Waziri Jafo apendekeza Stendi mpya ya Mbezi ipewe jina la Dkt. John Magufuli

Waziri Jafo apendekeza Stendi mpya ya Mbezi ipewe jina la Dkt. John Magufuli

Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo, amesema kutokana na stendi mpya ya mabasi ya Mbezi Luis kuwa na hadhi ya kimataifa, anapendekeza ipewe jina la Dkt. John Magufuli kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitihada alizofanya, ambapo amesema atamuomba Rais aridhie ombi hilo.

Stendi za mabasi ni alama ya miji husika ndio maana hazipewi majina ya viongozi.

Napendekeza amuombe ule uwanja wa ndege ndio upewe jina lake.

Tangu tupate uhuru hakuna na wala sijaskia stendi ya basi kupewa majina ya viongozi.

Tunafahamu nia ya kila mteule kumfurahisha mkubwa,ikianza utaratibu huu, utashangaa hata Wakuu wa Mikoa na Wilaya wataiga kubadilisha majina ya stendi za mabasi zilizo katika maeneo yao!
Ombi kwako Waziri achana na pendeķezo hili, mkubwa alishasema msubiri akishastaafu ndio mpe upendeleo sio sasa.
 
Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo, amesema kutokana na stendi mpya ya mabasi ya Mbezi Luis kuwa na hadhi ya kimataifa, anapendekeza ipewe jina la Dkt. John Magufuli kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitihada alizofanya, ambapo amesema atamuomba Rais aridhie ombi hilo.

😬😬😬
 
Pale Mpanda kuna mizengo pinda bus stand
Itakuwa "Isolated case", nitakupa mfano kuanzia Arusha mpaka Dar es Salaam

(i) Stand ya Mkoa Arusha
(ii) Stand ya Tengeru ( Wilaya ya Arumeru)
(iii) Stand ya Boma (Wilaya ya Hai)
(iv) Stand ya Moshi (Mkoa wa Kilimanjaro)
(v) Stand ya Njia Panda (Vunjo)
(vi) Stand ya Mwanga (wilaya)
(vii) Stand ya Same (wilaya)
(viii) Stand ya Mombo
(ix) Stand ya Korogwe
(xi) Njia panda ya Korogwe
(xii) Stand ya mkoa wa Dar es Salaam.

Kuanzia Arusha mpaka Dar es Salaam stand zote zinaakisi majina ya sehemu stand iliko
 
Itakuwa "Isolated case", nitakupa mfano kuanzia Arusha mpaka Dar es Salaam

(i) Stand ya Mkoa Arusha
(ii) Stand ya Tengeru ( Wilaya ya Arumeru)
(iii) Stand ya Boma (Wilaya ya Hai)
(iv) Stand ya Moshi (Mkoa wa Kilimanjaro)
(v) Stand ya Njia Panda (Vunjo)
(vi) Stand ya Mwanga (wilaya)
(vii) Stand ya Same (wilaya)
(viii) Stand ya Mombo
(ix) Stand ya Korogwe
(xi) Njia panda ya Korogwe
(xii) Stand ya mkoa wa Dar es Salaam.

Kuanzia Arusha mpaka Dar es Salaam stand zote zinaakisi majina ya sehemu stand iliko
Lakin Mpanda kuna mizengo pinda stand
 
Stendi za mabasi ni alama ya miji husika ndio maana hazipewi majina ya viongozi.

Napendekeza amuombe ule uwanja wa ndege ndio upewe jina lake.

Tangu tupate uhuru hakuna na wala sijaskia stendi ya basi kupewa majina ya viongozi.

Tunafahamu nia ya kila mteule kumfurahisha mkubwa,ikianza utaratibu huu, utashangaa hata Wakuu wa Mikoa na Wilaya wataiga kubadilisha majina ya stendi za mabasi zilizo katika maeneo yao!
Ombi kwako Waziri achana na pendeķezo hili, mkubwa alishasema msubiri akishastaafu ndio mpe upendeleo sio sasa.
Assume kibao cha gari kinasomeka Dodoma to Magufuli
 
Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo, amesema kutokana na stendi mpya ya mabasi ya Mbezi Luis kuwa na hadhi ya kimataifa, anapendekeza ipewe jina la Dkt. John Magufuli kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitihada alizofanya, ambapo amesema atamuomba Rais aridhie ombi hilo.


============

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo ameelekeza Uongozi wa Mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha Stendi Mpya ya Mabasi ya Mbezi Luis inaanza kutumika muda wowote kuanzia sasa baada ya kujiridhisha kukamilika kwa miundombinu yote muhimu kasoro Barabara ya kuingia kituoni hapo ambayo ipo hatua ya mwisho.

Waziri Jaffo amesema hayo wakati alipofanya ziara Katika Stendi hiyo ambapo amesema muda wowote ambao TANROAD watathibitisha kuwa Barabara ya kuingia kituoni hapo imekamilika ni vyema kituo kikaanza kutoa huduma.

