Waziri Bashe na wizara mnaandaa Watanzania kwa mipango ya upigaji

Waziri Bashe na wizara mnaandaa Watanzania kwa mipango ya upigaji

Kilimo kikianza kutoa hela kuliko betting watu watakimbilia tu.

Uhovyo wa kilimo chetu ni ile unpredictability of production wakati huo hakuna measures za kumnasua mkulima na majanga.

Maana yake uwekezaji wake ni kama kwenda kuvua samaki kwa mikono kwenye dimbwi lenye samaki na vyura, it is either uibuke na samaki au Chura.

Hatuwezi kutoka kwenye kilimo kwa namna anayoifikiria Bashe never.
Omba basi wakuteue utende miujiza
 
Jana tarehe 20 March 2023, Rais alifungua mradi wa mashamba ya pamoja, Mradi wa Kilimo wa Vijana. Sijui kama Waziri ana lengo zuri au ni kulifanya jina lake lisikike kila wakati mbele ya Rais kwa kujitambulisha kama mchapakazi. Kama ni mpango wa Wizara, basi ni muendelezo wa udanganyifu ulioanzia mambo ya Kilimo kwanza.

Wakulima wa nchi hii, zaidi ya 70%, wako vijijini. Huu ni upigaji wa wazi kabisa kuwashawishi vijana kwa kuwapa mashamba kama kambi ya JKT, ili washawishi wengine kuhusu kilimo. Hii ni hasara kwa wakulima. Waziri alianza na pikipiki za maafisa ugani ambazo hazionekani zilikwenda wapi na bado hazijaulizwa! Sasa amekuja na hili ambalo halimo hata kwenye mpango mkakati wa pili wa kuendeleza kilimo wa Wizara, ASDP II.

Huu ni upigaji wa wazi kabisa!
Ni waziri ambaye ameua kilimo kabisa kazi yake ni kupiga kelele tu
 
Ni mwendo wa kuzindua tu, kabla hili halijafika popote wanafanya hafla ya kuzindua lingine, Ni hafla za uzinduzi kwa kwenda mbele. Ikitoka hafla inafata warsha inafata semina , afu tunarudi Tena kwenye hafla. Kukagua kwamba hili limefikia wapi hamna.
Umesahau kusema kote umo pesa zinatafunwa sio kwamba bure bure ni pesa za Kodi zinatumika
 
Ni waziri ambaye ameua kilimo kabisa kazi yake ni kupiga kelele tu
Kuna mbunge alimpinga bungeni huwezi ukaenda kumchukua kijana amesomea udaktari unamwambia eti kwa kua haujapata kuajiriwa Basi akalime au kijana kasoma Tehama unamwambia kwa kua haujapata kuajiriwa twende ukalime ingawa KILIMO kinalipa
 
Nguvu kubwa imewekwa nje ya kilimo chenyewe. Bahati mbaya raisi sio mjuzi sana na wala hana tatizo na Hilo
Wizara imenunua Land cruiser za kutosha kwa ajili ya block farming, inashangaza sana
Mkuu vipi na huko Norway, kuna upuzi na utopolo kama huu?
 
Yaani mradi ndo kwanza umeanza alafu unasema upigaji alafu wala huweki wazi huo upigaji with facts and figures.
Tz tuna safari ndefu sana kufika tuliko kila mtu mjuaji.
Au usikute nawe ndo wale wamekosa nafasi kwenye ilo kundi la vijana
 
Bashe maneno mengi nimekuja kumgundua kwenye deliverance yuko nyuma mno, anaweka viterm vyake vya uongo na kweli unaweza kusema ni akili kubwa kumbe kichwani hamna kitu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] "It is very danger".Yule jamaa msanii sana!
 
kwa maono yangu naona bashe ndio moja ya mawaziri waliokuja kivingine katika suala la kilimo na kulibeba jukumu la waziri(kazi kuu ya waziri ni kuja na sera yenye utofauti na sio upuuzi wa kufokafoka na kutumbua au zima moto)
ni vyema kuwapa mtaji na kuwahakikishia soko wakulima vijana waliosomea au wenye uzoefu ili waajiri watanzania wengine.
Lengo la program hii liwe halisia na kweli tupu yaani lazima tuwe na "must made " multbillions farmers ambao watawezeshwa kuajiri watanzania,watakaozalisha malikilimo itakayouzwa nchini (food securitu purpose) na nje ya nchi(business purpose) .
zimepita dhana nyingi sana kuhusu kilimo hebu sasa tutengeneze "mafisadi" wa agro business ...ma settlers wa kibongo
wengi kila mkoa au kanda ambao wataenda "kutema" au kuvamia misitu iliyopo Africa .na pia tupate updates namna walivyoajiri na namna watakavyo -encroach soko la EaC na SADC.

