DOKEZO Wazazi wa wanafunzi Shule ya Sekondari BUJUNANGOMA, tumechoka na Michango, Rushwa, Utumikishwaji wa watoto wetu shuleni

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
Hii ni Shule ya Sekondari BUJUNANGOMA iliyoko Kata Katerero Wilaya ya Bukoba Vijijini, Mkoani Kagera.

Wazazi wa wanafunzi wa shule hii wameandika Barua kwa Rais Samia Suruhu Hassan, Waziri Mkuu na Waziri wa Elimu wakitaka kusaidiwa kutokana na kile wanachoeleza wamechoka na michango, rushwa , utumikishwaji wa watoto wao shuleni hapo.

Katika Barua hiyo ambayo wameandika leo, Wazazi hao ambao wengi wamesema watoto wao ni wale walimaliza kufanya mtihani wa kihitimu kidato cha nne 2023, imetokea michango kwa watoto wao ambayo haieleweki.

Kwanza wazazi hao wanasema kuwa watoto wao wanatakiwa kusaini Cheti cha kuondoka shuleni (LEAVING CERTIFICATE) ambapo cheti hicho usainiwa na kila mwalimu mwisho Mwalimu Mkuu.

Wanadai wametakiwa kulipa baadhi ya michango ndipo waweze kusaini hicho cheti, michango ambayo ni zaidi ya mitano, huku wakidai kuwa hata ambao tayari wamelipa michango hiyo hawajapewa Risiti.

Wanadai kuwa Pesa hizo wanataka kujua zinakwenda wapi? Lakini pia nani alipitisha hiyo Michango, na jambo kubwa wanashangaa kuona watoto wao wanalipishwa baadhi ya vitu ambavyo hawajawahi kuvitumia au kuvifanya.

Ifuatayo ni Michango ambayo Wazazi hao wameorodhesha kwenye Barua hiyo, ambayo watoto wao wametakiwa kulipa ndipo wasainiwe Leaving Certificate.

  • Mchango wa Mche wa Mti- Sh. 5000/= @ Mwanafunzi. Ambapo wanafunzi jumla wako 166. Inadaiwa Miti hiyo ilikauka kipindi cha kiangazi, wakati shule ikiwa imefungwa, lakini wametakiwa walipe hiyo miti wakiambiwa imekauka wakiwa shuleni.

  • Jezi @ Mwanafunzi Sh. 5000/= wanafunzi jumla wako 166. Wazazi hao wanadai kuwa wanafunzi hao hawakutumia hizo jezi, na badala yake walikuwa wanatumia jezi walizowanunulia wakati wanaanza kidato cha kwanza, lakini wameambiwa walipe hizo jezi maana zimepotea.

  • Mchango wa ujenzi wa Choo. @ Mwanafunzi Sh. 7,500/= Jumla wanafunzi ni 166.

  • Mchango wa Karatasi za Ream (Ream Paper) @ Mwanafunzi Sh. 20,000/=

  • Kila mwanafunzi ametakiwa kulipa Sh. 2000/= jumla wako 166, kwa ajili ya kununua Ndoo kubwa (DIABA) ambayo inadaiwa ilipasuka, na watoto wao hawakuhusika kupasua.

  • Kuna wanafunzi 40 ambao walipewa kitabu, lakini kikapotea. Kitabu thamani yake Sh. 20,000/= lakini kila Mwanafunzi ametakiwa kulipa 7,000/= ili kitabu kinunuliwe.
Wazazi hao wanasema kuwa pesa zote hizo watoto wao wanatakiwa kuzipeleka shule na siyo kununua vifaa, wanatakiwa kupeleka pesa shuleni ambapo jambo la Hajabu, hawapewi Risiti (Stakabadhi).

“ Tunashangaa eti watoto wetu walipe mti ambao ulikauka Sh. 5000/= huu ni wizi mkubwa, hii shule walimu wametuona kama mitaji yao, wamegeuza watoto wetu kama mitaji, haikubaliki kama wazazi, viongozi tunaomba msaada”

“ Mche wa mti ya kawaida huwa inauzwa Sh. 1000, inakuwaje wao leo wanasema ni Sh. 5000, lakini pia Diaba kuvunjika kila mwanafunzi eti 2000, kitabu eti kila mwanafunzi 7,000 wakati kinauzwa 20,000, na walivyo wajanja hawataki watoto wetu wanunue hivyo vifaa, wanataka ela tu na hawatoi Risiti”

Tunaomba Mhe: Rais, Waziri Mkuu, na Waziri wa Elimu, kuingilia hili jambo, tunataka ela zetu turudishiwe, tumelalamika kwa Mkuu wa hiyo Shule lakini amesema Lazima tulipe.

