Chief Kumbyambya
JF-Expert Member
- Jun 16, 2022
- 719
- 2,408
Nikitembea tu kidogo jasho kibao hata kama kuna baridi vipi. Mfano kukiwa na baridi yani ile baridi haswa naweza nikatembea fresh tu ila nikifika tu sehem nilipokua naelekea labda dukani au sehemu yoyote nikisimama tu jasho hizoo zinaanza kutiririka tena nyingi tatizo linaweza kuwa ni nini?
Nikiendaga mikoa yenye joto kama Dar es salaam ndiyo balaa hata nikae muda mrefu vipi kwamba labda mwili utakua umezoea lakini wapi yani huko ndiyo natembeaga huku najifuta futa mpaka leso yote inaloa chapa chapa.
Mwili wangu ni wa kawaida tu wala sio mnene kabisa mpaka naona sasa hili lishakua ni tatizo. Najua humu kuna wataalam mtanisaidia namna ya kufanya. Kiukweli sijisikii vizuri na hii hali. Tatizo laweza kuwa nini wazee? Na nifanyeje kupambana na hii hali?
Nikiendaga mikoa yenye joto kama Dar es salaam ndiyo balaa hata nikae muda mrefu vipi kwamba labda mwili utakua umezoea lakini wapi yani huko ndiyo natembeaga huku najifuta futa mpaka leso yote inaloa chapa chapa.
Mwili wangu ni wa kawaida tu wala sio mnene kabisa mpaka naona sasa hili lishakua ni tatizo. Najua humu kuna wataalam mtanisaidia namna ya kufanya. Kiukweli sijisikii vizuri na hii hali. Tatizo laweza kuwa nini wazee? Na nifanyeje kupambana na hii hali?