Wazee wa Yanga wanaomba kukutana Rais Samia kulalamikia adhabu ya Manara..Wanajua madhara ya kitendo hicho?

Smart AJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2022
Posts
5,564
Reaction score
5,884
Iwapo mama Samia au hata Waziri wa Michezo atatoa maamuzi juu ya kesi hiyo basi kitachotokea kitaitwa ”SERIKALI KUINGILIA MPIRA WA MIGUU”.

Kosa hilo likiwafikia wakuu wa soka FIFA, basi TFF inakula ban kama ligi ya Zimbabwe..

Coz ni marufuku Serikali kuingilia maamuzi ya chama au shirikisho la soka nchi yoyote ma adhabu yake huwa kubwa.

Ikumbukwe Wazee wa Yanga walishawahi kutaka kuonana na mama Samia ila nadhani hawakufanikiwa.

WAZEE WA YANGA MTAUPOZA MPIRA WA BONGO.
 
Si hivyo tu...

Tujenge taasisi.

Wazee wa Yanga watambue tunajaribu kujenga jamii inayotegemea maamuzi, taratibu, na mifumo ya taasisi za umma badala ya huruma za kiongozi mmoja mmoja.

Hivi ni kwa nini ma Jaji Wakuu na Wasajili wa mahakama za nchi hii hawakerwi na tabia hizi za jamii kuwavuka wao, na wala hata siku moja hawatoi tamko la kualika watu kwenye taasisi za kisheria kutatua matatizo ya migogoro ya haki?
 
Rais anao washauri wanaolewa hawezi akaingia mkenge wa hao vichaa
 
.
 
Hao Wazee hawajajikusanya Wenyewe bali ni Jeuri wanayopewa na Mstaafu wenu wa Mkoa wa Pwani ambaye ana Influence Kubwa ya Kiushawishi katika Awamu hii pamoja na Mama Karume kutoka Kwao Kisiwani Zanzibar.

Wanachokifanya hapa hawa Wazee ni Kumlazimisha Mama nae awapende na awapendelee Yanga SC ili iwe ni Kazi rahisi kwa Wanayanga walioko Serikalini akina Waziri Nchemba, Mzee Mkuchika, Manaibu Mavunde na Ridhiwani nao wasaidie katika Kumshawishi ili Rais wa TFF Karia atishwe na Kamati ya Maadili ya TFF itengue hiyo Adhabu.

Niliwahi kuonya huko nyuma kuwa Rais Samia akae mbali na kulazimishwa kuwa ( awe ) mwana Yanga SC kwani itakuwa na Athari Kubwa Kwake Kiutawala, Kiushawishi na hata Kiusalama vile vile kutokana na Nguvu Kubwa ya hivi Vilabu viwili ila sikueleweka na Wapumbavu wengi ila taratibu nilichokiona sasa kinakuja.

Anayeharibu Mpira wa Tanzania kwa sasa kwa kupitia Kampuni yake inayosimamiwa na GSM ni Mstaafu wenu wa Kikatiba kutoka Mkoani Pwani na asipoangalia au Watu wa TISS wasipoliingilia kati kwa kuacha Haki itendeke, Sheria zifuatwe na Mpira uchezwe kuna Machafuko makubwa na Hatari fulani GENTAMYCINE naiona.

Sisi wana Simba SC tunawasubiri tu wamalize Kuhangaika na huu Upumbavu Wao mkubwa ila Rais Samia akikubali tu kuingia katika huu Mtego anaotegwa na hawa wana Yanga basi ajue Safari yake ya kuwa Rais itakuwa na Misukosuko mingi, ataathirika mno Kisiasa na atakuwa ameshaleta Mpasuko mkubwa wa Kisiasa nchini kwani nasi wana Simba SC tutaamua kuwa kwakuwa Yeye anaipendelea Yanga SC kutokana na Rangi zake Kufanana na za Chama chake cha CCM basi nasi Simba SC tutakubaliana rasmi Wote tuwe wana CHADEMA ambao 85% ya Rangi yao ( zao ) inafanana na ya Klabu ya Simba.

Namalizia kwa Kukuuliza Swali ni kwanini Kipindi cha Hayati Rais Dkt. Magufuli Maamuzi kama haya dhidi ya Yanga SC yalipokuwa yakitokea ulikuwa ( hukuona ) hawa Wazee wa Yanga SC wakitishia kwenda Kuonana nae ( Hayati Rais Dkt. Magufuli ) pale ( hapo ) Ikulu?

Siasa ni Siasa na Soka ni Soka sawa?
 
Mada nyingine bhana! Hao Wazee wa Yanga ndiyo akina nani? Na wameomba kukutana lini na Rais? Kiongozi wao ni nani?

Hivi huoni kabisa huu uzi wako umejaa bla bla! porojo na tetesi zisizo na kichwa wala miguu!
 
Alichowahi kukisema Haji mwenyewe kwamba wenye akili Yanga ni wawili tu (Sunday Manara na Kikwete) naona kinazidi kujidhihirisha kila kunapokucha.



Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Na aliyekuwa Kocha Mkuu Wao Luc Eymael ( Raia wa Ubelgiji ) aliwahi kusema ( ipo YouTube ) kuwa Yanga SC wote ni Nyani, Mbwa na Sokwe.

Ninaomba niishie tu hapa tafadhali!!
 
Ni sawa naona kama Taifa tunahitaji default kwenye mpira wetu labda tutakuwa na heshima

Natamani tule Ban hata ya miaka 10 kwanza ili tukirudi tuwe na heshima na huu mpira katika kuuongoza
Kutokana na huu Upuuzi wa hawa Wazee wa Yanga SC na Rais Samia natamani isiwe tu hiyo Miaka yako 10, ila ikiwezekana iwe hata miaka 50 kabisa tu Mkuu ili tukome.
 
Wana Simba SC kwa hili la Wazee wa Yanga SC 'tunamzoom' tu na akithubutu tu kuingia katika Mtego wao ajue amesharibu Soka la Tanzania, FIFA itaingilia, Tanzania tutafungiwa na Sisi wana Simba SC wote hatutokuwa na Imani nae tena, nchi haitotawalika na hata Urais wake unaweza kumtokea Puani.

Awe makini mno na hili na akikurupuka nalo kwa Kushawishiwa na Mstaafu wa Mkoani Pwani ajue atakuwa responsible kwa negative Impact yake na asisahau tu kuwa 95% ya Wana Simba SC ni Wasomi ( Intellectuals ) wa Tanzania na huko Yanga SC Wasio na Akili ni almost 98% hivi.
 
Kama nchi itakula ban kisa wazee kuonana na rais, je mchengelwa alietoa huku kwa manara hakuingilia uhuru wa tff?
 
Hii timu bhana yaani kulialia mpaka inakera mara mama, waziri, caf, fifa sijui kujitoa kwenye ligi Bora isajiliwe netball
Sasa kama wana akina Bi. Aziza na Bi. Joyce kwanini wasiwe Wanalialia Mkuu? Kwani Wewe ukiwa 'Unambaioloji' Shemeji ( Shemela ) yetu Bi. Fulani huwa halii?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…