Halafu nimegundua hii nchi kuna mitaa midogo ambayo ni maarufu kwetu wakazi ila haitambuliki kiserikali. Na kuna ile mitaa mikubwa ambayo ndiyo inatambulika kiserikali ambayo tunaweza dhani ni kata kumbe kiserikali ni mitaa.
Mfano hiyo Geza Ulole ya Mbweni, kiserikali haitambuliki. Inahesabika ni Mtaa wa Mbweni, Kata ya Mbweni, Wilaya ya Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam, Nchi ya Tanzania, Bara la Afrika, Sayari ya Dunia, Galaxy ya Milky Way (joking).
Nilishangaa kumbe hata Ununio inahesabika ni mtaa ambao upo kwenye kata ya Kunduchi, wakati siku zote wengi tunajuaga Ununio ni kata inayojitegemea, mambo haya. Kuna wakazi wa Dar hadi leo bado wanajua Dar ina wilaya tatu.