Wazazi wa kisasa ni changamoto kubwa sana kwenye malezi

Hapo sijaona usasa utakuta mtoto bado mdogo anachezea ndani geti kali kwa usalama na kuangalia katuni ndo vinamuweka ndani na wanajifunza vitu vya utoto wao Kama wakubwa wanavyoangalia mpira, sasa mtu mzima yupo ugenini anataka kushindana na mtoto kuangalia TV kwanini usisaidie wenyeji kazi wewe ulilie kuangalia TV Ili mtoto asiangalie katuni?
 
Kweli watu wanatofautiana maoni aiseeh
Hivi ni kweli haya umeongea wewe ama ni nguvu ya balimi?
 
Mi bwana kuna ndugu yangu ni mpole sana, na siku ya kwanza nimemtembelea nilikua nakaa kama wiki hivi pale.

Sasa nimekuta kama anamdekeza mno mwanae na dogo akawa kashaanza mazoea ya kudeka deka. Kumbe yule bro anamlia timing tu dogo ajae maana alishaona dalili sio.

Aisee siku ya siku alimkung'uta yule mtoto, alimpa kichapo kweli kweli. Baada ya hapo dogo akawa na nidham ya hali ya juu. Na mshua wake kanamkubali kama kawaida ila heshima na kufuata maelekezo ni ya kiwango cha SGR.

Kwahiyo sometimes hao madogo wanafanya hivo wakijua hakuna wa kuwazingua na wana watetezi hata wakifanya upuuzi. Kichapo ni muhimu sana kwenye malezi.
 
Hata taarifa ya habari mkuu tuwe kwenye cartoon tuu!?
 
Ndiyo tabia za Sabaya hizi
 
Wakina junior wanaaibisha na wanatia hasira
 
Kila nyumba ina taratibu na ustaarabu wake. Hata Mbwa koko ukifika kwao anakubwekea bila sababu.
 
Mkuu mimi nipo kwa mjomba wangu hapa Chattle wiki ya tatu hii naangalia Nickelodeon na Cartoon network natamani nipate hata dakika 10 niangalie ITV labda ntakuta Tundu lissu anahutubia lakini JUNIOR kashikilia remote
Bora

Wageni wengine hamchelewi kumiliki remote na kuweka bongo movies

Dawa ni katuni mwanzo mwisho
 
Ila mi sion shida mtoto kuangalia katuni akishamaliza homework zake za shule
Bora huyo anaeangalia katuni kuliko yule anaeangalia bongo flava afu kesho unakuta anataka kumbusu mdogo au dada yake as amejifunza humo,
Shida ni ela tu,ukiwa na ela unaweka tv room ya watoto wanacheza na kuangalia katuni humo na wakubwa wanakaa sebleni
 
Matokeo ya malezi kama hayo ndio yalipelekea kuwa na majitu mipigaji tu pasipo kujali kundi kubwa la watz, na JPM alipojaribu kupambana nayo ndio yalimchukia kiasi cha kutaka afe! Mijitu mibinafisi kama fisi! Yapo tayari kuuza nchi kwa faida yao binafsi ya sasa! Wala hayaoni zaidi ya sasa😠! Ungelifinya na kulipa kelebu mpaka kule😠😜! Mfyuuuuuu 😡!
 
Mkuu, kwanza nakupa pole na maudhi katika nyumba ya watu ila nakushangaa karne hii kufikia kwa ndugu...ni heri ungelala lodge menu ndio ukapige kwa bro.anyways labda fungu lilibana..natumai hutarudia.
Pili nakubaliana na wewe kuwa malezi ya sasa ni shida sana. Wazazi wa sikuhizi ni dot.com..wakidhani kumpa kila kitu mtoto ndio kumpenda. Wazungu wameweza kutubrain wash ili tuharibu akili za watoto wetu. Kibaya..jamii kubwa inaona ni sawa kabisa..na unavyosema wengine hapa wanakuzomea. Ladba tu nitoe madhara machache wenye akili watafakari. Mtoto unaemlea kama junior, atapata madhara yafuatayo
  • kujiona bora zaidi ya watu wengine na hivyo kushindwa kuwa na mahusiano bora na wenzake
  • Ugumu kati kujituma; mtoto wa jinsi hiyo kashazoeshwa na wazazi kufanyiwa kila kitu..matokeo yake atakuwa mzigo katika familia na hasa ndoa mahali ambapo anatakiwa kujituma na kuijenga familia
  • Shida katika kufanya maamuzi kwa sababu anaweza kuwa mtemi ktk anapofanya maamuzi..maana anajiamini kupitiliza..na wazazi wamemlea kuona matakwa yake ni command...hivo huwa mbishi sana kusikiliza ushauri wa wengine na hivo..kujikuta akifanya maamuzi ya hovyo
-Mzigo katika mahusiano...atakuwa mtu anapenda kufanyiwa kila kitu ..maana ndivo alivojengwa tangu utotoni..hawa ndio waume ambao hupenda kulelewa..ama kutojali mwenzio bali yeye ndio hupenda kujaliwa..hii ni ngumu ktk kujenga mahusiano yenye afya.

Wazazi tuwe makini na malezi ya hovyo!
 
Nimekuelewa sana mkuu nimejifunza kitu hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…