Watoto wetu wameambiwa bila ya kulipa michango yote hiyo, hawatasainiwa Cheti hicho.

Pia soma;
  1. DOKEZO - √ - Shule ya Msingi Tumaini ya Tabata Kimanga Wanafunzi wasiochangia Tsh. 800 wanatolewa Darasani
  2. DOKEZO - √ - Malalamiko yaendelea kuhusu malipo ya 'Mchango wa Uendeshaji wa Shule Tsh 65,000' licha ya Serikali kufuta ada
  3. DOKEZO - √ - Wanafunzi wa kidato cha tano kukataliwa kisa hawajamaliza michango ni usumbufu kwa wanaotoka mbali
  4. DOKEZO - Wanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Chanika wazuiliwa kuingia darasani kutokana na kutochangia 500 ya masomo

Hata hivyo Wazazi hao wanakwenda Mbali zaidi na kueleza kuwa wamechoshwa na utumikishwaji wa watoto wao shuleni hapo. Wanasema kila wakati watoto wapo kwenye kilimo.

“ Kila siku watoto wetu ni kulima tu, watoto wamekomaa mikono, kila siku ikifika saa saba mchana, na hawa walimu hawajali hata jua kali, watoto ni kwenda kulima tu. Sasa hivi hii shule inaitwa Shule ya Kilimo kwenye hii kata yetu”

Wazazi hawa wametakiwa kupewa ufafanuzi wa michango hiyo pamoja na kusitishwa tabia za watoto wao kutumikishwa.

HII HAPA BARUA YAO KWENDA KWA RAIS, WAZIRI MKUU, WAZIRI WA ELIMU.


Soma Majibu ya Waziri wa Elimu; Waziri wa Elimu, Prof. Mkenda apiga marufuku Shule kuzuia Wanafunzi ambao hawajalipa fedha za michango
 
Hii ni Shule ya Sekondari Bujunangoma iliyoko Kata Katerero Wilaya ya Bukoba Vijijini, Mkoani Kagera.

Wazazi wa wanafunzi wa shule hii wameandika Barua kwa Rais Samia Suruhu Hassan, Waziri Mkuu na Waziri wa Elimu wakitaka kusaidiwa kutokana na kile wanachoeleza wamechoka na michango, rushwa , utumikishwaji wa watoto wao shuleni hapo.

Katika Barua hiyo ambayo wameandika leo, Wazazi hao ambao wengi wamesema watoto wao ni wale walimaliza kufanya mtihani wa kihitimu kidato cha nne 2023, imetokea michango kwa watoto wao ambayo haieleweki.

Kwanza wazazi hao wanasema kuwa watoto wao wanatakiwa kusaini Cheti cha kuondoka shuleni (LEAVING CERTIFICATE) ambapo cheti hicho usainiwa na kila mwalimu mwisho Mwalimu Mkuu.

Wanadai wametakiwa kulipa baadhi ya michango ndipo waweze kusaini hicho cheti, michango ambayo ni zaidi ya mitano, huku wakidai kuwa hata ambao tayari wamelipa michango hiyo hawajapewa Risiti.

Wanadai kuwa Pesa hizo wanataka kujua zinakwenda wapi? Lakini pia nani alipitisha hiyo Michango, na jambo kubwa wanashangaa kuona watoto wao wanalipishwa baadhi ya vitu ambavyo hawajawahi kuvitumia au kuvifanya.

Ifuatayo ni Michango ambayo Wazazi hao wameorodhesha kwenye Barua hiyo, ambayo watoto wao wametakiwa kulipa ndipo wasainiwe Leaving Certificate.

  • Mchango wa Mche wa Mti- Sh. 5000/= @ Mwanafunzi. Ambapo wanafunzi jumla wako 166. Inadaiwa Miti hiyo ilikauka kipindi cha kiangazi, wakati shule ikiwa imefungwa, lakini wametakiwa walipe hiyo miti wakiambiwa imekauka wakiwa shuleni.

  • Jezi @ Mwanafunzi Sh. 5000/= wanafunzi jumla wako 166. Wazazi hao wanadai kuwa wanafunzi hao hawakutumia hizo jezi, na badala yake walikuwa wanatumia jezi walizowanunulia wakati wanaanza kidato cha kwanza, lakini wameambiwa walipe hizo jezi maana zimepotea.

  • Mchango wa ujenzi wa Choo. @ Mwanafunzi Sh. 7,500/= Jumla wanafunzi ni 166.

