Waziri Bashe na wizara mnaandaa Watanzania kwa mipango ya upigaji

Waziri Bashe na wizara mnaandaa Watanzania kwa mipango ya upigaji

Jana tarehe 20 March 2023, Rais alifungua mradi wa mashamba ya pamoja, Mradi wa Kilimo wa Vijana. Sijui kama Waziri ana lengo zuri au ni kulifanya jina lake lisikike kila wakati mbele ya Rais kwa kujitambulisha kama mchapakazi. Kama ni mpango wa Wizara, basi ni muendelezo wa udanganyifu ulioanzia mambo ya Kilimo kwanza.

Wakulima wa nchi hii, zaidi ya 70%, wako vijijini. Huu ni upigaji wa wazi kabisa kuwashawishi vijana kwa kuwapa mashamba kama kambi ya JKT, ili washawishi wengine kuhusu kilimo. Hii ni hasara kwa wakulima. Waziri alianza na pikipiki za maafisa ugani ambazo hazionekani zilikwenda wapi na bado hazijaulizwa! Sasa amekuja na hili ambalo halimo hata kwenye mpango mkakati wa pili wa kuendeleza kilimo wa Wizara, ASDP II.

Huu ni upigaji wa wazi kabisa!
ndugu yangu hilo liko wazi kwa mtu yule anaetambua! Wengi hawajui kua io ni blueprint ya kuchakata fedha! Mimi kiukweli natamani kumjua mtu aliebuni hili wazo nimpe heshima yake! Jamaa ni kichwa aisee! Yaani hapa hadi escape root ya izo negative outcomes ipo tayari! Nawaonea wivu hawa jamaa watavoponda maisha kiulaini!
 
Chukulia huu mfano.

Watanzania wengi sana wanapenda maharage.

Mtaji wa tsh 10 billion.

Unajenga warehouse kubwa yenye kuajiri ata watu 500

Unapata industrial pressure cooker yenye uwezo wa kupika tani elfu kadhaa kwa siku.

Nitatoa biashara kwa mtu wa kuniuzia aluminium cans za size tofauti

Biashara kwa mtu wa kunitengenezea label za kwenye kopo

Nanunua ma lorry used kama 20

Biashara ya maharage ambayo nishayachemsha mtu kazi yake kuunga ipo sana; wanafunzi wa vyuo tu wana tosha achilia families with appropriate marketing mix yaani soko ni kubwa balaa la ndani tu. Tena hilo mashine unaweza chemshia ata vyakula vingine vya jamii ya kunde.

Kwa sababu nanunua kwa wingi na ku distribute mwenyewe naweza ata kupanga bei ya chini ambayo retailer asizidishe yeye apate na mimi nipate na iwe nafuu kwa mlaji.

Hapo nakuwa nimetengeneza ajira za wasomi na wasio wasomi, natoa biashara kwa biashara zingine (B2B), naanza kulipa kodi za PAYE, VAT, Income Tax ndani ya muda mfupi, nachochea mapato ya biashara zingine TANESCO umeme, vituo vya mafuta na si ajabu guest houses.

Sio huku kwenda kutupa hela ovyo kwenye kilimo, badala ya kuanza kufikiria kuanza kuongeza thamani ya kilichopo sasa.

Ni hivi Tanzania watu wenye hela wao wanachojua ni mabasi, hotels, ma lorry, bar/mgahawa, taxi, boda boda, maduka ya nguo na kuhonga.

Lakini mtu mwenye exposure uwezi kuwa na access ya mtaji Tanzania ukakosa cha kufanya kwenye kuongeza thamani kwa bidhaa za shambani; opportunities ni vast.

Ni muda wa serikali kufikiria viwanda wameshatupa hela za kutosha kwenye kilimo, viwanda vikiwepo watu watakimbilia mashambani wenyewe.

Kupata utajiri Tanzania na kufilisika ni ushamba. Sawa kuimba hujui, lakini Diamond Platnumz ambae ajamaliza ata darasa la saba akushinde na kwenye biashara huo sasa ni ufala.
Ndugu mayor naomba niwe rafikiako angalau naona tunaweza share vitu positive kama hivi! Akili kubwa ziko chimbo bado hazijaingia barabarani!
 
Tumpe tu nafasi, labda he has a way which isn't obvious to us...Chamsingi kilimo chetu kiweze kuleta tija. I pray for his success!
Kabla ya kumpa muda kwenye hili, kwa nn tusimpime kwenye mengine mfano mbolea ya ruzuku? Kwa nn hili tu? Bashe ni mtu wa maneno pasipo vitendo
 
Na hao matajiri watakaokuwa ma'boss' wa hawa vijana ni akina nani hasa?
Wamekwishapatikana katika mpango huo? Wamepatikana kwa njia zipi? Kulikuwa na tenda zilizotangazwa?

Na baadhi ya vijana hao wakulima wakikataa kuuza mazao yao kupitia kwa huyo "mnyonyaji", itakuwa vipi?

Hawa watanufaika kwa jasho la waTanzania wote kwa mikopo itakayolipwa na waTanzania?


Jibu lako lipo hapo hao watu hakuna Mwigulu kaenda U.K. kutafuta hao wawekezaji na juzi walikuwa S.A kwa shughuli hiyo hiyo ya kubembeleza wawekezaji wa kwenye mashamba makubwa.
 
Mimi kilichonishangaza ni hadi raisi kukubaliana na huu mradi Hadi kwenda kuuzindua
The woman is clueless, gullible na washauri wake personal wa maswala ya uchumi na biashara sijui ni hakina nani huko Ikulu hawana msaada wowote.

