Wazazi wetu:-Mgeni akiwa anakula ukimuangalia unapigwa, ukipigwa ukalia unapigwa na usipolia unapigwa

Mimi nilikuwa na tabia ya kujificha kila nionapo mgeni/wageni; kama nipo ndani sitoki na kama nipo nje napotea mazima. Lakini ajabu nikaja kuwa 'mteule' wa kula chakula na wageni maalum. Hapa juhudi ilikuwa kunitafuta ili nile na wageni, wazee waliona ninao 'ustaarabu' niwapo mezani!!!
 
Acha kunipa chai jua kali loote hili🤣

Mimi sasa kuna siku tulienda kuwinda ndege, af mzee ashasemaga tusicheze na majirani, kulikua na jiran mmoja tu ndo tulikua tunaenda kucheza hapo, sasa sku hyo huyo rafiki si kapitiwa na wenzake tukafunga safari hadi maporini kuwinda, tume pambana huku na kule mpaka jioni ndo tuna pata ndege mmoja. Hapo mind yangu najua mzee kurudi usiku!

Asee nilipofika home nakuta mmfanyakazi alikua mdada kashachuma mipera ya kutosha sito sahau shoo ya sku hiyo mpk leo. Kesho yake skuli desk langu halikukalika buts zilivimba🤣
 
Aisee ulikuwa una pambania haki yako isi ishe😂🤣
 
Enzi zetu za kucheza mpira barabarani, akipita mkubwa mpira unasimama, kama ndo wa mtaani anamzigo, mtaubeba kuupeleka kwake. Maana kipindi hicho mzazi yeyote ukizingua anakata fimbo ni mwendo wa njiti tu. Ukizingua zaidi unashikwa shati-kaptula 🤣🤣🤣 unakula njiti hadi kwenu na kule unapokelewa na njiti
 
Usipo lia unapigwa (unakiburi), ukilia unapigwa ili unyamanze, ukinyamanza unapigwa ( unadharau).
 
Mzee wako ni mjeshi??😂😂😂
 
Chakula kikitengwa kuna bakuri la baba ,huwa ndio kuna mapaja na nyama nyingi ,ole wako ukaweke mkono huko ...kichapo mpaka baba mwenyewe akupe[emoji23]

KHe 🤔🤔🤔 mlikua mkitendewa na hivi????

Kwetu ilikua watoto tunapakuliwa kwanza ndio anafuata Baba
 
Mzee wako ni mjeshi??😂😂😂
Hamna 🤣🤣,
Umesoma ID yangu nini! Ni self employee, ila balaa lake wanajeshi wakasome. Zaman tulikua tukiwa tunacheza, ukisikia tu mlio wa gari unachunguza kama ni yeye anakuja, unaruka fensi fasta kurudi nyumbani.
 
Hamna 🤣🤣,
Umesoma ID yangu nini! Ni self employee, ila balaa lake wanajeshi wakasome. Zaman tulikua tukiwa tunacheza, ukisikia tu mlio wa gari unachunguza kama ni yeye anakuja, unaruka fensi fasta kurudi nyumbani.
Hanna nimewaza tu kwa ukali huo atakua mwanajeshi😃
 
[emoji16][emoji16]
 
Kuna jicho Moja mama alikuwa akinikata la message sent,delivered na anwered....yaani linatuma ondoka hapa dk hii....mwili unatii...ole wako usisikilize hahaaaaaaa Wacuba hoyeee
 
[emoji16][emoji16]
 
Weeee mtoto asinyimwe fimbo sema ziwe kiasi Kwa ngozi nyeusi Tena Tz zinasaidia mno...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…