Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Watu wa Dar hamna upendo kabisa[emoji19]

.....
Huko kigamboni nitsenda kwa kupita darajani..
Ila kwenye maji siji kuthubutu mimi.
Siyo hatuna upendo tatizo foleni za hilo jiji. Zamani wakati bado kula kulala nilikuwa na muda wa kufunga safari from Tegeta to Tabata ili tu nikatafute kijiwe kipya cha kula na kunywa nilikuwa siwazi kuhusu foleni maana sina pa kuwahi.

......

Tangu maisha yawe magumu huo utoto nimeacha asee kwenda sehemu ni hadi kuwe na jambo la msingi la kunipeleka. Nikimaliza kilichonipeleka ndiyo nitaangalia kama kuna kijiwe kizuri ila siyo nikifungie safari toka huko daah uongo.

......

Basi mimi huwezi amini ile njia ya darajani nayo nina zaidi ya mwaka sijaipita na siipendi sababu iko mbali kwangu ni kama nazunguka. Mixer foleni za ile misemi inayotoka na kuingia bandarini aahh mie ni mwendo wa pantoni tu shwaaa tayari.
 
Sure mkuu mwenyewe Buza hadi leo napasikia sijawahi fika na natamani siku nifike nikapaone tu lakini ukiwaza unajiona jau yaani unafunga safari toka lets say Boko hadi Buza ili tu ukapaone. Mimi naona ni rahisi mtu kuzurura maeneo ambayo ni karibu na Makazi yako hapo inakuwa haina noma.
 
Wakishua itabidi nikutafute nikulete Buza upaone.
 
Hahaaaaaa kwa hiyo badala ya nchi, jobless ndio watanadiwa
 

Mi na uzee huu starehe yangu ni kula

Nafunga safari Ila Zile sehemu ambazo hazitanisumbua kurudi

Hela naisaka kwa Tabu hata kuitumia nibanie [emoji134] hapana
 
Mi na uzee huu starehe yangu ni kula

Nafunga safari Ila Zile sehemu ambazo hazitanisumbua kurudi

Hela naisaka kwa Tabu hata kuitumia nibanie [emoji134] hapana
Mimi hadi kesho starehe yangu ni kusafiri. Kula siyo starehe yangu sababu kunanifanya ninenepe tu wengine tunakula basi tu ili tusife njaa.

Hata safari za kikazi mtu anaweza akaona kama amenikomoa kumbe ndiyo kampa kichaa rungu. Sie wengine hatuoni shida kuwa safarini hata kila wiki.

Mimi safari siichukulii kama adhabu bali naichukulia kama adventure na exposure. Kuna mtu akiambiwa kuna safari anatamani hata kulia dooh.
 
Usiniambie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…