Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Siku hizi unaenda ata border saa nane usiku

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Ijumaa

Nimetoka kabanga/ngara, nikiwa na tani 30 za maharage

Nimepanda k9 usiku wa saa 7 hadi benaco salama salimini, nikashuka mizani nyakatura, nikaenda kupumzika nyakanazi

Mapema tu nikalianzisha na P 360 kidot, kupitia mbogwe, runzewe hadi kahama, mzigo ukawa umecheza nikapanga upya

Toka kahama tinde, nzega, igunga singida nikalala manyoni Emirates pale..

Alfajiri nikalianzisha shusha salanda salanda bahi na dom kagua mzigo, gari shwari

Barabara ni safi kabisa hakuna utekaji wizi wala usumbufu

Shida ikaanzia kibamba hapo, vijana wakadandia wakachana turubai bahati nikaona, nikasimama nikaomba ulinzi shirikishi hapo hadi sokota, nikawalipa

Saa namalizia kushusha mzigo wa watu hapa temeke
 
salute.
 
Heshima kwako.... bila nyinyi uchumi unasimama
 
Hivi kibamba bado wanaiba?
 
Jana wakati natoka arusha kuja dar nimekanyaga accelerator mpaka kisigino kikafa ganzi.

Njia Panda mpaka Mombo nimetembea 140 - 150. Napunguza kupanda tuta au kwenye kona.

Segera to Dar nimetembea 100 - 120.

Niliondoka Arusha saa 6 mchana nimeingia dar saa 2.00 usiku.

Lucky enough sikusimamishwa na polisi.
 
My Favorite roads 2021 kama unapenda kunyoosha goti!
1. Manyoni - Tabora (Via Itigi hatari sana but usipate breakdown hakunaga msaada ile njia[emoji1787]
2. Arusha-Longido
3. Arusha - Manyara, na Kondoa- Dom
4. Biharamulo - Muleba
5. Makambako - Igawa (sema mchana kuna tochi kali sana)

My Best Sceneries

1. Moro - Iringa
2. Mbeya - Kyela (Nature ya hapa ni balaa)
3. Arusha-Namanga (Landscapes, vilima, wanyama)
4. Muleba - Chato (driving along Lake Victoria)
5. Himo-Marangu, Kilema, Rombo (hizi njia ukipata muda pita tu hata bila sababu kunavutia sana sana)
6. Mombo- Lushoto
7. Mbeya- Chunya
8. Mara-Serengeti- Ngorongoro Arusha Kama una gari ya juu don’t miss this

Zingine muongezee wazee
 
Touché

I second you

Plus Dodoma - Iringa view ya Mtera Dam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…