Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Huwezi kukuta IST highway inaenda mwendo wa kinyonge, wote wanakamua balaa!
Hatari sana aisee. Kuna jamaa aliwahi kunipita na Vitz aisee sikuiona hadi naingia Dodoma. Jamaa ni alikuwa anapaa, anaendesha kama kavuta bangi, hata overtake zake hazizingatii tahadhari kabisa. Hawa jamaa hawafai kupewa magari yenye performance kubwa maana tutawapoteza sana
 
Sasa huoni raha hio mwezio anapiga 140KPH kwa 13KM/L wewe ukipiga speed hio hio ngoma inatafuna 7KM/L [emoji28][emoji28][emoji28]
Sahihi kabisa, tofauti ni kubwa sana. Mnasafiri umbali sawa, na spidi sawa na mnafika pamoja lakini mwingine anatumia nusu ya mafuta aliyotumia mwengine. Ndio maana hawa wa Vigari vidogo muda wote wanavinyaga sana
 
[emoji22][emoji22][emoji22]Mjepu mnamchukulia poa sana..??
Zile limiter ndiyo kikwazo kikubwa....
Kwa mfano chukulia 2GR au VQ35, halafu ziwe limiter imechokonolewa...

Si mchezo...
Mjapani wanamletea kibesi sababu anaishia 180KPH ila mi nakwambia siku moja tukutane huko nina Lexus yangu ya 280KPH majibu watayapata mbona.
 
Wazee wa Road Trip naombeni ushauri kidogo... Kuna gari Honda CR-V second generation (2002) nataka kuichukua, ila kabla sijaichukua nimekuja hapa kupata muongozo kwenu wadau.

Wasifu wa hii gari ni manual transmission yenye real time 4WD, gari ni left hand drive, mmiliki ni muhindi anakaa upanga hapo, aliinunua ikiwa zero mileage plate number ni CK, Hadi Sasa inasoma 130,000 mileage. Nimevutiawa na dash yake inasoma Kmh220 na Mph140.

Kwa wasifu huu mfupi mnanishaurije wadau? Kwenye swala la upatikanaji wa spare na mengineyo muhimu. CC RRONDO Bavaria Kijana wa hovyo hovyo Offshore Seamen ISO M.CodD na wengine wenye uzoefu na hii gari..

Natanguliza shukran.

Wazee wa picha :

View attachment 2065999View attachment 2066000View attachment 2066001View attachment 2066002
Gari nzuri japo sijawahi kuvutiwaga na Honda cars
 
Back
Top Bottom