Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Ndio maana ikaitwa ni shirki.
Kwasababu kuna kitu nje ya dini unakifanya japo unatumia maandiko yake.
Miaka ya nyuma sana, ndani nilikuta kitabu , kile kitabu kiliandikwa kama mashairi flani na wazee wa kiislamu wakiomba Sadam Hussein aliyekuwa rais wa Iraq anyongwe.

Ilikua kabla hata ya US kuivamia Iraq, ni kijitabu kidogo nilikisoma juu juu nikakiacha.

Baada ya Saddam kukamatwa na US akanyongwa kweli.
Hapo niliamini ..maombi yapo.

Nilikitafuta kile kitabu sikupata kukiona tena, nahisi kilikua cha mzee wangu.

Kitabu kizima kilikua ni maombi ya Saddam Hussein anyongwe.
 
Hakuna cha albadiri wala albajoto mimi ni muislamu na nimechukizwa sana na hichi kitendo ila kusema ukweli izo dua za albadiri sijui albajoto hamna lolote zaidi ya watu kufanya ushirikina tu

Muislamu wa kweli anoijua vizuri dini yake hafanyi huo upuuzi
Albadiri ipo mzee sema tu ule ni ushirikina au uchawi.....na inategemea kwa unaemwendea amajipangaje kwa mashambulizi.
 
Mkuu kesho kutwa hapa tu natimiza miaka 40 , hizi stories za chai kwenye dini hata mimi nilikua maarufu
Wallah Mkuu, siwezi kuweka kila kitu open kwa sababu nina verification identity, amini ninachokuambia. Usijichanganye ukakutana na Wajuvi wa mambo utaniambia na ushahidi upo maeneo ya kwetu huku Makumbusho viliibiwa vifaa vya Salon ya kike likawekwa tangazo kama kutoa taarifa
 
Inafanya kazi endapo ukionewa ,kuna bodaboda walichoma gari ya mpemba moto aisee ni noma bodaboda waliiona ngondoigwa walipukutika wote kila siku walikuwa wanakula "BUYU" mmoja baada ya mmoja.

KUna jamaa yangu alikuwa na duka sehemu flani hivi akavamiwa majambazi yamamuibia fedha ,jamaa akaenda kuwapiga tego la ndizi aiseee walipukutika wote.
Hakusoma Albadiri, albadiri haipo
 
Inafanya kazi endapo ukionewa ,kuna bodaboda walichoma gari ya mpemba moto aisee ni noma bodaboda waliiona ngondoigwa walipukutika wote kila siku walikuwa wanakula "BUYU" mmoja baada ya mmoja.

KUna jamaa yangu alikuwa na duka sehemu flani hivi akavamiwa majambazi yamamuibia fedha ,jamaa akaenda kuwapiga tego la ndizi aiseee walipukutika wote.
Kuna watu wanakataa haya mambo wanajisifu kabisaa kwamba wao hawagusiki nawaangalia naaamua kunyamaza ,kuna watu tumeona makubwa dunia hii hiyo ya ndizi inafanana na jani la mkonge lile ndio baya kuliko kwa sababu hata kama sio mshirikina unamaliza ukoo mzima kwa afya ya jamii sitaweka yote hapa
 
Wallah Mkuu, siwezi kuweka kila kitu open kwa sababu nina verification identity, amini ninachokuambia. Usijichanganye ukakutana na Wajuvi wa mambo utaniambia na ushahidi upo maeneo ya kwetu huku Makumbusho viliibiwa vifaa vya Salon ya kike likawekwa tangazo kama kutoa taarifa
Mkuu kwa umri wangu na mambo niliyoshuhudia haya mambo ni stories tu hayana maana.
 
Kuna watu wanakataa haya mambo wanajisifu kabisaa kwamba wao hawagusiki nawaangalia naaamua kunyamaza ,kuna watu tumeona makubwa dunia hii hiyo ya ndizi inafanana na jani la mkonge lile ndio baya kuliko kwa sababu hata kama sio mshirikina unamaliza ukoo mzima kwa afya ya jamii sitaweka yote hapa

Hatari ni noma ,ogopa wapemba ni hatari kwa hayo mambo...Kama hawaamini wamle mke wa mpemba.
 
Sio kweli hmna chochote ni ushirikina tu kma wengine wanavoenda kwa waganga
kuna kipindi fulani kuna watu nawajua waliiba vito vya thamani ..na mm siri nikiijua .wakaitwa hao mashehe kusoma albadiri .mpk leo wale watu wanadunda tu hakuna cha uchizi au kufa ..toka pale sikuamini kitu..na wote tulilambishwa dawa hola hakuna alodhurika nawez na nawajua
 
Wewe huwa ni Mstaarabu na Muelewa katika Dini hupaswi kuuliza swali kama hilo....kuna haya katika Quran inayohusu kumsomea Mtu Kifo?

Twende taratibu
Quran ni kitabu cha mwongozo na rehema kwa wanadamu wote, na haifundishi uhasama, laana, au kumtakia kifo mtu mwingine. Badala yake, inasisitiza juu ya huruma, msamaha, na haki.
 
Kutoka Tanga inaripotiwa kuwa wazee wa Tanga wamepanga kusoma dua ya kushitakia almaarufu kama albadil kwa walioshiriki kumuua mzee mwenzao Alli Mohamed Kibao.

Watakaosomewa duwa hiyo ni wale waliopanga njama za maauaji,walioshiriki kumteka,waliomuua,waliofahamu mpango mzima wa mauaji hayo,nk

Kwenye suala la duwa ukiondoa wazee wa Pemba basi wanafuata wazee wa Tanga

PIA SOMA
- TANZIA - Dar: Ally Mohamed Kibao, kiongozi wa chadema auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
Nitachangia mahitaji Yoyote
 
Wazee wa tanga wameamua kupiga kurujuan,Yan aliyepanga,aliyefanya,aliyesababisha,alina kutoa wazo wote ni kurujuan,na sisi huku kwa msisi tunajiandaa jmosi.safi sana
 
Back
Top Bottom