Wazimu mwingine upo nishati na huu uwekezaji wa renewable mtu anatakiwa awaambie huko serikalini stop pursuing that nonsense awahitaji kwa sasa hiyo miradi inayoenda dilute mapato ya TANESCO shirika lenyewe linaishi kwa ruzuku za walipa kodi.
 
The woman is clueless, gullible na washauri wake personal wa maswala ya uchumi na biashara sijui ni hakina nani huko Ikulu hawana msaada wowote.

Wazimu mwingine upo nishati na huu uwekezaji wa renewable mtu anatakiwa awaambie huko serikalini stop pursuing that nonsense awahitaji kwa sasa hiyo miradi inayoenda dilute mapato ya TANESCO shirika lenyewe linaishi kwa ruzuku za walipa kodi.
Huko kwenye nishati napo raisi amenishangaza sana, niliona akienda kuzindua mjadala wa watu kuanza kutumia gesi badala ya kuni na mkaa. Ilikua jambo la ajabu mno.

Nilikuuliza Ina maana raisi hajui kwa nn watu wanatumia kuni na mkaa badala ya gesi? Nchi maskini kama Tanzania bado raisi anashangaa kwa nn wananchi wake wanatumia mkaa badala ya gesi?

Kilichotakiwa kuanza ni kuboresha uchumi wa nchi na wananchi wake, alafu ndio uwaeleze masuala ya kutumia gesi badala ya mkaa.
 
Kumbe na wewe ulikuwa juani unasubiria hayo mashamba bloangu?
Unajua hili taifa la Tanzania kuna kiongozi alishawai kumwambia Nyerere kwamba Anaongoza maiti sio binadamu walio hai.
Sisi ambao sio maiti tunajitahidi kuoji,kupinga na kutafta mwafaka mzuri ili wasiendelee kutuona maiti wote ila UNAIBUKA TENA WW MAITI unaleta hoja za kishoga kisa unapewa buku 7.
 


Jibu lako lipo hapo hao watu hakuna Mwigulu kaenda U.K. kutafuta hao wawekezaji na juzi walikuwa S.A kwa shughuli hiyo hiyo ya kubembeleza wawekezaji wa kwenye mashamba makubwa.

Inanibidi kujiuliza sana na hizi hatua wanazochukua hawa viongozi hii tabia ya kujiuza kama bidhaa huko nje. Bidhaa bora, ambayo kwa kila kigezo Tanzania ni bidhaa bora kabisa kati ya mataifa mengi duniani; kwa nini ijifanye kuwa bidhaa hafifu kiasi hiki cha kujitembeza kama malaya kila sehemu.

Hawa viongozi kama siyo kuwadharau na kuwaona wanachi wao kuwa chini ya viwango vya watu wengine duniani, kwa nini hawana imani na uwezo wa hawa waTanzania kuleta maendeleo ndani ya nchi hii?

Mpango huu wa mashamba, kwa mfano, kuna nchi yoyote duniani iliyowahi kuutumia kama model ya kuleta maendeleo, au ni mpango tu umebuniwa na kufanyiwa majaribio kwa Tanzania?

Ni nchi gani duniani ilileta mageuzi makubwa kwa kutegemea wawekezaji toka huko nje, huku wananchi wake wakiambulia makombo na hisani za hao wanaoitwa wawekezaji?

Mwigulu na wenzake wote, na hasa huyo mama anapashwa kutumia muda wake mwingi kufanya kazi na waTanzania, hapa hapa, na hasa huko vijijini kuliko kwenda kujitembeza kama malaya huko nje.
Wananchi wetu ndio wanaohitaji mazingira mazuri ya kuwezesha juhudi zao kuzaa matunda, siyo kwenda kutafuta watu watakaotuletea matatizo zaidi na kututawala nyumbani kwetu wenyewe. Mazingira ya kuwavutia hao wawekezaji ni mabadiliko yatakayoletwa na juhudi za waTanzania kwa kazi zao wanzozifanya.

Wachina hawakusubiri au kwenda kujitembeza kutafuta wawekezaji. Wawekezaji walipigana vikumbo wenyewe kwenda China walikuoona kuna kazi na na mazingira mazuri yaliyowahusu wananchi wa huko.

Hawa viongozi wana tabia za kitwana sana, na wanaifanya nchi hii iwe kama ya watwana.
 
Kipindi cha Rais Mstaaf Mwinyi kulikuwa na mradi wa mbogamboga kule Tanga (sina uhakika na mikoa mingine) ukiitwa 4H (Head, Hands, Heart and Healthy). Mradi huu ulikuwa pamoja na mambo mengine ukiwajenga watoto wadogo hususan wa shule za msingi kukipenda na kukithamini kilimo kama sehemu ya kujikwamua kimaisha, kuongeza kipato na kuimarisha afya.

Kwangu mimi hii ndio ilipaswa kuwa BBT (Build Better Tomorrow) na sio hii ya muundo wa Bashe! Isitoshe ni wanasiasa hao hao wanaosema vijana ni Taifa la leo, sasa kwaninini tusiwaandae watoto kuwa Taifa la kesho lenye kupenda kilimo.

Anyway, let's build better tomorrow but we have to eat today!
 
Unajua hili taifa la Tanzania kuna kiongozi alishawai kumwambia Nyerere kwamba Anaongoza maiti sio binadamu walio hai.
Sisi ambao sio maiti tunajitahidi kuoji,kupinga na kutafta mwafaka mzuri ili wasiendelee kutuona maiti wote ila UNAIBUKA TENA WW MAITI unaleta hoja za kishoga kisa unapewa buku 7.
Umepanik bloangu eeeh??
Pole mnooo,
Kwa kuwa huna subra,utaendelea kuwa ni mlalamikaji na msindikizaji tu kwa umauti wa subra ulionao.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom