Kuna watu wanaamini sana vyombo vyao na maneno ya mitaani. Kabla ya huyo wakati niko njia ya Msata Bagamoyo nyuma yangu ikatokea gari inataa nzuri ananiflash,kawaida kuna taa nikiziona najua sio gari ya kipuuzi nikampisha na fujo zake! Kuangalia ni Hilux mpya D4D nikajisemea hunijui wewe. Nikaanza kumtafuta dakika mbili niko takoni na indicator ya kulia,akakaza nikakandamiza mguu nikakaa kulia. Kuna down fulani kabla ya Msata njia imebonyea kiaina inarusha sana magari, pick up ilirushwa jamaa akawahi breki,nikapita hapo hapo na bumps zake na 160kph nikapotea kaja kunikuta Wami njia ina mawimbi nabembeleza gari huku mbele kuna malori, akapita baada ya daraja pale unapandisha hivi.
Nikapata upenyo nikaanza kumtafuta,njia pale imenyooka na up and down fulani amazing, dakika mbili nyingi nina kama 170 namuona yule Hilux inatoa moshi tu, mita 50 nyuma nikakaa kulia na nimewasha indicator nikawaambia abiria hio Hilux itatoa moshi hadi iungue mimi napita hapo alikuja kunikuta mkata tunakula nyama. Kifupi yule kijana wa kiarabu na wenzie walikuja kunisalimia tukaongea sana kuhusu magari, sasa hivi ana 2011 audi a4 na 2010 range rover sport sdv6