Wazee wa baraza wasema 'Lulu' ameua bila kukusudia, Jaji kutoa hukumu Novemba 13

Wazee wa baraza wasema 'Lulu' ameua bila kukusudia, Jaji kutoa hukumu Novemba 13

Tuaminishe wewe nani alimuua Kanumba kama siyo hicho kitoto. Jaribu kufuatilia mwenendo wa hii kesi, Lulu kaonyesha namna Mahakama zetu zilivyo na Double Standard, na sidhani kama hii case itakuja tumika kama precedent huko mbele ni.
JPM alikuwa sahihi sana na huu muhimili pamoja na Wanasheria wa Serikali, unaruhusuje mtuhumiwa kubadilisha maelezo ya utetezi tofauti na yale aliyotumia jitetea hatua za awali!

Huyu mtoto alikana kuwa na Mahusiano ya Ngono na Kanumba katika hatua za mwanzo za usikilizwaji wa hii kesi
LEO HII ANAKUBALI KUWA ALIKUWA MPENZI WA KANUMBA -Tafsiri yake ni kuwa Kibatala na Msando waliosema wapo nyuma yake wamem_coach...
Lulu huyu huyu aliiambia mahakama kuwa alipomkimbia Kanumba ndani alipanda gari na kuelekea Coco Beach (Aliendeshwa na mmoja wa wenzie walio kuwa wanamsubiri nje) leo hii anasema Ali_drive mwenyewe! Bado Mahakama na Mwanasheria wa Serikali wanaona sawa tu! Maelezo ya mtu aliyeua pasipo kukusudia hayawezi kupinda kwa kiwango hiki, Lulu alifundishwa namna ya kusema Mahakamani as if yupo kutengeneza Movie
Mwanasheria wa Serikali hajaona haja ya kumuuliza Lulu wale wenzie alioenda nao kwa Kanumba walio ondoka baada ya Muda gani, na jee alipata muda wa kuonana nao tena, pia anaweza waleta Mahakamani ili mahakama Ione kama wanachochote cha kuiambia mahakama, hasa kipindi anadukuliwa na Kanumba..

Ukweli hii kesi imeidhalilisha KADA YA SHERIA VIBAYA MNO.

Lulu kaua vitu viwili kwa Mpigo, Kamuua Kanumba gwiji wa Filamu za Kibongo, na hakuishia hapo KAUA BONGO MOVIE PIA
Kihalali hata hicho kifungo cha nje sio haki kwa Lulu, yangekua ni mazingira ya sumu tungeamini kua Lulu alifanya yake lakini sio tukio kama lilivyoripotiwa kutokea. Lulu kwa umri na umbo alilokua nalo kipindi kile ni vigumu kuiaminisha jamii kua anaweza kumua Kanumba kwa kipigo.
 
Wanasheria nisaidieni, kwa mfano familia ya kanumba ingeamua kusema kuwa wao wanamuachia Mungu au kwa sabbu yoyte ile hawana haja ya kuendelea na kesi na wanapeleka ombi la kuifuta kesi kama walifungua wao, na wasingeshiriki ktk kutoa ushahidi wwte ule je Jamhuri ktk mazingira kama hayo hiyo kesi proceedings zake zikoje.
 
Mkuu toka mwanzo ilikuwa inajulikana kuwa aliua bila kukusudia..hao wazee wametimiza wajibu wao tu!Jaji ndo atatoa maamuzi ya kumwachia,faini au apigwe mvua!kikubwa jaji ataangalia mambo mengi sana...umri,ugonjwa wa kanumba,pombe..nk...ila kwa mawazo yangu mm ..atatemwa au faini!
Kwa mara ya kwanza nasoma hapa, mtu aliyefanya Manslaughter kupewa adhabu ya fine.....mkuu hii umeitoa kwenye authority gani?
 
Kutokukusudia ina maana nia haikuwepo ni tokeo lilotokea sio kwa kufanya kitu hicho unasonga ugali lakini kwa bahati mbaya huna unga wa kutosha unakuwa uji. Je utaadhibiwa kwa kupika uji?
 
[QUOTE="Nkanini, post: 24142094, member: 437353kuse pamoja na haki hiyo,elewa jaji ana uwezo wa kutoa hukumu na akatoa sababu kuwa hakuna mahakama nyingine ambayo inaweza kufikia uamuzi tofauti kwa hiyo haki inakuwa haipo na elewa ni jaji aliyetoa hukumu ndiye anayetoa ridhaa ya rufaa.[/QUOTE]
Acha uwongo wewe.
Hakuna jaji yeyote anayeweza kusema eti hakuna kukata rufaa.
Hebu toa mfano wa kesi ambayo judge alitoa hukumu na kasema hakuna rufaa
 
Angempatia uroda Mungu wa Mzizima angemsaidia aiseeee daaaah kwani hao wazee wangesema hana hatia
 
mkuu hebu elewa basi..kwa mfano mimi na wewe tukawa tunagombana kwa kurushiana maneno..sijakugusa..lakini nikakusababishia mshituko ukadondoka ukafa...hapo kosa ninalo..la kuua bila kukusudia..its that simple..Lulu na mdogo wa kanumba wamesema wote kwamba kulikuwa na ugomvi kati ya lulu na kanumba...mbona ni simple kuelewa
mkuu hii ni hadithi,jaji ni muhimu aridhike behond doubt kuwa mtuhumiwa aliuwa au alisababisha kifo,sio stories za vijiweni.
 
