Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Dodoma to Tabora via Manyoni na Itigi sio? Aisee bonge la mkeka kona kitu gani tuko na sedans mkuu?

Mimi nilitumia 3 hours Nkuhungu to Tabora, trip meter hiyo hapo, 127kmph average. Ile lami ni tamu MNO!

View attachment 1815749

Tabora Nzega pia ni burudani ila pafupi only 120km wakati Tabora to Manyoni ni around 250km.
Ila ukiwa unaenda dodoma fupi ni ya manyoni, kuliko kupitia nzega.. mkeka ni mtaaamu sanaa.. nachopendea hakuna unafiki wa trafic kule.. unatembea tani yako
 
Pale opposite na kitete hospitali wanapika mchemsho wa kuku wa kienyeji unaitwa 'Abuja'.

Mzito kama roast, una hoho kibao unakuwa wa kijani kinyama. Ladha ya kipekee sana. Ndio kitu unique kuhusu Tabora, sijaona pengine.

Ila pisi za hii town ukiwa viwanja zina shobo hatari. Zinajirahisisha balaa. Kukufuata kukuomba uwanunulie bia sio ishu sana. Ukisalimia tu unaombwa bia.

View attachment 1815900
20210428_215543.jpg
 
Chunya road! Kwenye zile kona zetu za mkoa!

Nimesikia jana kuna ajali imeua watano kwenye hii barabara ila sijajua ni wapi exactly! Leo matraffic wamejaa kila kona wamechachamaa wanataka level seats tu abiria yeyote anayezidi anashushwa njiani!

Sema hii barabara nayo ni kisanga kingine! Kona kali sana japo nayo ina breath-taking views kama zote!View attachment 1810812View attachment 1810815
Naona kibao hicho. Yani barabara inapiga U turn. Hatari sana ukiingia kichwa kichwa
 
Naona kibao hicho. Yani barabara inapiga U turn. Hatari sana ukiingia kichwa kichwa
Acha tu mkuu barabara inapita juu ya milima na kuna sehemu kule juu lazima mkutane na yale mawingu yanayosababisha ukungu barabarani kwahiyo dereva inabidi uende mdogo mdogo tu hamna namna

Inasemekana ndiyo barabara kuu inayopita juu zaidi kuliko barabara zote Tanzania kutoka kwenye usawa wa bahari

Kona zake hata ile barabara ya Mombo-Soni-Lushoto sidhani kama inaona ndani kwa hii
 
RRONDO huu uzi hautufai wengi wetu humu. Unaweza kumuiga Holy Man ukaishia pabaya aiseee...masaa matatu dodoma to Tabora? Hahahah...bado nina hamu ya kuenjoy uchumi wa kati wa mama Samia...
Fanya kile unachopenda mkuu. Mfano mimi siogopi kufa na mambo na raha za dunia najuaga ni vitu vya kupita, kipindi tunapita lazima kukamua kile upendenacho😀😀. Tumezaliwa watupu na tutaondoka watupu.
 
Back
Top Bottom