TISS iwekee mkakati mahsusi katika hii dhana ya Bashe kikamilifu tunaweza kutoka hapa tulipo.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Inanibidi kujiuliza sana na hizi hatua wanazochukua hawa viongozi hii tabia ya kujiuza kama bidhaa huko nje. Bidhaa bora, ambayo kwa kila kigezo Tanzania ni bidhaa bora kabisa kati ya mataifa mengi duniani; kwa nini ijifanye kuwa bidhaa hafifu kiasi hiki cha kujitembeza kama malaya kila sehemu.

Hawa viongozi kama siyo kuwadharau na kuwaona wanachi wao kuwa chini ya viwango vya watu wengine duniani, kwa nini hawana imani na uwezo wa hawa waTanzania kuleta maendeleo ndani ya nchi hii?

Mpango huu wa mashamba, kwa mfano, kuna nchi yoyote duniani iliyowahi kuutumia kama model ya kuleta maendeleo, au ni mpango tu umebuniwa na kufanyiwa majaribio kwa Tanzania?

Ni nchi gani duniani ilileta mageuzi makubwa kwa kutegemea wawekezaji toka huko nje, huku wananchi wake wakiambulia makombo na hisani za hao wanaoitwa wawekezaji?

Mwigulu na wenzake wote, na hasa huyo mama anapashwa kutumia muda wake mwingi kufanya kazi na waTanzania, hapa hapa, na hasa huko vijijini kuliko kwenda kujitembeza kama malaya huko nje.
Wananchi wetu ndio wanaohitaji mazingira mazuri ya kuwezesha juhudi zao kuzaa matunda, siyo kwenda kutafuta watu watakaotuletea matatizo zaidi na kututawala nyumbani kwetu wenyewe. Mazingira ya kuwavutia hao wawekezaji ni mabadiliko yatakayoletwa na juhudi za waTanzania kwa kazi zao wanzozifanya.

Wachina hawakusubiri au kwenda kujitembeza kutafuta wawekezaji. Wawekezaji walipigana vikumbo wenyewe kwenda China walikuoona kuna kazi na na mazingira mazuri yaliyowahusu wananchi wa huko.

Hawa viongozi wana tabia za kitwana sana, na wanaifanya nchi hii iwe kama ya watwana.
Eti Kilimo kibadilishwe na kundi la vijana mia nane tu ambao hawana hata background ya kilimo.

Kesho siyo mbali itatupa majibu ya kusikitisha.
 
Jana tarehe 20 March 2023, Rais alifungua mradi wa mashamba ya pamoja, Mradi wa Kilimo wa Vijana. Sijui kama Waziri ana lengo zuri au ni kulifanya jina lake lisikike kila wakati mbele ya Rais kwa kujitambulisha kama mchapakazi. Kama ni mpango wa Wizara, basi ni muendelezo wa udanganyifu ulioanzia mambo ya Kilimo kwanza.

Wakulima wa nchi hii, zaidi ya 70%, wako vijijini. Huu ni upigaji wa wazi kabisa kuwashawishi vijana kwa kuwapa mashamba kama kambi ya JKT, ili washawishi wengine kuhusu kilimo. Hii ni hasara kwa wakulima. Waziri alianza na pikipiki za maafisa ugani ambazo hazionekani zilikwenda wapi na bado hazijaulizwa! Sasa amekuja na hili ambalo halimo hata kwenye mpango mkakati wa pili wa kuendeleza kilimo wa Wizara, ASDP II.

Huu ni upigaji wa wazi kabisa!
Sikia wataalamu wa Bashe kwenye kuandaa BBT project!
 
Sikia wataalamu wa Bashe kwenye kuandaa BBT project!View attachment 2563647
D4E26826-F10A-41B1-8412-F9612536D869.jpeg


Mwangalie huyo dada mwenye t-shirt ya njano, wapembeni yake mwenye kilemba na dada mwingine nae kavaa kilemba cha njano upande wa pili na miwani.

Kwa muonekano wao tu hao ni watu wakulima shamba la hector 10 peke yao. Sampuli hiyo imejaa kibao, yupo mmoja nimemuona kwenye video wakati wanawasili kwenye mafunzo ata kuburuza begi lake mwenyewe aliloenda nalo kasheshe ndio akalime heka 10.
 
View attachment 2563662

Mwangalie huyo dada mwenye t-shirt ya njano, wapembeni yake mwenye kilemba na dada mwingine nae kavaa kilemba cha njano upande wa pili na miwani.

Kwa muonekano wao tu hao ni watu wakulima shamba la hector 10 peke yao. Sampuli hiyo imejaa kibao, yupo mmoja nimemuona kwenye video wakati wanawasili kwenye mafunzo ata kuburuza begi lake mwenyewe aliloenda nalo kasheshe ndio akalime heka 10.
'Mayor', unaweza kuua bila kukusudia. Nimecheka sana hadi machozi yakanitoka.

Hapana. Tunaweza kusema kwamba hawa ni ma-'agents' tu wenye kazi zao wapo mafichoni. Kwa hiyo kazi inaweza kuendelea kwa baadhi yao vizuri kiasi.
 
