Wazee wa baraza wasema 'Lulu' ameua bila kukusudia, Jaji kutoa hukumu Novemba 13

Hapana, huwezi. Inabidi uangalie udhaifu wa hoja za hukumu
Pagumu hap😵therwise wawe wameamua kumbeba
Lulu nakafahamu sana.Nilibahatika kuchovya enzi flani za perfect vision
Naomba Mungu amsaidie
 
Lakini kipindi yanatokea haya Lulu si alikuwa minor/chini ya miaka 18...mtusaidie hapa
 
Hayo yalikuwa ni maoni ya wazee tu, Mahakama pia ina nafasi yake ya kureason...na mahakama inaweza kukubaliana na maoni ya wazee au kuyakataa. Kama mahakama itaridhika kuwa Ushahidi wa kimazingira ulotolewa mahakamani ni myoofu (watertight) basi itamuhukumu ipasavyo na kama ikiona ushahidi huo bado unawacha shaka ya maana basi itamuachia huru.

Kikubwa zaidi tusubiri hukumu ya mahakama vyovyote itavyokuwa,lakini cha kuangalia zaidi ni reasoning za mahakama katika kumtia hatiani au kumuachia huru....nnachojua majaji ni watu makini sana,japo mapungufu kama wanadamu wengine hayakosekani.
 
Report ya uchunguzi wa mwili wa Marehemu ilisema amekufa kwasababu ya Brain Concussion.

Mtu hawezi kufa kwa kusukumwa, kupigwa, ajali etc. Kusukumwa, kupigwa, ajali etc kunaweza kusababisha mtu kuanguka, kujigonga na kupelekea mtu kuvuja damu kwa wingi, mtikisiko wa ubongo, kuvuja damu kwenye ubongo, mshtuko wa moyo na mengineyo yanayoweza kusababisha kifo. Hivyo, daktari hawezi kuthibithisha kifo kusababishwa na kuanguka, bali kifo kwa sababu mtikisiko wa ubongo etc.

That said, mahakama haiwezi kutumia sababu ya kifo kuhukumu bali kuoanisha sababu ya kifo na kisababishi cha sababu ya kifo/tuhuma za mauaji zinazomkabili mtuhumiwa. Kisababishi cha sababu ya kifo ndio hupimwa kisheria kama ilitokea kwa kukusudia au kutokukusudia kuua.

Kusema report ya Kifo cha Kanumba kuonyesha alikufa kwa concusion haina maana kuwa mtuhumiwa hakuhusika kuua kwa maana alisababisha sababu ya kifo, na ndio maana kakutwa na kesi ya kujibu ambayo sasa inasubiri hukumu.

Kwa vile sheria ni practice, basi lolote laweza kutokea kwenye hukumu, akahukumiwa vyovyote.
 
Well said ,bila shaka utakuwa wakili msomi
 
Sasa mkuu tunaposema ushahidi wa kimazingira ndo tunamaanisha huko kukosekana kwa eye witnesses!

Kama huyo eye witness angekuwepo na akathibitisha kuwa alishuhudia tukio mwanzo mwisho,basi kusingekuwepo hiyo circumstantial evidence bali ni direct evidence...sasa hii direct evidence ndo ingekuwa funga kazi.
 
Mwenye ujuzi wa sheria kuua bila kukusudia hukum yake ni nini?
 
Uwe mwepesi wa kuelewa na kutofautisha kati ya mauaji na mauaji ya bila kukusudia, Lulu kesi ya yake ni mauaji ya bila kukusudia ambayo inawezekana hata kuachiwa huru au kufungwa
 
MBONA HUJAMALIZIA NA HII MKUU?

"HUWENDA PIA ALISUKUMWA NA KUANGUKIA/KUJIGONGA KISOGONI"
 
Attitude inaweza kuwa imemponza

Ni kweli kabisa, alitakiwa awe kama mtu aliyesingiziwa asisikilize maneno ya mawakili, alitakiwa aende pale amesuka twende kilioni. Ni wazo nililokuwa nalo tangu zile picha zilipoanza kumiminika mitandaoni
 
Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni huko Arusha maeneo flani hivi kuna kijana aliua kwa kumchoma kisu kijana mwenzake kisa, huyo muuaji kwao kulikuwa kunauzwa maji ya bomba sasa marehemu alikuwa ni mteja wao wa maji siku ya tukio marehemu alikwaruzana na huyo kijana muuza maji, bila kutarajia muuza maji akamchoma kisu mwenzake akafa akipelekwa hospita, huyu kijana alikaa ndani miezi sita tu akachomolewa kwa kuwa alikuwa na miaka 17, na watu walishangaa sana ila ilisemekana kwa kuwa alikuwa na undugu na yule jamaa aliekuwa kwenye tume ya uchaguzi nae ni mwanasheria mkuu, wakahisi labda rushwa ila mpaka leo jamaa anadunda mtaani. Wale ndugu wa ,arehemu nao hawakuwa na la kusema ila nadhani walifanya yao maana jamaa hapo kwao kawa msumbufu haswa chizi si chizi mvutabangi wala hana akili timamu kabisa. Hii ya lulu tusubiri tu siku ya hukumu.
 
Lulu hajashtakiwa mahakamani na familia bali ameshtakiwa na Jamhuri ila siyo yule Kiwelu.
 
Wanasheria hatu comment kwa yaliyo mahakamani subiri hukumu itoke ndo kazi yetu itaanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…