Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Mbwembwe zinakuwa hamna, aisee ile Morroco- Mwenge wahuni wanapasuka vibaya mno yani jana kuna mwamba ana Royal saloon mwendo aliokuwa anaenda nao nahisi alifika 16O ni shida.😂😂😂
Hapo watu wanakatiza taa nyekundu bila kujali mwendo huo ni kutafuta kifo. Hizo gari kama hujitambui inakuua.
 
Leo nimetoka dar saa sita nimekuja moro saa nane na nusu nipo moro napata msosi.
Leo njia ilikuwa wazi sana bila shaka. 3hrs ndio mwendo sahihi wa Dar-Moro ukiwahi sana unatumia 2hrs 4Omins. Hilo ni ukikubaliana na cheti lakini maana kutembea hizo speed mchana hawakuachi. Wao wanataka uende dsm-moro kwa masaa 5.
 
Ila uwe na hela ya wese ya kuzidi maana wale
mipasuko yao lazma ikuchomee wallet. Wanagusa 14O-18O humo.
 
Mkuu wewe mwanachama mwenzangu wa night
trips bonge moja la experience. Lami imepoa engine inatembea on optimum perfomance.
Yes mkuu mimi ni team moja na wewe,Nina move zaidi usiku mchana hapana ,huu muda wa mchana ni kulala baada ya kuhakikisha chombo cha usafiri kipo safi, motor, taa za mbele,tailing lights, wiper, all fluids zipo kwenye level yake na kitu muhimu ni tyres, maana hii ndio contact pekee Kati ya gari na barabara.
 
Eeh tyres ndio mchawi, sema uwezekano wa kuzingua usiku ni mdogo sana sababu lami imecool. Alimradi ziwe nzima tu
 
Ila uwe na hela ya wese ya kuzidi maana wale
mipasuko yao lazma ikuchomee wallet. Wanagusa 14O-18O humo.
Ni kweli mkuu hizi ITS ni moto mno ila convoy yao ni safi na unakua salama, pale Msamvu unafanya PR nao ili wasikuone ni intruder, mkifika pale petrol station ya ipogolo (kituo kikubwa)sio mbaya kuzungusha coffee ☕ kwa convoy nzima,hii PR inakusaidia mno maana wanakuona ni sehemu yao
 
Eeh ni kweli mkuu, jamaa hawarembagi wale 😂😂😂
 
Eeh ni kweli mkuu, jamaa hawarembagi wale 😂😂😂
Wale ni moto mkubwa ila usiwe nyuma sana,ukiwa nafasi ya 3 ni safi maana pointer usimpoteze kabisa,unapokwenda kulia na wewe unakwenda pale pale, tailing lights zake zitakuwa zinaongea, aki apply brakes utajua Pana tatizo na wewe unakua umeshajiandaa to break
 
Jamaa wanakatizaga mikumi kama mshale 😂😂😂
 
Mi nakumbuka kuna wakati nilitoka mbeya na tyre za kuunga unga ila nilifika DSM salama kabisa. Yote ile kutembea usiku bila hivyo mchana ningeadhirika.
Yes tyres za kuunga ni very risk, halafu uzuri wa usiku pale kitonga pass hapasumbui sana maana trucks nyingi zinakua zimeshapaki ,ni tankers chache zinakua barabarani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…