Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Yaani kila sehemu hiyo Dar pana/paliwahi kuwa na maeneo ya uswahilini
Obay na Masaki hapajawi kuwa na hakuna uswazi. Aliokwambia paliwahi kuwa na uswazi akwambie wapi. Usikute mnazungumzia Msasani maandazi road na bonde la mpunga. Maeneo ya mkoloni hayo wamejenga miaka hio sehemu tupu zilikuwa na mashamba ya mkonge.
 
Nashukuru Sana mkuu.

Nimeweka utani sijalalamika.

Hayo mengine ya Kua deal au sio deal nafunika kombe....

Muhimu uhai na afya njema. Mungu awajalie afya njema.
Usiwaze mkuu. Kuna jamaa mmoja humu anajiitaga nani sijui yeye kwenye zile nyuzi zinazohusu sijui kutaja member unayemkubali au kumtakia member unayemkubali heri ya sikukuu fulani huwa analalamika kuwa hajawahi kutajwa.

Na kuna siku alishawahi hadi kutishia kuondoka jf mazima kisa anaona hapendwi na watu hivyo hana maana. Nikasema duuh hii ishu unaweza kuta tunaichukulia poa kumbe kwa wengine ni serious hadi wanawaza mambo ambayo hayapo.
 
Sasa uneishi huko halafu hujui kuwa ni mitaa au nini [emoji15][emoji15]
Mie najuaga ni mitaa pamoja na hizo alizotaja extrovert. Sasa alivosema ni majimbo ndiyo kanichanganya, kuwa usikute mi miaka yote najuaga ni mitaa kumbe kitambo yashabadilishwa yamekuwa majimbo, maana hii nchi kila mwaka vijiji, mitaa, kata, majimbo, miji, majiji, wilaya na manispaa mpya zinazaliwa.
 
Ndio mchezo wangu huo. Yani taa zikiwaka kijani na hamna boda boda around ninachomoka vibaya mno
Achaneni na hio njia! Kuna siku natoka Mwenge nimeiachia taa zote kijani kufika hapa ilipokuwa Halotel zamani kuna jamaa akaingia na Crown niko 100+ nilipiga breki moja nikaswerve kushoto nilimkosa kama cm mbili nikajikuta nimefunga barabara zote mbili. Hizi barabara za mjini sio kabisa kuna wehu zile taa kwao hazina maana.
 
Achaneni na hio njia! Kuna siku natoka Mwenge nimeiachia taa zote kijani kufika hapa ilipokuwa Halotel zamani kuna jamaa akaingia na Crown niko 100+ nilipiga breki moja nikaswerve kushoto nilimkosa kama cm mbili nikajikuta nimefunga barabara zote mbili. Hizi barabara za mjini sio kabisa kuna wehu zile taa kwao hazina maana.
Alikuwa anawahi nyekundu ya upande wake sio? Taa za ile barabara ya mwenye zinakuwaga kijani muda mrefu mno, unapoikaribia intersection kuna kila sababu ya kupunguza mwendo kwanza maana watu uvumilivu unawashinda wanazivukaga.
 
Alikuwa anawahi nyekundu ya upande wake sio? Taa za ile barabara ya mwenye zinakuwaga kijani muda mrefu mno, unapoikaribia intersection kuna kila sababu ya kupunguza mwendo kwanza maana watu uvumilivu unawashinda wanazivukaga.
Hata sijui alikuwa anafikiria nini, ndo maana nasema hizi taa usiziamini kuna mwenzio anaosha tu.
 
Nilikua natoka Dom - Arusha.
Kufika makuyumi huwa Kuna kizuizi usiku kwajili ya magari makubwa kukaguliwa, gari ndogo zina pita.

Baada ya kizuizi kuna mizani hivyo magari makubwa yakitoka kukaguliwa huingia mizani alafu yanaendelea mbele uelekeo wa Arusha.

Kumbe kuna gari kubwa moja walipita pale kwenye kizuizi kimagumashi Kwa kutoa ela ya kiwi kwasababu gari Lao bovu sanaa.

Ghafla nikalikuta halina taa hata moja, halina reflector na linatoa Moshi mwingi Sana wakati huo chombo imesha kubali gear na upande wapili kuna chombo ingine iko mafuta Sana.

Option niliyo Kua Nazo za haraka ni kuigonga Kwa nyuma Ile gari mbovu, kuigonga Uso Kwa uso Ile gari ilyo Kua inatoka Arusha au kulimwaga porini.

Mind you hapo barabara iko juu porini ni chini na kuna wanyama.

Basi nikalitupa huko porini likapinduka mara mbili lakini kabla nilisha hangaika na brakes gari ikawa ina sota Tu it was too late.

Alipo kuja mkuu wa kituo pale makuyumi aliwasema Sana wale police kwanini alishindwa kuifwata Ile gari kubwa kumbe washa Kula Chao.

Msaada mkubwa ulitoka Kwa maderava wa magari makubwa. Hawa WA gari ndo walikua wanapita shwaaaa shwaaaaaaa shwaaaaa

Ilikua hivyo.
Hapo unaweza sali salamu maria kwa speed ya mwanga.

Ila kusafiri usiku ni changamoto sana mkuu.

Unaweza kutana na hatari 50M toka ulipo, hata ukiwa 100kph, maamuzi ya ghafla hayasaidii sana. Mind you usiku ndo wanatembea wabovu wote wasioruhusiwa kutembea mchana.

Pole sana.
 
Obay na Masaki hapajawi kuwa na hakuna uswazi. Aliokwambia paliwahi kuwa na uswazi akwambie wapi. Usikute mnazungumzia Msasani maandazi road na bonde la mpunga. Maeneo ya mkoloni hayo wamejenga miaka hio sehemu tupu zilikuwa na mashamba ya mkonge.
Sehemu wanakaa mabalozi wote ukute uswahili.?

Labda wale waswahili wanaoendaga Coco Beach kula mihogo.
 
Back
Top Bottom