alikarubuni wakapanga chumba na kuishi pamoja kama mtu na mwenza wake.Kwa maelezo yabinti nikwamba huyu mwanaume ana zaidi ya miaka48.
Baada ya likizo fupi ya kumaliza semester ya kwanza, wapenzi hawa walitawanyika kila mmoja akienda nyumbani, binti alirudi kwa wazazi huku mwanaume akienda kwa mke nawatoto wake.
Shida imeanza baada ya likizo ambapo binti alitangulia kurudi huku jamaa akiahidi kurudi siku za mbeleni kidogo. Muda umeenda jamaa harudi huku binti akiishi maisha yashida kwani alikuwa anamtegemea yule mwanaume kwa kila kitu ikiwemo kodi ya chumba.
Jana nimemkuta mahali analia anadai baada yakuona anaumwa mara kwa mara ilibidi aende hospital ambapo amekutwa na magonjwa ya ngono ikiwemo VVU/UKIMWI.
Taarifa zauhakika kutoka kwa wanaomfahamu huyo mzee nikwamba ni mgonjwa wa miaka mingi na kutokana na sababu zakifamilia amesitisha masomo hatarudi tena chuoni.
Kilichoniuma binafsi nikwamba naamini mzee kama huyu hakosi binti wa umri kama huyo aliyemharibia kesho yake kwa makusudi. Alishindwaje kuvaa viatu vya mzazi mwenzake ambaye alitumaini kuwa elimu anayompa binti yake itaenda kumfaidisha siku zijazo? Ni vipi angejisikia endapo binti yake angefanyiwa unyama kama huo na mzee mwenzake?
Mwisho; Watoto wa kike mkienda vyuoni kumbukeni yale maneno mnaoambiwa na wazazi/walezi wenu.