Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Halafu huwezi amini sijawahi kukufuma unatukanana na mtu humu jukwaani yale matusi ya nguoni kabisa kama wengi. Kwahiyo nashangaaga ni matusi gani hayo hadi unafungwa jela.
Ha ha kuna kejeli za reja reja tu😅 ila huwa zinachoma sana! Huwa nampa mtu anayejifanya chizi wakati yu hali timilifu!

Huwa sio matusi ya nguoni in such😎
 
Kukupa shkamoo mtoto mwenzie wa miaka 20 ni haki yako kutokujibu.
 
Halafu huwezi amini sijawahi kukufuma unatukanana na mtu humu jukwaani yale matusi ya nguoni kabisa kama wengi. Kwahiyo nashangaaga ni matusi gani hayo hadi unafungwa jela.
Basi hujamkuta kwenye anga zake.
Ana matusi huyo acha kabisa.
Walishaogeshanaga na yule iceberg,,jamaa wote wawili ni maexpert🤣

Mimi hadi kule MMU nikiona tu ameanza kupata moto kichwani basi namswitch off kwa kuadjust tu comments,natembea na beat lake anavyotaka.
 
Pole sana, hii ndio sababu sipendi kuendesha usiku. Kingine mtu akiwa anaendesha na mbele kuna lori au gari lolote anachochea tu ili alipite bila kujua kuwa unapoikaribia ile gari na mwendo wako mkubwa mbele inaweza kutokea gari ingine ushindwe kupita utaingia nyuma ya lori au porini.
Ni kweli kabisa watu wa malori ni watu wanajitoa sana kwenye majanga. Sisi wa magari madogo tunajiona tuna haraka zetu bila kujua kilomita chache mbele unaweza kuwa wewe unaehitaji msaada.
 
Ilikuwa bado kidogo zipigwe sema ukabadili ID 😅
 
Hahahah hio Mistake huwa naepuka sana yani ku overtake kiboya bila kuona mbali, uupate mnyooko kama Wa Ruvu ule hapo naweza chomoa maana barabara ni tambarare nafasi ipo 😅😅😅

Ila unakuta usiku mkali eti mtu anatanua kilima cha wami kile huku anapush ki Vits cha 1.0L 😅😅😅unajiuliza huyu zimo kweli? Anakomaa akate Semi 3 matokeo yake anaminywa tu na Scania au Fuso ilioiva!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…