Wazee naombeni msaada, mwili wangu unatoa sana jasho tiba ni nini?

Wazee naombeni msaada, mwili wangu unatoa sana jasho tiba ni nini?

Ugonjwa unaitwa Hyperhidrosis ingia Google soma na namna ya kukabiliana nayo
Cleveland Clinic
Access Anytime Anywhere | Cleveland Clinic › 17...
Hyperhidrosis: Types, Causes, Symptoms & Treatment

ukisoma hapo
wanasema chanzo inaweza ikawa ni
1)shida ya kuzaliwa nayo/kurithi au hitilafu ya kimaumbile ya tezi za jasho chini ya ngozi jasho linapotokea kupelekea kifanya kazi kuliko kawaida,

2)magonjwa mbali mbali ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza
mfano kisukari,maginjwa ya moyo na ,uvimbe,goita,kifua kikuu ,ya mfumo wa fahamu
3)matumizi ya dawa fulani zinazopelekea hali
4)hali ya wasi wasi,mazoezi ,kazi za nguvu zinaweza kupelekea jasho kuzidi

MATIBABU
INABIDI UENDE HOSPITALI UONANE NA DAKTARI BINGWA ATAKUTIBU KUTOKANA NA CHANZO CHA TATIZO
kama ni kifua kikuu kama walivyoshauri wachangiaji utapimwa utapewa majibu ,utachunguzwa utapatiwa matibabu
NENDA HOSPITALI MKUU
POLE SANA.
 
Nikitembea tu kidogo jasho kibao hata kama kuna baridi vipi. Mfano kukiwa na baridi yani ile baridi haswa naweza nikatembea fresh tu ila nikifika tu sehem nilipokua naelekea labda dukani au sehemu yoyote nikisimama tu jasho hizoo zinaanza kutiririka tena nyingi tatizo linaweza kuwa ni nini?

Nikiendaga mikoa yenye joto kama Dar es salaam ndiyo balaa hata nikae muda mrefu vipi kwamba labda mwili utakua umezoea lakini wapi yani huko ndiyo natembeaga huku najifuta futa mpaka leso yote inaloa chapa chapa.

Mwili wangu ni wa kawaida tu wala sio mnene kabisa mpaka naona sasa hili lishakua ni tatizo. Najua humu kuna wataalam mtanisaidia namna ya kufanya. Kiukweli sijisikii vizuri na hii hali. Tatizo laweza kuwa nini wazee? Na nifanyeje kupambana na hii hali?
Kutokwa na jasho kupita kiasi, au hyperhidrosis, ni hali inayoweza kusababishwa na jeni (urithi), mabadiliko ya homoni, wasiwasi, uzito wa mwili, au magonjwa kama vile kisukari na magonjwa ya tezi.

Unaweza kutatua au angalau kusaidia kupunguza tatizo.

1. Dawa za Kupaka
Antiperspirants zenye aluminamu kloridi, mara nyingi hutumika kudhibiti jasho nyingi.
Hizi hutumiwa hasa usiku kwenye sehemu zinazotoa jasho sana kama kwapani, viganja, na nyayo.

2. Dawa za Kumeza

Katika baadhi ya hali, daktari anaweza kutoa dawa zinazosaidia kupunguza jasho, hasa kama hyperhidrosis inasababishwa na wasiwasi au matatizo ya homoni.

3. Tiba ya Sindano za Botox
Sindano hizi hufanya kazi kwa kuzuia ishara za neva zinazofanya tezi za jasho zitoe jasho.
Tiba hii inahitaji kurudiwa kila baada ya miezi kadhaa.

4. Matibabu ya Iontophoresis
Ni tiba inayotumia maji na umeme wa kiwango kidogo kutuliza jasho kupita kiasi kwenye viganja na nyayo.

5. Kuepuka Vyakula na Vinywaji Vinavyoongeza Jasho
Epuka vyakula vyenye pilipili, kahawa, na vileo ambavyo vinaweza kusababisha mwili kutoa jasho zaidi.

6. Upasuaji
Katika hali za nadra sana, upasuaji unaweza kufanywa ili kuondoa baadhi ya tezi za jasho au kukata mishipa ya fahamu inayosababisha jasho nyingi.

Ova
 
Ni jasho la mwili mzima linaanziaga kwenye paji la uso, usoni kwenyewe, shingoni, na kifuani, tumboni, mgongoni na kote huko kwingine kasoro kuanzia mapajani kuelekea miguuni tu. Mafuta napaka ya mgando tu lotion niliacha kitambo sana baada ya kuona nikipaka ndo nasweat zaidi alafu usoni inanifanya nafikinya fikinya sana macho yani yanakua yanauma. yani nikipaka lotion baada tu ya muda kidogo lazima nikanawe uso ili kuitoa sababu ya macho kuuma
Au WEWe Ni Mtu Wa Maji.. .























sUCh kiNd 0f WAtEr bENdEr ?
 
Nyenyegua hunyandui mtu vilivyo na kwenye sex huridhiki so mijasho hayo hutoka toka maana haitoki au huchoshwi kwenye games,. Jingine hii hali ni unakunywa maji mengi sana na hufanyi mazoezi
Figo zimefeli awahi mapema
 
Kacheck figo hizo wewe tusije soon JF tukapokea tanzia
 
Ni jasho la mwili mzima linaanziaga kwenye paji la uso, usoni kwenyewe, shingoni, na kifuani, tumboni, mgongoni na kote huko kwingine kasoro kuanzia mapajani kuelekea miguuni tu. Mafuta napaka ya mgando tu lotion niliacha kitambo sana baada ya kuona nikipaka ndo nasweat zaidi alafu usoni inanifanya nafikinya fikinya sana macho yani yanakua yanauma. yani nikipaka lotion baada tu ya muda kidogo lazima nikanawe uso ili kuitoa sababu ya macho kuuma
Ni system yako tu ya mwili hilo tatizo halikomi....
 
Back
Top Bottom