Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300

Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300

Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Jerry Silaa, ametangaza kusitisha matumizi ya kituo cha mafuta cha Barrel kilichopo Mikocheni, mkoani Dar es Salaam akidai kuwa kituo hicho kujengwa bila kufuata utaratibu wa Wizara hiyo.

Waziri huyo amesema hayo alipotembelea eneo hilo, kilipojengwa kituo hicho, ambapo amebainisha kuwa, kuna watu walimfuata wakitaka kumpa rushwa ya Tsh.Mil. 300 ambazo amedai kuwa amezikataa na kubakia kusimamia ukweli katika sakata hilo.

Waziri huyo pia amewaagiza Wakuu wa Idara wa Ardhi na Mipango Miji nchi nzima kufanya uhakiki wa vituo vya mafuta vilivyo kwenye maeneo yao, kwa kuangalia matumizi yake pamoja na mchakato uliotumika kupatikana kwa viwanja hivyo.

Kituo hicho kilichopo mikocheni kiliwaibua wananchi wanaolizunguka eneo hilo kuwa kimejengwa eneo la makazi ambalo ni hatarishi kwa usalama, kati ya wakazi waliopinga uwepo wa kituo hicho eneo hilo ni Prof. Anna Tibaijuka.View attachment 2852361View attachment 2852362
Huyu rais ana kazi gani? Aliyetoa rushwa hàtajwi, aliyepewa akaikataa ni waziri Jerry Slaa. Nchi ngumu sana hii.
 
Walifikia hadi kubagein bei?, possibly alihitaji nyingi ya hizo wakachomoa ndiyo akaja kutafuta kiki
 
Nimepita mitandaoni baada ya kuwa nje ya mitandao kwa miezi kadhaa. Katika pitapita zangu nakutana na habari ya Slaa kukataa rushwa ya mil 300.
Hivi huyu jamaa ukimcheki hata kwa mbali anaweza kuchomoa hata mil 20 kweli ?
Ebu fikiria safari ya Dubai , bandari na ,Slaa na DP world?
 
Alitaka nyingi zaidi
Let us say, Thamani ya kituo ni Tsh 800 ml+ Ardhi, lakini je ni kweli Unaweza Risk Tsh 300ml kama rushwa Kwa kituo 1 tu Cha mafuta?

Haya Cha pili,Kwa Slaa, umeletewa Rushwa umekataa je hatua gani uliochukua Kwa watoa rushwa ? Umeenda Takukuru? Au huyu Slaa anatafuta Publicity/ populism,

Walio soma Cuba hawawezi kumuamini huyu Slaa, Kutuoa/kusawishi , Rushwa ni kosa ningemuamini Slaa angetamka hadharani wahusika na kuwapeleka Takukuru,nje ya hapo ni Publicity inatafutwa
 
Let us say, Thamani ya kituo ni Tsh 800 ml+ Ardhi, lakini je ni kweli Unaweza Risk Tsh 300ml kama rushwa Kwa kituo 1 tu Cha mafuta?

Haya Cha pili,Kwa Slaa, umeletewa Rushwa umekataa je hatua gani uliochukua Kwa watia rushwa ? Umeenda Takukuru? Au huyu Slaa anatafutwa Publicity/ populism,

Walio soma Cuba hawezi kumuamini huyu Slaa, Kutomba/kusawishi kutoa Rushwa ni kosa ningemuamini Slaa angetamka hadharani wahusika na kuwapeleka Takukuru,nje ya hapo ni Publicity inatafutwa
Kutomba = kuomba
 
Waziri wa Ardhi, William Lukuvi amesema rushwa imekithiri kwenye sekta ya ardhi kiasi kwamba wafanyabiashara wawili walimuahidi rushwa ya Sh5 bilioni afanikishe mpango wao wa kuiuzia Serikali ardhi kwenye eneo linalotakiwa kujengwa mji wa kisasa wa Kigamboni.

Kuwa makini ni Wanasiasa, they're hypocrisy, Huwezi ukaja na tuhuma nzito kama hizo bila kuchukua hatua,ni Bora wangekuwa wanakaa kimya,but remind you, huo ni mchezo ni mtaji wa kisiasa Kwamba wawo ni waadirifu hakuna jipya.
 
Let us say, Thamani ya kituo ni Tsh 800 ml+ Ardhi, lakini je ni kweli Unaweza Risk Tsh 300ml kama rushwa Kwa kituo 1 tu Cha mafuta?

Haya Cha pili,Kwa Slaa, umeletewa Rushwa umekataa je hatua gani uliochukua Kwa watoa rushwa ? Umeenda Takukuru? Au huyu Slaa anatafuta Publicity/ populism,

Walio soma Cuba hawawezi kumuamini huyu Slaa, Kutuoa/kusawishi , Rushwa ni kosa ningemuamini Slaa angetamka hadharani wahusika na kuwapeleka Takukuru,nje ya hapo ni Publicity inatafutwa
Imeisha hiyo
 
Back
Top Bottom