Bajeti ya wizara ya kilimo alisema imeongezwa Mara 3 ya mwanzo hadi kufikia bil 750, hebu sema nini kimebadilika hadi sasa?
Kwa uhakika kabisa naamini Rais anajua uchizi anaofanya Bashe, tatizo tunaendesha nchi kwa ushirika na urafiki. Huwezi kuruhusu Bashe aendeshe Wizara kwa ubinifu ambao haujapitishwa kitaifa, halafu unaancha taarifa rasmi ya kitaifa inayoeleza jinsi ya kuinua kilimo nchini. Halafu anatum,ia pesa kununua pikipiki na magari bila hata faida ya maana.

Bashe hajui chochote ktk kilimo, ina maana anategemea wataalamu wa Wizara. Mtaalamu gani ktk wizara atashauri mbinu za aina hii wakati anafahamu kulikuwa na ASDP I na sasa ni ASDP II.
 
Serikali iache blah blah ,kwanini wasiandae mashamba + mfumo wa kuwajengea kilimo cha umwagiliaji(irrigation schemes)kwa kila vijiji
Na huko wawepo mabwana shamba

Ova
 
Serikali iache blah blah ,kwanini wasiandae mashamba + mfumo wa kuwajengea kilimo cha umwagiliaji(irrigation schemes)kwa kila vijiji
Na huko wawepo mabwana shamba

Ova
Hilo pekee lingeleta transformation kubwa sana kwenye kilimo.

Siyo hizi blah blah za Bashe
 
Mie niliposikia eti katika kila eneo akitolea mfano wa shamba la hector 30000.

Vijana wanachukua labda hector 10000. Halafu mwekezaji mkubwa anapewa hector 20000.

Condition ya mwekezaji mkubwa ni lazima kununua mavuno yatakayopatikana kwenye hizo hekari 10000 za vijana.

Halafu maeneo mengine wamepanga kulima zabibu; sasa unless huyo mkulima mkubwa na yeye ana biashara nyingine ya kutengeneza juice ya zabibu au wine sioni mantiki ya yeye kutaka kununua zabibu zote hizo.

Kumbuka zabibu ni perishable good inayotakiwa kutumika haraka baada ya mavuno. Kwa ivyo zisipo nunuliwa in time zinaharibika.

Kawaida wenye uwezo huo huwa ni makampuni, mfano ‘Starbucks’ hiyo ni sehemu ya operation strategy yao duniani ata kama sio kwa jina lao directly wanaweza kuwa na wakala anaelima ‘Coffee Arabica’ na kuwa na uwezo wa kununua kiasi kikubwa kwa wakulima wadogo wa maeneo hayo. Huyo wakala anajukumu la kuwasaidia mbinu za kupata mavuno mazuri wakulima wadogo.

Kama ilivyo Mfindi kwa wakulima wa chai na Unilever, Babati na TBL kwa wakulima wa burley, Cadbury Chocolate na cocoa ya Ghana; etc. Mara nyingi ukiona hivyo elewa kuna conglomerates nyuma ya hiko kilimo.

Lakini mkulima ambae hana soko maalum kubwa kumtwika huo mzigo ni wazimu halafu mazao yenyewe sio nafaka ambayo watanzania wanahitaji.

Nimewahi kusikia mipango mingi ya ovyo Tanzania lakini huu, I am sorry to say kwa atakae kwazika nitakachoandika tuna watu wajinga mno serikalini how on earth watu walioenda shule waliweza pitisha mradi kama huu wenye kasoro zaidi ya 700 ambazo ata kuziongelea zinaleta uvivu ni waste of money aijwahi tokea Tanzania.

Huyo Bashe wamtoe hapo Kilimo na kumtafutia wizara nyingine.
Nchi zetu hizi viongozi hawapangi mambo kwa manufaa ya taifa au wananchi. Kila waziri anahakikisha anafaidika na wizara aliyopo, hata kama akiondolewa anakua amefaidika yeye binafsi. Ni wengi wa aina ya Bashe. Hata ujenzi wa kiwanja cha ndege Msalato waziri anaendesha biashara zake za kokoto.

Anayefahamu kilimo hawezi kubuni uhuni wa aina hii. Hii ni nchi ambayo tunaambiwa tatizo kubwa ni ukame na ufumbuzi ni umwagiliaji ktk maeneo ambayo wizara inayajua kwa miaka 60 iliyopita. Sasa waziri anaacha mipango yote inayoeleweka!

Aibu ni kwamba Rais yupo anaangalia tu! Wabunge nawalaumu kwa kutoliona tatizo la waziri, lakini siwalaumu kwa kutokataa maana hakuna mpango wa serikali ambao umewahi kukataliwa bungeni. Spika huhakikisha yote yanapita, kila semacho waziri ni jawabu hata matusi ya mawaziri kama Mwigulu yanavumiliwa.
 
Back
Top Bottom