Waziri Bashe: Tutailazimisha Benki Kuu kuipa upendeleo Benki ya Ushirika

Waziri Bashe: Tutailazimisha Benki Kuu kuipa upendeleo Benki ya Ushirika

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema hawataiomba Benki Kuu ya Tanzania bali watailazimisha kutengeneza mfumo utakaowezesha Benki ya Ushirika kupata upendeleo wa kurahisisha utoaji wa mikopo kwa wakulima



Pia soma Waziri Bashe aipaka matope Tanzania Kimataifa

Bashe kwa asili ni lobbyist, kwahiyo jitahidi tu kumuelewa. Kuna maana nyingi sana za neno "kulazimisha" ikiwemo kumuacha mtu hana option nyingine zaidi ya ile uliyoileta wewe katika meza ya mazungumzo.
Nadhani hiyo ndio anayoimaanisha waziri Bashe.

Tukiweka pembeni mihemko, unazi, mazoea mabaya na uzamani, tutakubaliana kwamba huyu jamaa anao uthubutu wa kuyabadili yale yanayoonekana kuwa kikwazo katika kilimo.
Bashe atatusaidia.
Tumpe muda (hata kama hatumpendi sana).
 
Benki kuu Haina hela zake utailazimishaje?

Hela zilizoko Kule ni za mabenki ya biashara ambayo ndio yenye akaunti pale na huwekwa pesa zao pale

Pesa zingine zilizopo pale ni za akaunti za Serikali na wizara zake ikiwemo wizara yake ya kilimo.

Wenye mamlaka na hizo pesa zilizoko benki kuu ni wateja wenye akaunti zao yaani mabenki ya biashara na Wizara zenye akaunti zao

Sasa Bashe anaposema atalaximsha benki kuu kivipi labda ?
 
Benki Kuu ya Tanzania imekuwa ikifanya mabadiliko mengi ya kisera na kimfumo bila shinikizo kutoka chombo au mtu yoyote kwa kuzingatia mabadiliko ya kiuchumi na matokeo ya tafiti mbalimbali, BOT imejipatia umaarufu mkubwa kimataifa na kupewa tuzo mbalimbali kutoka taasisi zinazoaminika duniani. Iweje leo inaenda kulazimishwa na kushinikizwa kutoa upendeleo katika mfumo wa utoaji wa mkopo wa benki ya ushirika pekee? Bashe achunguzwe anaweza kusababisha matatizo makubwa
 
Bashe kwa asili ni lobbyist, kwahiyo jitahidi tu kumuelewa. Kuna maana nyingi sana za neno "kulazimisha" ikiwemo kumuacha mtu hana option nyingine zaidi ya ile uliyoileta wewe katika meza ya mazungumzo.
Nadhani hiyo ndio anayoimaanisha waziri Bashe.

Tukiweka pembeni mihemko, unazi, mazoea mabaya na uzamani, tutakubaliana kwamba huyu jamaa anao uthubutu wa kuyabadili yale yanayoonekana kuwa kikwazo katika kilimo.
Bashe atatusaidia.
Tumpe muda (hata kama hatumpendi sana).
Akitaka afanye hela za Korosho, hela za sulphur,stakabadhi ghalani,all agri rerated money, saccos zipitie hiyo benk hapo sawa, lakini tayari NMB,CRDB wana mikataba na hiyohiyo wizara anayoiongoza😁
 
Waziri wa Kilimo anahusikaje na utendaji kazi wa Benki Kuu. Bashe apunguze kuongea, kila kukicha anaonesha udhaifu.
Hili tatizo linahusu zaidi sisi Waafrika ni kwamba ukishaambiwa ni kiongozi mara unajitia ufahamu kichwani kuwa wewe una akili, hekima na busara katika kila jambo kuliko kila mtu unayemwongoza au ambaye hana cheo juu yako! Kwa maneno mengine ni kutokujua maana ya uongozi kwa sababu ya ama shule nyembamba, uzoefu finyu au kiburi. Ukitazama historia, utakuta watu hawa wanazidiwa hata na Ma chifu wa jadi au Sultani ambao walikuwa na jopo la washauri ambao waliwasaidia kuziba mapengo ya uwezo wao.Uzuri, hawa watu mwishowe huwa wanagundua tatizo lao lakini wanakuwa wamekwisha kosa fursa ya uongozi wakati huo. Nitatoa mifano hivi karibuni.

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
Yaani badala ya kutunga sera zitakazratibu benki za ushirika (sio hii tu iliyopo sasa) wao wanayaka kutumia mabavu. Je zikitokea kesho benki tatu za namna hii kimuundo na kiutendaji, nazo zitapata faida ya lazimisho la waziri ambaye mwaka mmoja baadae anaweza kuwa hayuko tena???

Huenda mambo mengi yanaendeshwa kimabavu mamna hii. CAG anajua anachoona!!!
 
Bashe kwa asili ni lobbyist, kwahiyo jitahidi tu kumuelewa. Kuna maana nyingi sana za neno "kulazimisha" ikiwemo kumuacha mtu hana option nyingine zaidi ya ile uliyoileta wewe katika meza ya mazungumzo.
Nadhani hiyo ndio anayoimaanisha waziri Bashe.

Tukiweka pembeni mihemko, unazi, mazoea mabaya na uzamani, tutakubaliana kwamba huyu jamaa anao uthubutu wa kuyabadili yale yanayoonekana kuwa kikwazo katika kilimo.
Bashe atatusaidia.
Tumpe muda (hata kama hatumpendi sana).
Amesaidia nini cha maana zaidi ya kubwabwaja tu. Hi staili ya kelele nyingi na ubabe wa kishamba ilishafeli toka awamu ya 5. Hata yeye ni suala la mda tu!
 
Hili tatizo linahusu zaidi sisi Waafrika ni kwamba ukishaambiwa ni kiongozi mara unajitia ufahamu kichwani kuwa wewe una akili, hekima na busara katika kila jambo kuliko kila mtu unayemwongoza au ambaye hana cheo juu yako! Kwa maneno mengine ni kutokujua maana ya uongozi kwa sababu ya ama shule nyembamba, uzoefu finyu au kiburi. Ukitazama historia, utakuta watu hawa wanazidiwa hata na Ma chifu wa jadi au Sultani ambao walikuwa na jopo la washauri ambao waliwasaidia kuziba mapengo ya uwezo wao.Uzuri, hawa watu mwishowe huwa wanagundua tatizo lao lakini wanakuwa wamekwisha kosa fursa ya uongozi wakati huo. Nitatoa mifano hivi karibuni.

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
Well spoken mkuu. Bashe ujuaji mwingi mpaka anazidisha chumvi.
 
Back
Top Bottom