Mkuu naona sheria imekupita kushoto..kisa cha kupewa dhamana mapema walichunguza na kugundua kuwa aliua bila kukusudia...kama angeuwa kwa kudhamiria ..hilo kosa halina dhamana!
Kwahiyo sheria kama imekupita kulia ndo uwe mjeuri? nimekuambia eleza tuelewe kushoto imeingiaje hapa khaaaaa
 
Wanasheria nisaidieni, kwa mfano familia ya kanumba ingeamua kusema kuwa wao wanamuachia Mungu au kwa sabbu yoyte ile hawana haja ya kuendelea na kesi na wanapeleka ombi la kuifuta kesi kama walifungua wao, na wasingeshiriki ktk kutoa ushahidi wwte ule je Jamhuri ktk mazingira kama hayo hiyo kesi proceedings zake zikoje.
Hakuna kitu kama hiki Mkuu kwenye kesi za jinai...
Kesi ya jinai mshtaki ni Jamhuri.
Alichokifanya Lulu ni jinai dhidi ya Jamii ya Watanzia siyo kwa Mama Kanumba ama familia ya Kanumba. Lulu kafanya kosa ambalo lime_affects the public welfare, na kwa kufanya hivyo kaenda kinyume na SHERIA zilizowekwa na Serikali hivyo anastahili adhabu kadiri ya matakwa ya kisheria....

Kwa ufupi criminal cases hazina tukakubaliane nje ya MAHAKAMA, Unless kesi yako uifanye civil Case na iwe ya Madhara (Tort)
 
sasa hiyo ripoti ina m link vipi na Lulu?acha jazba tujadili hoja hapa ,kuumia huko kwa Kanumba wewe umekuhusisha vipi na mtuhumiwa?je kulikuwa na murder weapon(s) kwenye eneo la tukio?vielelezo vya vilivyotokea pale vipo wapi?na self defence ya mtuhumiwa imeifikiria hapa,je history ya marehemu towards mtuhumiwa ilikuwepo mahakamani?please ebu angalia wenzetu wanavyochunguza na kuendesha kesi za namna hii.
Mkuu acha kukurupuka, elewa nilichojibu kuhusu hoja iliyotolewa. Niliemnukuu alisema hakuna forensic report iliyotolewa kuhusu marehemu. Rudia kwanza post za hapo nyuma ndio utaelewa vizuri.
 
Kitakachomgharimu huyu binti ni kutokusema ukweli. Kwa nini Kibatala amemfindisha mteja wake kusema uongo mahakamani? Kwa wenye kumbukumbu nziri na hili tukio. Mimi nakumbuka kipindi hicho huyu binti alisema Kanumba aliteleza wakati anamkimbiza, sasa mahakamani akasema mambo hata kwa akili ya mlevi naye hawezi kukubali. "Alinisukumiza kitandani na kuanza kunipiga kwa panga kwenye mapaja. Niliziba uso ili asiniumize usoni. Kanumba wakati ananipiga alikuwa akilalamika...sauri yake ilikuwa kama ya mtu aliyekabwa. Nilisikia panga likidondoka chini...Kanumba alidondoka chini na kujigonga. Alikuwa akitapatapa na akijigonga tena. Nilikimbilia chooni, nikapiga kelele kuomba msaada".
Msaada huwa unaombwa chooni kweli? Hata mimi ningekuwa mzee wa baraza nisingekubali. Lazima ningehisi kuna kitu unakificha. Aliyemfundisha haya maelezo ni mwehu. Kuna loop holes nyingi katika hayo maelezo ambayo yanaweza kumpa mtu yeyote mashaka.

Maelezo ya Mshumbushi nayo ni ugolo mtupu. Kutoa maelezo ambayo yanalenga kuonesha kuwa Kanumba alikuwa na matatizo makubwa ya kiafya hasa ya Moyo mpaka kusababisha kuwa na upungufu wa hewa kwenye ubongo nao ni wendawazimu. Wakili wa Lulu anataka kuionesha mahakama kuwa Kanumba alianguka na kupoteza maisha kutokana na magonjwa yaliyosemwa na Mshumbushi!

Ni bora defence wangeiweka kuwa; Kanumba aliteleza wakati wa purukushani za kumpiga Lulu ingeweza kumsaidia, kwa sababu report ya postmortem ilisema Kanumba alipatwa na brain concussion. Tatizo la brain concussion ni kwa ubongo hushuka na kuuziba ugwemgongo baada ya kugonga kichwa hasa sehemu ya kisogo kwa nguvu, kitendo ambacho husababisha ubongo kukosa hewa ya oksijeni. Sasa hapo defence ingekuwa ni kutafuta njinsi gani Lulu hakuhusika na kugonga kisogo chini kulikotokea.

Daah! Balaa likupidhie mbali, unaweza pata adhabu kwa kosa ambalo siyo lako au ni lako kwa namna moja ama nyingine. Ukweli mnaujua nyie wawili, lakini mwenzio hayupo tena. Huenda angekuwepo, angekutetea kuwa hauna kosa katika hilo. Ogopa kesi ya kichwa, ni hatari sana.
 
Back
Top Bottom