  • Mchango wa Karatasi za Ream (Ream Paper) @ Mwanafunzi Sh. 20,000/=

  • Kila mwanafunzi ametakiwa kulipa Sh. 2000/= jumla wako 166, kwa ajili ya kununua Ndoo kubwa (DIABA) ambayo inadaiwa ilipasuka, na watoto wao hawakuhusika kupasua.

  • Kuna wanafunzi 40 ambao walipewa kitabu, lakini kikapotea. Kitabu thamani yake Sh. 20,000/= lakini kila Mwanafunzi ametakiwa kulipa 7,000/= ili kitabu kinunuliwe.
Wazazi hao wanasema kuwa pesa zote hizo watoto wao wanatakiwa kuzipeleka shule na siyo kununua vifaa, wanatakiwa kupeleka pesa shuleni ambapo jambo la Hajabu, hawapewi Risiti (Stakabadhi).

“ Tunashangaa eti watoto wetu walipe mti ambao ulikauka Sh. 5000/= huu ni wizi mkubwa, hii shule walimu wametuona kama mitaji yao, wamegeuza watoto wetu kama mitaji, haikubaliki kama wazazi, viongozi tunaomba msaada”

“ Mche wa mti ya kawaida huwa inauzwa Sh. 1000, inakuwaje wao leo wanasema ni Sh. 5000, lakini pia Diaba kuvunjika kila mwanafunzi eti 2000, kitabu eti kila mwanafunzi 7,000 wakati kinauzwa 20,000, na walivyo wajanja hawataki watoto wetu wanunue hivyo vifaa, wanataka ela tu na hawatoi Risiti”

Tunaomba Mhe: Rais, Waziri Mkuu, na Waziri wa Elimu, kuingilia hili jambo, tunataka ela zetu turudishiwe, tumelalamika kwa Mkuu wa hiyo Shule lakini amesema Lazima tulipe.

Watoto wetu wameambiwa bila ya kulipa michango yote hiyo, hawatasainiwa Cheti hicho.

Hata hivyo Wazazi hao wanakwenda Mbali zaidi na kueleza kuwa wamechoshwa na utumikishwaji wa watoto wao shuleni hapo. Wanasema kila wakati watoto wapo kwenye kilimo.

“ Kila siku watoto wetu ni kulima tu, watoto wamekomaa mikono, kila siku ikifika saa saba mchana, na hawa walimu hawajali hata jua kali, watoto ni kwenda kulima tu. Sasa hivi hii shule inaitwa Shule ya Kilimo kwenye hii kata yetu”

Wazazi hawa wametakiwa kupewa ufafanuzi wa michango hiyo pamoja na kusitishwa tabia za watoto wao kutumikishwa.

HII HAPA BARUA WALIYOANDIKA KWENDA KWA RAIS, WAZIRI MKUU, WAZIRI WA ELIMU.

 
Poleni Ila ni vizuri mkajifunza kuandika barua katika mpangilio mzuri pia hilo tatizo anaweza kulitatua DC ,au DED AU VEO wote hao wanaweza.

Poleni Sana wazazi shule mbovu za kata hazifai kusomesha mtoto ni umasikini tu.
 
Wazazi lipeni hiyo michango,elimu ni gharama
 
Mkuu wa Wilaya ashughulikie hilo mapema maana ni utapeli wa kutisha.

Likifika ngazi ya juu maana yake ngazi za chini wameshindwa kulitatua sasa hapo mtu akiliwa kichwa asije kulaumu.
 
Baadhi ya walimu ni wapuuzi kupindukia. Yaani umaskini wao wanataka wazazi ndiyo wautatue?

Wazazi wasilipe hiyo michango waanzie kupeleka malalamiko yao ngazi ya kata ikishindikana ndiyo wafike kwa waziri litashughulikiwa fasta.
 
Uwalimu ni mateso kwelikweli😀😀😀,
Sasa mwanafunzi kapoteza kitabu hataki kulipa na hayo mengine hamkukubaliana
 
LIKUD
 
Poleni Ila ni vizuri mkajifunza kuandika barua katika mpangilio mzuri pia hilo tatizo anaweza kulitatua DC ,au DED AU VEO wote hao wanaweza.

Poleni Sana wazazi shule mbovu za kata hazifai kusomesha mtoto ni umasikini tu.

Kuna mpuuzi humu anajificha kwenye kivuli cha umaskini wake kutetea shule za Kayumba LIKUD
 
Hii shule imeshindikana kwa kweli michango isiyoeleweka watoto wanatumikishwa Kama wafungwa iwe mvua iwe jua wanalima kilimo Cha kufa mtu jaman hapana na tatzo lipo kwa headmaster ndo kiongozi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…