Wazee wa Yanga wanaomba kukutana Rais Samia kulalamikia adhabu ya Manara..Wanajua madhara ya kitendo hicho?

Wazee wa Yanga wanaomba kukutana Rais Samia kulalamikia adhabu ya Manara..Wanajua madhara ya kitendo hicho?

Tupigwe ban tu. Haiwezekani Karia awe juu ya sheria aa TFF
 
Yanga viongozi na mashbiki wake na we mleta mada wendawazimu, rais aache mambo ya msingi asikilize wapuuzi kama hawa
 
Wapi alitoa hukumu kwa Manara? Yani kuwaasa viongozi kufuata sheria na nidhamu ni kosa? Au na wewe ni Mzee wa Yanga?
Vipi vita vya Ukraine, Russia anaendelea kula kichapo?
 
Mada nyingine bhana! Hao Wazee wa Yanga ndiyo akina nani? Na wameomba kukutana lini na Rais? Kiongozi wao ni nani?

Hivi huoni kabisa huu uzi wako umejaa bla bla! porojo na tetesi zisizo na kichwa wala miguu!

Una simu janja bro??basi skizaga hata kipenga xtra ya kindoki tu
 
Hii timu bhana yaani kulialia mpaka inakera mara mama, waziri, caf, fifa sijui kujitoa kwenye ligi Bora isajiliwe netball

Mwakalebela aliwahi kusema watawaomba caf waanzie ugenini...sidhani kama ni suala la kuomba ila ni suala la points tu sjui kama hawajui sheria au wanataftaga tu kiki
 
Kama nchi itakula ban kisa wazee kuonana na rais, je mchengelwa alietoa huku kwa manara hakuingilia uhuru wa tff?

Sikumskia akimtaja manara...bro wanaelewa kuwa ni hatari sana serikali kujihusisha na soka ndo mana hata sku ile kwenye hafla ya tuzo hakumtaja manara moja kwa moja
 
Huyo Mshauri ndiyo ( Ndiye ) aliyeiharibu na Kuifelisha Tanzania Kimaendeleo kati ya mwaka 2005 hadi 2015 na Watanzania na Tanzania ilidharaulika kiasi cha hadi kuonekana ni Gulio la Wapumbavu na Ghala Kuu la Kuhifadhia Dawa za Kulevya kwa Bara la Afrika na hasa hasa Ukanda wa EAC na ule wa SADC.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]we jamaa unajua kuwa zee la msoga lipo humu jei efu??
 
Haya ndio madhara ya Mpira kuongozwa na wapumbavu hapa nchini

Naitamani sana Ban ya FIFA kwenye mpira wetu

Na sidhani kama serikali itaruhusu soka liwe ban coz kuna faida nyingi sana kwa nchi kupitia soka..achilia mbali wadhamini na warusha matangazo kuna akina sisi ambao ni wapenda soka hatutafurahia suala hilo.
 
Iwapo mama Samia au hata Waziri wa Michezo atatoa maamuzi juu ya kesi hiyo basi kitachotokea kitaitwa ”SERIKALI KUINGILIA MPIRA WA MIGUU”.

Kosa hilo likiwafikia wakuu wa soka FIFA, basi TFF inakula ban kama ligi ya Zimbabwe..

Coz ni marufuku Serikali kuingilia maamuzi ya chama au shirikisho la soka nchi yoyote ma adhabu yake huwa kubwa.

Ikumbukwe Wazee wa Yanga walishawahi kutaka kuonana na mama Samia ila nadhani hawakufanikiwa.

WAZEE WA YANGA MTAUPOZA MPIRA WA BONGO.
Yanga ina wazee wajinga kuwahi kutokea
 
Iwapo mama Samia au hata Waziri wa Michezo atatoa maamuzi juu ya kesi hiyo basi kitachotokea kitaitwa ”SERIKALI KUINGILIA MPIRA WA MIGUU”.

Kosa hilo likiwafikia wakuu wa soka FIFA, basi TFF inakula ban kama ligi ya Zimbabwe..

Coz ni marufuku Serikali kuingilia maamuzi ya chama au shirikisho la soka nchi yoyote ma adhabu yake huwa kubwa.

Ikumbukwe Wazee wa Yanga walishawahi kutaka kuonana na mama Samia ila nadhani hawakufanikiwa.

WAZEE WA YANGA MTAUPOZA MPIRA WA BONGO.
Yanga ina wazee wajinga kuwahi kutokea
 
........kwa mpira wetu huu wacha tu serikali iingilie; adhabu inatumika kama njia ya kukomoana badala ya kurekebisha.

Hiyo kamati ilikuwa na uwezo wa kumrekebisha Manara kwa kumtoza faini let say 3,000,000 kwa kuwa alionesha uungwana kwa kuomba msamaha.

Lakini sasa kwa kuwa mwenyekiti wa kamati ana mgongano wa kimaslahi na klabu nyingine wakaamua kushusha nondo kimhemko. Hii haina faida ktk soka

Kamati ijitathmini kwa undani maamuzi yake kama yana lengo la kurekebisha au kukomoana
Hopeless
 
Tusiruhusu siasa ikaingia kwenye michezo yetu kwani madhara yatakayotokea mbele ya safari yatakuwa makubwa sana hasa soka au baadhi ya timu zikija kujifungamanisha na vyama vya siasa. Kwa hili la wazee wa Yanga kama kweli wanataka kwenda kumuona raisi kwa ajili ya suala la kufungiwa Manara basi wasaidizi wa raisi wamshauri aachane nalo. Taratibu zifuatwe kupitia ngazi husika kwa Manara kukata rufaa kama hajaridhika na adhabu aliyopewa na TFF.

Manara ni mwanafamilia wa mpira kama wanafamilia wengine wa mpira na anatakiwa afahamu hivyo na asitake kupewa umaalumu fulani. Njia ni rahisi sana akate rufaa ngazi ngazi kwa ngazi mpaka apate haki yake kama anaona ameonewa. Kama atashinda rufaa basi adhabu zitapunguzwa au kuondolewa kabisa kwa hiyo sioni sababu za hao wazee kwenda kumsumbua raisi kwa suala ambalo linatakiwa kukatiwa rufaa. Vinginevyo hao wazee aidha wanauelewa mdogo katika mambo ya soka au kuna maslahi wamepata kwa kuibeba ajenda ya Manara kutaka kuipeleka ikulu.
 
Back
Top Bottom