Waziri Jafo asema atabandika majina hata ya wale waliojitoa na kura zitapigwa

kijan kadata kwamba ni wagombea huru hao hadi wabaki kwenye mchakato hahahahaha!

jamaa nilikuwa namkubali sana ila kwa hili hahahahaha eti wagombea hawajajitoa
 

Hoja nyingine ya nguvu!
 
Mtu anasema nimejitoa, sitaki, wewe unasema nitakuweka kwa nguvu! Jafo, hivi unakosa kitu gani/unapata hasara gani/ipi mtu akijitoa?
Aliyejitoa ni nani?
Waliogombea ndiyo waliokata rufaa!
Waliojitoa ni viongozi wa vyama ambao siyo wagombea!
 
Hujui unaliliongea.
 
Awamu hii kilakitu nimanguvu tu
 
Siku ya kwanza Chadema walipojitoa waziri alionyesha kuguswa na kulalamika kuwa hata wagombea wa upinzani waliopitishwa watakuwa wamepoteza nafasi ya kugombea. Leo baada ya kupata "tuitio" amerudi na ujasiri kuzuia kujitoa!. Tanzania ya Nyerere imekuwa hivi! Incredible.
 
Kwahiyo kwa tamko lake siku hizi ugombea huru bila chama unaruhusiwa sio?
 
Japo nadhani ameanza kuondokewa na akili. Anayegombea amesema amejiondoa, wewe unasema, lazima uwemo. Hivi wewe unayesema hivyo utakuwa mzima?

Uzima unatoka wapi hapo! Hiyo ni akili ya mwendawazimu 100%.
 
Chama ndo mdhamini wa mgombea, sasa kama mdhamini kagoma unampitishaje mgombea bila ya kuwa na mdhamini?
 
Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo amesema vyama vya siasa ndivyo vimejitoa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa sio wagombea, na kwamba wagombea wa vyama vilivyojitoa waliokata rufaa, matokeo ya rufaa yakitoka na wakishinda, majina yao yatajumuishwa kwenye karatasi za uchaguzi..

Hoja:

Ivi mtu akienguliwa na chama huwa anabaki kuwa mwanachama? Na mtu akivuliwa uanachama na ni diwani au mbunge huwa anabaki na cheo chake? Hii sheria imetungwa lini?

Kwanini wanalazimisha ushiriki kwanini hawafurahi wapinzani kuwaachia waendelee kushinda bila lupingwa
 
Mtu anasema nimejitoa, sitaki, wewe unasema nitakuweka kwa nguvu! Jafo, hivi unakosa kitu gani/unapata hasara gani/ipi mtu akijitoa?
Wamepagawishwa na sasa wanaweweseka...
Sitoona ajabu baadhi ya maeneo wakiwashindisha MARUHANI!!!
 

Hapa technicalities ndizo zinazo waangusha wapinzani. Kama wagombea hawaja jitoa rasmi kwa utaratibu uliopo basi ni washiriki halali wa uchaguzi.
 
Hapa technicalities ndizo zinazo waangusha wapinzani. Kama wagombea hawaja jitoa rasmi kwa utaratibu uliopo basi ni washiriki halali wa uchaguzi.
akili zile zile za Lumumba! zile zile! Hatuna mgombea binafsi, chama ndiyo kinasimamisha mgombea., kikijitoa basi kila kitu kina collapse!
 
'Confused government'.....eti huyu Jafo ndo wanasema ni presidential material duh ameshindwa kumdhibiti Magufuri kwa hilo, sasa anae aibika niyeye.....
 
Nadhani kuna conflict of interest kwa upande wa waziri Jafo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…