Aidha Waziri Jaffo amesema Kutokana na Stendi hiyo kuwa na hadhi ya kimataifa anapendekeza ipewe jina la Rais Dkt. John Magufuli Kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitiada alizofanya ambapo amesema atamuomba Mhe. Rais aridhie ombi hilo.

Hata hivyo Waziri Jaffo amemuelekeza Mkandarasi anaejenga eneo la maegesho ya magari madogo kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya wiki mbili kuanzia leo huku akitaka taa zifungwe ndani ya wiki moja kuanzia leo.

Pamoja na hayo Waziri Jaffo ametoa pongezi kwa uongozi wa Mkoa wa Dar es salaam kwa usimamizi madhubuti uliosaidia Stendi hiyo kukamilika ikiwa na ubora uliokusudiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam Bi.Spora Liana amesema kazi zinazoendelea kwa Sasa ni Ufungaji wa Viyoyozi, Lifti, ufungaji wa taa na Vifaa vya matangazo, uunganishwaji wa maji kwenye Vyoo na miundombinu mingine ambayo nayo ipo hatua ya mwisho kukamilika na kusisitiza kuwa kwa Sasa Stendi inaweza kuanza kutumika.
Swaziland ilibadilishwa jina ikaitwa Eswatini. Kwanini Tanzania isiwe Magufulini?
 
maaana kabla yake tulikuwa hata hatuvuti hewa lakini toka kuingia yeye madarakani tunavuta oxygen kwa wingi, mvua zimeongezeka na hata ardhi imekuwa na rutba zaidi.
😀😀😀😀😀 'Mimi ndimi bwana Mungu wako. Usiabudu miungu wengine.'
 
Ombi kwako Waziri achana na pendeķezo hili, mkubwa alishasema msubiri akishastaafu ndio mpe upendeleo sio sasa.
Akishastaafu itawezekana kweli? El bashir, Yahaya Jameh, Trump, B. Compaore etc walipostaafu sijasikia maeneo ktk nchi zao yalipewa majina yao.
 
Uwanja wa Ndege Chato ndiyo uitwe Magufuli International Airport - MIA
 
Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo, amesema kutokana na stendi mpya ya mabasi ya Mbezi Luis kuwa na hadhi ya kimataifa, anapendekeza ipewe jina la Dkt. John Magufuli kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitihada alizofanya, ambapo amesema atamuomba Rais aridhie ombi hilo.


============

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo ameelekeza Uongozi wa Mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha Stendi Mpya ya Mabasi ya Mbezi Luis inaanza kutumika muda wowote kuanzia sasa baada ya kujiridhisha kukamilika kwa miundombinu yote muhimu kasoro Barabara ya kuingia kituoni hapo ambayo ipo hatua ya mwisho.

Waziri Jaffo amesema hayo wakati alipofanya ziara Katika Stendi hiyo ambapo amesema muda wowote ambao TANROAD watathibitisha kuwa Barabara ya kuingia kituoni hapo imekamilika ni vyema kituo kikaanza kutoa huduma.

Aidha Waziri Jaffo amesema Kutokana na Stendi hiyo kuwa na hadhi ya kimataifa anapendekeza ipewe jina la Rais Dkt. John Magufuli Kama sehemu ya shukrani na kuthamini jitiada alizofanya ambapo amesema atamuomba Mhe. Rais aridhie ombi hilo.

Hata hivyo Waziri Jaffo amemuelekeza Mkandarasi anaejenga eneo la maegesho ya magari madogo kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya wiki mbili kuanzia leo huku akitaka taa zifungwe ndani ya wiki moja kuanzia leo.

Pamoja na hayo Waziri Jaffo ametoa pongezi kwa uongozi wa Mkoa wa Dar es salaam kwa usimamizi madhubuti uliosaidia Stendi hiyo kukamilika ikiwa na ubora uliokusudiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam Bi.Spora Liana amesema kazi zinazoendelea kwa Sasa ni Ufungaji wa Viyoyozi, Lifti, ufungaji wa taa na Vifaa vya matangazo, uunganishwaji wa maji kwenye Vyoo na miundombinu mingine ambayo nayo ipo hatua ya mwisho kukamilika na kusisitiza kuwa kwa Sasa Stendi inaweza kuanza kutumika.
Mimi napendekeza waiite Samial Suluhu Hassan. JPM wanamlundikia vingi mno mwishowe atakakuwa anavikataa halafu matokeo yake watavipa majina hata yasiyostahili. JPM yuko na Majaliwa na Samia, why many things be in his name? Mimi ningefurahi sana safari hii kama stand hiyo wataiita Samia iwe kumbukumbu kwa vizazi vyote kwamba huyu mama aliwah kuwa Makamu wa kwanza wa Rais mwanamke, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 
Halafu Kuna pimbi mmoja anaotea eti jafo awe rais wa tz 2025. Ujinga wa hali ya juu sana
 
Kwani ikiitwa Mbezi Bus Terminal kama ilivyo kwa Ubungo Bus Terminal kuna nongwa gani?

Tupunguze kuendekeza mambo ya kijinga.
 
Back
Top Bottom