Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

[emoji172][emoji172][emoji172]
Green City.

Nafarijika kuona watu wanapiga trip za Mbeya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tushaingia Green City na pikipiki kutokea Dar....

Tunatembelea sana Mbeya boss

20210727_233047.jpg


mysterio
 
Mabaunsa wa pale wapu.mbavu sana, ipo siku kuna mmoja nitamuundia zengwe.. kuna siku wamenigomea kuingia kisa nipo na ka dogo wakajua sie ni wafunzi.. mabaunsa ya pale ni kama maroboti hayana akili 🙂🙂🙂
Dah bambalaga wana dharau sana [emoji23][emoji23][emoji3]. Yamenikuta haya pia mkuu. Ukienda na mtu mwenye umbile dogo haingii. Hawataki proof of age wala nini yani wanaangalia tu kwa macho wanaamua kugoma, wanasema "humu hamna watu wa rika hilo"
 
Unatembea, alafu hujui tu. kuna watu wana kila kitu na kuna wasio nakila kitu, ila hupendelea safari za miguu kutoka mkoa hadi mkoa au nchi hadi nchi for fun
Yaani atembee for fun na huku Nyumbani hata kula ni ya shida!?!
Njiani anakula nini?

Kwamba mtu anatoka tz hadi Malawi kwa mguu?
Labda ile Malawi ya kwetu ambayo mtu akivuka mto tayari yupo Malawi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ipo kimyaaa sana, sijawai lala pale huwa haijalishi nimeingia saa ngapi na natakiwa nitoke saa ngapi, huwa nahakikisha naondoka
Usiku wa kwanza nilipaki nje ya giraffe bar wanapokesha pale, nikapiga kvant yangu nikalala kwenye gari [emoji23][emoji23][emoji23]

Kesho yake ndio nikafanya utaratibu wa malazi. Chato pako kushoto sana
 
Dah bambalaga wana dharau sana [emoji23][emoji23][emoji3]. Yamenikuta haya pia mkuu. Ukienda na mtu mwenye umbile dogo haingii. Hawataki proof of age wala nini yani wanaangalia tu kwa macho wanaamua kugoma, wanasema "humu hamna watu wa rika hilo"
Hawana akili wale marobot, shemu yenyewe ni kawaida sanaaa, tunaendaga pale watu tuna mambo yetu ila hapana u matawi yoyote hadi kuleta zile dharau vile..
 
Usiku wa kwanza nilipaki nje ya giraffe bar wanapokesha pale, nikapiga kvant yangu nikalala kwenye gari [emoji23][emoji23][emoji23]

Kesho yake ndio nikafanya utaratibu wa malazi. Chato pako kushoto sana
😀😀😀😀 kumbe walala kwenye magari tupo wengi, umenichekesha sana. Hasa nikiwa nimejikuta nipo maeneo imenikuta night kali alafu harakati hazijakamilika, mala nyingi nazama kwenye gari nawasha heater nalala zangu tu
 
😀😀😀😀 kumbe walala kwenye magari tupo wengi, umenichekesha sana. Hasa nikiwa nimejikuta nipo maeneo imenikuta night kali alafu harakati hazijakamilika, mala nyingi nazama kwenye gari nawasha heater nalala zangu tu
Lifestyle hii lazima tu utalala kwenye gari mara moja moja. Kwetu tunaotafuta mkate kwa kuzurura hili halikwepeki.

Gari zinatusitiri sana.
 
Yani nilijisikia kudhalilika vibaya mno. Na huenda ikawa last time mimi kukanyaga pale.
Inauma sana, mtu mwenyewe anae leta dharau ukimuangalia hata ishi yake ya mashaka mashaka. Kuna mmoja nitammundia zengwe lazima akalale ndani baada ya kumueleza vizuri kuhusu dogo nilie nae akafanya nisukuma.. huwa sitaki makuu nikaa nje pale tukaagiza ali nitreat kama mbwa koko.. but halitoisha hilo, nilijiapiza kabisa siku naondoka pale kuwa nitarudi tena ili tubalance mambo 😎 😎
 
Lifestyle hii lazima tu utalala kwenye gari mara moja moja. Kwetu tunaotafuta mkate kwa kuzurura hili halikwepeki.

Gari zinatusitiri sana.
😀😀 huwa kuna raha yake, pia huwa nafanya hivi kupunguza gharama, unakuta natakiwa kukaa siku tatu, nikilala kwenye gari hotelin nitalipa siku mbili na ndio sababu ya safari za usiku na alafajiri kupunguza gharama
 
Uwezo wa kufanya mambo.

Kwako utajiri ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmh uwezo wa kufanya mambo gani

Mimi kwangu utajiri ni kuwa na pesa za kukimu yale mahitaji yote muhimu ya binadamu na bado zikabaki nyingine za kutosha kufanya maendeleo na kuweka akiba (na hii ndiyo tafsiri ya kawaida ya kiuchumi tukiachana na hizi ngonjera za utajiri wa moyo sijui nafsi)

In short kwangu mimi tajiri ni yule mtu ambaye pesa zake siyo za mawazo

Sasa wewe mwenzetu unachotaka kutuaminisha hapa ni kwamba hata mtu akipata nauli tu ya kuweza kumfikisha Mbeya au Moshi na kurudi akasema na yeye asafiri aoshe macho kidogo basi tayari ni tajiri

Wakati unaweza kukuta amesacrifice vitu kibao hapo ambavyo ni vya muhimu ili tu kujichanga hadi kufikisha hiyo hela kusudi tu na yeye asafiri sababu kusafiri ni hobby yake

Mimi kwangu huyo siyo tajiri maana hela zake ni za mawazo na hata mimi kama nina hela za mawazo kama hizo siwezi kujihesabia kuwa ni tajiri na hata mtu akisema mimi ni tajiri nitakuwa naona kama ananitukana tu

Kwahiyo siyo kila anayesafiri ni tajiri
 
Back
Top Bottom