Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Asalaam, mrejesho wangu sio wa kulalama ila ni kujaribu ku draw attention ya politicians to do something, T1 yetu inahitaji msukumo hasa wa political will,tuijenge upya sio kuiwekea viraka, yule mkandarasi aliyejenga kile kilima cha kushukukia mikumi mjini aturudishie chenji yetu ule ujenzi ni zero, Iyovi pass not bad ile zile tutas loo, why tutas in the middle of nowhere?,Kitonga pass ni cancer level 4(mgonjwa anakufa sio kutibika),Chimala hadi Tunduma OSBP ni mbovu mno ,T2 kuanzia Nakonde hadi Isoka ni mix bag (inajengwa na ikiisha itakuwa super road),Isoka to Chinsali ni safi, na kati ya Chinsali to Serenje nayo ni mix bag,Ile bwawa la samaki limepigwa kifusi cha ovyo, na kutoka Serenje to kapiri ni safi,checks points za T1 hasa Sanga Sanga, Ruaha darajani ni pasta kichwa ,T2 zile za Chinsali, Mpika na Mkushi nazo ni Pasua kichwa, Dar to Moro ni lazima tufanye maarifa ya kupunguza traffic jam, like malori yapewe muda maalum wa kusafiri kwenye kipande hiki, thanks

Nakubaliana na huu mrejesho kwa kweli. T1 ni changamoto kubwa. Pia, kuna many growing towns kama (Mikumi, Tanangozi, Mafinga) unakuta malori yanapaki barabani kwa sababu hayana mahali pa kuwekwa. Barabara yenyewe tayari nyembamba! It is very dangerous.
 
Mkuu ilula ni mbali sana na makazi ya watu kama vile yameharibu ule muonekano!







Ukitoka kile kijiji cha mahenge wanachouza karanga barabarani, sogea mpaka ilipokuwa kitonga comfort then sogea tena mpaka pale zege ya mlima inapoanzia..







Hakika hicho kipande kinavutia sana, ni miongoni mwa maeneo machache yanayopendeza sana!!!







Msimu wa mvua, unaweza kuyasikia maji ya mto Lukosi yakiporomoka huko kando ya barabara!!



Karanga usiku...mkuu wale ndugu zetu ni wanapambana sana na maisha, kwa waendesha usiku kama mimi,ukipita pale hata kama ni saa nane us,iku utawakuta!
 
Kweli kabisa mkuu wale vijana ni wanauza karanga zao masaa yote!

Cha kufurahisha zaidi ni kwamba zile karanga wamezichambua kwa uweledi wa hali ya juu!
Unaweza kuzitafuna hata gizani bila shida..

Hiyo ni njia yangu kuu kwenye kusaka ugali so mara kadhaa nimelala pale baada ya kukuta parking ya ruaha mbuyuni imejaa..
 
Kweli kabisa mkuu wale vijana ni wanauza karanga zao masaa yote!

Cha kufurahisha zaidi ni kwamba zile karanga wamezichambua kwa uweledi wa hali ya juu!
Unaweza kuzitafuna hata gizani bila shida..

Hiyo ni njia yangu kuu kwenye kusaka ugali so mara kadhaa nimelala pale baada ya kukuta parking ya ruaha mbuyuni imejaa..
Safi sana mkuu, pia pako salama kulala pale
 
Dar Moro wasipofanya kitu kuna siku foleni itakamata watu 48hrs. Kuna siku watu washakaa kuanzia saa4 usiku hadi 11 asubuhi na siku ingine tano usiku hadi 11 asubuhi.
Dawa ni expressway ya kulipia waliyoizungumzia ijengwe na zile njia sita kimara-kibaha zifike Morogoro.
Tatizo wenye maamuzi hawana exposure. Kama imewezekana kujenga sgr inashindikana kujenga proper highway?
Wenye maamuzi wanapiga king'ora unakaa pembeni wao wanapita tu.

Nyie mtafuata sheria zote.
 
Kweli kabisa mkuu wale vijana ni wanauza karanga zao masaa yote!

Cha kufurahisha zaidi ni kwamba zile karanga wamezichambua kwa uweledi wa hali ya juu!
Unaweza kuzitafuna hata gizani bila shida..

Hiyo ni njia yangu kuu kwenye kusaka ugali so mara kadhaa nimelala pale baada ya kukuta parking ya ruaha mbuyuni imejaa..
In my next road trip to Iringa, ntasimama kununua karanga na mimi. Niwaunge mkono vijana wetu wanaaopambana.

Ila Mahindi ya kuchoma pale baada ya kupandisha Kitonga sinunui! Yaani wote wauzaji na wanunuzi kwenye magari mpaka washike shike muhidi wote - eti wanachagua; Nilitaka kutapika kwa kuangalia tu what happened~
 
In my next road trip to Iringa, ntasimama kununua karanga na mimi. Niwaunge mkono vijana wetu wanaaopambana.



Ila Mahindi ya kuchoma pale baada ya kupandisha Kitonga sinunui! Yaani wote wauzaji na wanunuzi kwenye magari mpaka washike shike muhidi wote - eti wanachagua; Nilitaka kutapika kwa kuangalia tu what happened~

Pls do that, utalii wa ndani unasaidia sana hizi less privilege family
 
Mimi humu ni msindikizaji tu sijui kama Kuna siku nitamiliki gari yangu binafsi kila nikipiga hesabu naona daah sio leo wa kesho..kila la heri mnaomiliki vyombo.
Weka nia ya kumiliki usafiri wako, usikate tamaa kwenye utafutaji pia..

Hali ya kutokuwa na gari isikufanye ujione msindikizaji, zaidi iwe ni chachu kwenye mapambano yako!!!
 
In my next road trip to Iringa, ntasimama kununua karanga na mimi. Niwaunge mkono vijana wetu wanaaopambana.

Ila Mahindi ya kuchoma pale baada ya kupandisha Kitonga sinunui! Yaani wote wauzaji na wanunuzi kwenye magari mpaka washike shike muhidi wote - eti wanachagua; Nilitaka kutapika kwa kuangalia tu what happened~
Hope utazifurahia sana hizo karanga mkuu!!

Yale mahindi hata mimi nayaogopa mkuu, nikiwa na hamu na mahindi choma huwa namwambia amenye kisha achome nikiwa naona..

Hako kakituo wanakochoma mahindi baada ya kumaliza mlima, kanaitwa IKOKOTO!!
 
Dom to moro chap!
IMG_20230221_123704.jpg
 
Back
Top Bottom