Waziri Bashe: Tutailazimisha Benki Kuu kuipa upendeleo Benki ya Ushirika

Kama hicho ndicho unajua kuhusu benki kuu..pole kwa kuchelewa, weka bidii ipo siku utafahamu zaid ya hapo.
 
Taja hayo mabadiliko ya kisera na matokeo yake kwa watz, sababu wao ndiyo wanawalipa mishahara benki kuu na sio hao unaosema wamewapa tuzo..taja hizo tafiti walizofanya zinazoonyesha kiwango cha ujuzi wao na maarifa ku-manage uchumi wa nchi..na matokeo yake kwa jamii ya watz.
 
Kuanzishwa bank ya ushirika ni wazo zuri sana.
Ila chanzo cha mtaji wake ni kipi?

Mpaka sana kuna bank ya uwekezaji na bank ya maendeleo ya kilimo zikiwa na mitaji kidogo sana.

Wakiweza kutafuta dhamana ya BOT bank hii mpya ikawepo kila mkoa na ikiwezekana kila wilaya hasa kwenye mazao ya kimkakati, na uhusike pia kwenye kukopesha fedha kununua technology ili kukuza uzalishaji na kuchakata mavuno hii sio tu itakuwa mkombozi wa wakulima, bali itasisimua sana uchumi wa nchi hii.

Ila wasaka Urais huko mbele wakijua hii initiative itamwinua Bashe kisiasa, kuna namna watampigisha shoti.
 
Swala sio matawi ya benki kuwa kila mkoa na kila wilaya!! Tanzania wenye pesa hawataki kulima wanataka kufanya biashara zingine za mijini hata mabilionea kama Bakhresa wanataka tu kuwa wachuuzi wanunue tu nafaka wasage wauze

Vijijini wengi hawana mpango wa kulima mashamba makubwa yaani estates wameridhika na kilimo chao kidogo
Solution ni kuleta wawekezaji
 
Ame benchmark wapi? Au ndiyo ana invert a new wheel?
 
Huyu kama hajuwi Taifa hili lina deep state mwache ajiachie tu akifikiri Rais atampigia makofi.. watu wanamuangalia tu na agender zake za siri zenye sura ya uzalendo.
 
Ame benchmark wapi? Au ndiyo ana invert a new wheel?
Kwani ni lini amepata platform kama hii aliyonayo sasa na hata tumhukumu kwa utendaji wake huko ?

Mimi ninadhani tupunguze kumzonga "bila sababu za msingi" na tumwache afanye kazi ili tumpime kwa matokeo.

Bila kuathiri haki ya mtu yeyote yule anayeuona mwanzo mbaya wa waziri, mimi ninauona mwanzo mwema sana kwa waziri huyu juu ya sekta ya kilimo.

Kwa mnaouona mwanzo mbaya, basi angalau leteni sababu zenye mashiko pengine mtufumbue macho na sisi.

Hizi shutuma za jumla jumla, (anajifanya mjuaji, anaongea sana, yule msomali, pamoja na blah blah zingine) zinaweza zisilete picha nzuri ya kile ambacho mnaweza kuwa mnakisimamia juu ya mwenendo na utendaji wa waziri Bashe.

NB: Ideally, kwa mujibu wa maoni randomly ya sisi watanzania, kila kiongozi ni "kiongozi mbaya".
 
Mambo ya kitaalamu hayafanywi kazi kama mchezo wa bahati na sibu au kwa kubahatisha, yana mifumo yake iliyo fanyiwa tafiti na kujaribiwa. BoT kama wataalamu waachwe wafanye kazi yao bila shinikizo. Tuache siasa kwenye mambo ya kitaalamu. Tujifunze kwenye issue ya Covid 19 wakati wa awamu ya 5.
 
Kwa ufahamu wangu, sekta ya kilimo hapa nchini, pamoja na matatizo yake meengi mengine, sekta hii pia iko "inadequately financed".
Hivyo basi, jitihada zozote zile za kukitafutia fedha kilimo, kwangu mimi jitihada hizo ni njema.

Yeye Bashe kama mtu anayesimamia sekta hii, anapofurukuta kutafutia mianya ya ku inject hela kwenye kilimo, mimi ninamuelewa. (Hata kama anatumia njia ambazo pengine hazijazoeleka sana).

Sina mashaka kabisa na utaalam wa mambo ya fedha na masuala ya uchumi wa watu wa BOT, lakini tusifunge milango kwa any possible suggestions (hata kama zinaweza ku sound unusual) kwa kivuli cha kwamba "eti" wao watu wa BOT ni wataalam.

Mtazamo wangu ni huo, sijaona kama waziri amejaribu "kuwapanda kichwani" BOT au ameleta "ukilimo" kwenye mambo ya fedha.

NB: Sekta ya kilimo kwa muda mrefu ilitawaliwa na "uzamani pamoja mazoea", angalau naziona jitihada za viongozi wa sasa (kwa ngazi ya wizara), kuki commercialise na kukipa usasa kilimo. Pengine jitihada zao hizo zinanipofusha kuona makosa makubwa (terrible mistakes) ambayo Waziri Bashe anayafanya, kama mnavyoyaona wenzangu.
 
comrade bado wapo wanaotaka kulima au kunenepesha wanyama ili kuongeza thamani.

Credit facility kwa uwekezaji wa kilimo-biashara bado ni deal, ndio maana kuna washua wamekuja toka walikotoka na kupewa heka laki moja.

So far, ni aibu ku-import maziwa toka Oman au Netherlands.

Oman iko jangwani, Netherlands ni kama ka-wilaya nchini.

Ila kupanga ni kuchagua, walau JPM alimhamisha Bakhresa awekeze kwenye kuzalisha sukari na akampatia shamba ili alime miwa na kuzalisha sukari pia.

Nchi inapojipambanua kuwa uti wa mgongo ni kilimo, kilicho cha sasa chahitaji uwekezaji, uwekezaji bila banking facility kwenye level ya wilaya, tunakuwa tunachechemea huku wenzetu wanapaa
 
Nyerere aliwahi sema.kuwa ili kilimo na ufugaji kibadilike ni pale wasomi watakapojitosa kwenye.kilimo.na ufugaji

Kwenye kufunga kuku Walau wasomi wameingia japo ni kwa small scale ya banda la.kuku

Kilimo wasomi bado kujitosa

Kuinua kilimo ni pamoja na kubadilisha mindset za wasomi wajitose huko
 
Professionalism should prevail. Kama ni fedha kwaajili ya mikopo ziwe solicited kwa namna nyingine siyo kwa mashinikizo au kwa upendeleo
 
Seasoned Agriculture Engineer,Chief Agriculture Economist,Financial Expert and The Knowledgeable Mtukufu Hussein Bashe🤣🤣
 
Huyu jamaa his first appointment alikuwa Banker baadaye akaenda Mwananchi Communication hatimaye ndio kaingia kwenye Politics
Ni lobbyist mzuri sana, siasa ameanza tangu akiwa chuoni pale Mzumbe
Nadhani badala ya kuongeza misururu ya Benki wangeangalia jinsi ya kuiongezea nguvu TADB Bank ika merge na hiyo bank ya Ushirika
 

Hata hivyo, lazima abaki kwenye lane yake; vinginevyo atasababisha ajali mbaya!
 
Wewe ni Bashe?!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…