BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Zanzibar, Riziki Pembe Juma amesema ili kukomesha vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, ipo haja wanaume wanaofanya vitendo hivyo kuhasiwa.
Amesema licha ya sheria kuwapo na serikali na wadau wengine kupambana dhidi ya vitendo hivyo lakini bado vinaendelea kushamiri.
Ametoa kauli hiyo leo Novemba 25, 2022 wakati wa kufungua siku 16 za uanaharakati kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto katika ukumbi wa Abdulwakil mjini Unguja, Zanzibar, ambapo mgeni rasmi ni Mke wa Rais wa Zanzibar, Mariam Mwinyi.
“Niombe ombi maalumu kwako utufikishie ombi hili kwa Mheshimiwa Rais (Hussein Mwinyi), tunajua sheria zipo na zinafanya kazi yake lakini bado wanaofanya vitendo hivi wanaona kama sheria zinawachombeza,” amesema.
“Tungalie namna bora ya kuwapo na adhabu mbadala badala ya mtu kufungwa miaka 30 kwenda kuitia hasara Serikali kule ndani bado afikirie wote wanaodhibitika kufanya hivyo, wahasiwe,” amesema.
Huku akiwahoji washiriki wa mkutano huo wanasemaje na wao kumuitikia ndiyoooo…Waziri Pembe amesema “kwakweli tumechoka, tumechoka tumechoka, wenzetu, ukifanyika mfano wa wabakaji watatu tunaamini wanaume wote itakuwa funzo kwao na wataacha tabia hiyo,” amesema.
Ameongeza kuwa “Tunaomba sana, kama wanaona kubaka ni haki basi na kuhasiwa iwe ni haki,” amesema.
Hata hivyo amesema wizara imeanzisha kitengo maalumu cha kuratibu vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto kwa kushirikina na wadau na wanaharakati na jumuiya za wanawake na wanaume kuona wanasimama pamoja kupinga vitendo hivyo.
Vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto vilishamiri mwaka 1991.
Kutoka na hali hiyo, lianzishwa kampeni ulimwenguni kote ambayo ilitokana na mkutano wa wanaharakati kufuati mkutano uliofanyika Kolombia Amerika kati ya Novemba 18 hadi 21 mwaka 1991 na kuweka maazimio ya kupinga vitendo vya ukatili.
Mkutano huo uliazimia na kuchagua siku 16 za kila mwaka kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 ambayo ni siku ya kimataifa ya Haki za binadamu kwa lengo la kuhusisha ukatili na ukiukwaji wa haki za binadamu ulimwenguni kote kuwa siku ya kimataifa dhidi ya vitendo vya ukatili na udhalilishaji.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Abeida Rashid Abdalla amesema faraja imepotea miongoni mwa jamii kutokana na vitendo hivyo.
MWANANCHI
Amesema licha ya sheria kuwapo na serikali na wadau wengine kupambana dhidi ya vitendo hivyo lakini bado vinaendelea kushamiri.
Ametoa kauli hiyo leo Novemba 25, 2022 wakati wa kufungua siku 16 za uanaharakati kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto katika ukumbi wa Abdulwakil mjini Unguja, Zanzibar, ambapo mgeni rasmi ni Mke wa Rais wa Zanzibar, Mariam Mwinyi.
“Niombe ombi maalumu kwako utufikishie ombi hili kwa Mheshimiwa Rais (Hussein Mwinyi), tunajua sheria zipo na zinafanya kazi yake lakini bado wanaofanya vitendo hivi wanaona kama sheria zinawachombeza,” amesema.
“Tungalie namna bora ya kuwapo na adhabu mbadala badala ya mtu kufungwa miaka 30 kwenda kuitia hasara Serikali kule ndani bado afikirie wote wanaodhibitika kufanya hivyo, wahasiwe,” amesema.
Huku akiwahoji washiriki wa mkutano huo wanasemaje na wao kumuitikia ndiyoooo…Waziri Pembe amesema “kwakweli tumechoka, tumechoka tumechoka, wenzetu, ukifanyika mfano wa wabakaji watatu tunaamini wanaume wote itakuwa funzo kwao na wataacha tabia hiyo,” amesema.
Ameongeza kuwa “Tunaomba sana, kama wanaona kubaka ni haki basi na kuhasiwa iwe ni haki,” amesema.
Hata hivyo amesema wizara imeanzisha kitengo maalumu cha kuratibu vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto kwa kushirikina na wadau na wanaharakati na jumuiya za wanawake na wanaume kuona wanasimama pamoja kupinga vitendo hivyo.
Vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto vilishamiri mwaka 1991.
Kutoka na hali hiyo, lianzishwa kampeni ulimwenguni kote ambayo ilitokana na mkutano wa wanaharakati kufuati mkutano uliofanyika Kolombia Amerika kati ya Novemba 18 hadi 21 mwaka 1991 na kuweka maazimio ya kupinga vitendo vya ukatili.
Mkutano huo uliazimia na kuchagua siku 16 za kila mwaka kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 ambayo ni siku ya kimataifa ya Haki za binadamu kwa lengo la kuhusisha ukatili na ukiukwaji wa haki za binadamu ulimwenguni kote kuwa siku ya kimataifa dhidi ya vitendo vya ukatili na udhalilishaji.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Abeida Rashid Abdalla amesema faraja imepotea miongoni mwa jamii kutokana na vitendo hivyo.
MWANANCHI