Waziri Bashe acha kuchezea Kodi zetu kwa maono mfu! Kilimo siyo filamu

Waziri Bashe acha kuchezea Kodi zetu kwa maono mfu! Kilimo siyo filamu

Naomba ungeelewa maana ya fact na supposition. Supposition ya kilimo kinachotakiwa ni kile kisichohusisha jembe la mkono wala kuomba dua za mvua. Ni mechanized agriculture. Ofkoz, kwa nchi yetu itachukua muda kuwaondoa wakulima hao, lakini for sure lazima waondoke (phased out not kicked out) as time goes. Hili neno la wakulima wa vijijini tumelitengeneza tu lakini kiuhalisia yapasa neno wakulima wa vijijini na mjini lisiwepo. Just wakulima tu.

Hao wakulima wa vijijini watakaposhindwa kuingia kwenye mfumo rasmi Wana hiyari mbili. Kuingia contract ya kuzalisha kwa kiwango cha wakulima rasmi na kuwauzia au kuwa vibarua/wafanyakazi wa kilimo watimize mahitaji yao . Simply hivyo.
Kwani kilimo hakiwezi kuwa mechanized bila kuua wakulima wadogo ?

Unapoua wakulima wadogo zoezi lako litahusisha pia land grabbing siyo ?

Unafikri ukiondoa wakulima wadogo kwenye mfumo wa uzalishaji ni mfumo upi mpya ambao unafikri utaweza kuwa mbadala wa kulinda kundi hili lisife kwa njaa ?
 
Nashukuru kwa kusaidia kuuliza swali zuri sana maana maelezo yangu hayakueleweka!!
Kama vision ya BBT ni kuondoa wakulima wadogo kwenye mfumo wa uzalishaji basi mpango huu utakuwa ni mpango wa kishetani.

Na hautakiwi kuungwa mkono.
 
Bashe is doing for the sake of doing to impress, hii game alishindwa zamani sana..

Hizo hela za block farming angezipeleka kuanzisha na kuendeleza cooperative unions Wakulima wakope pembejeo huko... na serikali idai cooperative unions... sasa hizi blabla ni outdated and we will never go anywhere.
Hii ilishafeli huko nyuma. Walikopeshwaga wakaishia kufungwa na kujinyonga na kutoroka.
 
Mpango wa block farm ungefanikiwa kana ungehusisha wakulima wazoefu,bila ubaguzi wa umri!

Wakulima wenye uzoefu na mapenzi na kilimo ndio wanaweza kuvumilia suluba za kilimo!

Hawa wakulina wa kuchonga watamuangusha mno mh Bashe! Nia ya mh Bashe ni nzuri,lakini njia anayotumia ni mbaya!
Pengine vision ya mradi siyo kuboresha kilimo ila ni kupanua goli ili wafunge hata kama wamefumba macho hii nchi haishiwi maajabu.
 
Kama vision ya BBT ni kuondoa wakulima wadogo kwenye mfumo wa uzalishaji basi mpango huu utakuwa ni mpango wa kishetani.

Na hautakiwi kuungwa mkono.
Nimeuliza kule juu kwamba inakuwaje siyo wakulima asilia ndiyo wawechukuliwa badala yake wamechukuliwa wapya kabisa!!
 
Nadhani Waziri ana nia njema ya kuanzisha Kilimo biashara block farming kwa baadhi ya mazao kama Katani inafanya vizuri kutokana na soko la uhakika.Moja ya component za BBT ni pamoja na marketing ya mazao kwa hiyo nasema kazi iendelee
 
Vijana wametolewa mjini, wengine. Ni uvccm wamejazwa , yako matrekta , wataystumia wapi.

Bashe alikuwa anwazo zuri sana Lakini limekuwa na upendeleo wa itikadi kama chama ,siasa ,ukanda,

Na kuachia wahusika wakikosa nafasi.


Mfano apo wanafundishwa kulima zabibu lakini Kuna vijana waMEtolewa Dar, SS sijui wakirudi wataenda kulima jagwan
Kila kitu kina mwanzo wake, hao walioanza waacheni waendelee. Isingewezekana kuwa deploy vijana wote wa Tanzania kwa resources chache tulizonazo.

Believe in the process
 
Kila kitu kina mwanzo wake, hao walioanza waacheni waendelee. Isingewezekana kuwa deploy vijana wote wa Tanzania kwa resources chache tulizonazo.

Believe in the process
TuWaTakie heri
 
Hii nchi ina haribiwa na udalali tu, ka dalali uchwara hakana lolote zaidi ya sim mkononi kanakuthaminishia mali zako!

Unapaona pale mabibo sokon wale madalali uchwara wanakula pesa za wakulima na wafanya biashara kirahisi pumbavu kabisa.

Mimi najiuliza kama mtu una viazi vyako kutoka shamba,kwann kusiwe na utaratibu wa kuuza mwenyewe pale sokoni? mpaka umpe dalali yeye ndo auze alafu akate posho yake na hata kama umepata hasara yeye dalali hana hasara!! Yaani hata akiuza gunia 10 vingine vikaoza vyote hela ya dalali ipo pale pale! Huu si uchawi kabisa..

Ukipeleka mazao yako dar lazima umpe dalali auze bila hivo utarudi nayo ulikoyatoa,, waweke utaratibu mtu unakuja na viazi vyako labda unalipia tu ushuru unaingiza gari unauza mwenyewe sio upumbavu unaofanyika pale
 
Serikali inapaswa ije na mfumo ambao automatically utawatoa madalali kwenye mfumo. Hii itakuwa ahuen kwa mkulima
Halafu wala sio kitu complex. Ni portal tu kwa ajili ya wanunuzi na wakulima. Bei wanapanga wakulima wenyewe kila mtu na bei yake. Mwenye bei competitive anauza. Wateja wanaingia kwenye hio portal wanafanya contact na wauzaji.

Serikali ipige marufuku magenge ya udalali sokoni, kila mkulima auze na kununuzwa kupitia hio system. Hapo watawaweza.
 
Kila kitu kina mwanzo wake, hao walioanza waacheni waendelee. Isingewezekana kuwa deploy vijana wote wa Tanzania kwa resources chache tulizonazo.

Believe in the process
Sizungumzii vijana wote wa participate Kwa pamoja, mfano Hilo shamba darasa linalenga hasa zao la zabibu, Sasa kuchukuwa vijana ambao wanatoka maeneo ambayo haya zilishi Hilo zao Kwa wingi ama kabisa hawazalishi,
Sasa hapo tija itatoka wapi ndugu
 
Bashe is doing for the sake of doing to impress, hii game alishindwa zamani sana..

Hizo hela za block farming angezipeleka kuanzisha na kuendeleza cooperative unions Wakulima wakope pembejeo huko... na serikali idai cooperative unions... sasa hizi blabla ni outdated and we will never go anywhere.
Kivip Sasa hiyo
 
Sizungumzii vijana wote wa participate Kwa pamoja, mfano Hilo shamba darasa linalenga hasa zao la zabibu, Sasa kuchukuwa vijana ambao wanatoka maeneo ambayo haya zilishi Hilo zao Kwa wingi ama kabisa hawazalishi,
Sasa hapo tija itatoka wapi ndugu
Mkuu si wamesema wanawapa hayo masamba kwa kuwamilikisha labda mim ndio sijaelewa hiyo concept ya ile misheni
 
Back
Top Bottom