Waziri Kabudi akanusha kuthibitisha kifo cha Mwanahabari, Azory Gwanda

Waziri Kabudi akanusha kuthibitisha kifo cha Mwanahabari, Azory Gwanda

prof. hakukosea kabisa ila tumewazoea mkitengeneza tafsiri zenu mnapomchukia mtu na natambua Prof anachukiwa kwa nguvu na uwezo alionao katika kujenga hoja.

mlipokosea ni kudhani kwamba prof anaweza kuongea kama Sugu au Mbowe, lazima daima ujue kwamba yule mtu anapoongea anaongea mambo mazito na magumu kwa watanzania wengi kuyaelewa haraka
hivi we jamaa una akili timamu kweli ?
 
Proffessa hapa unachomekea DELA better keep quite "disapered and died" maana yake nini Kwa hiyo yuko hai Azory?
 
Kwa nini unaamini ni suala la sentence structure na tafsiri ya lugha tu na si kile ambaçho kiko katika kichwa chake?
Kwa nini unataka kuuzika huu mjadala kirahisi namna hiyo?
Alipaswa kusema ‘waliopotea au kuuwawa’.

Siyo ‘waliopotea na kuuwawa’ maana hiyo inaacha mwanya wa tafsiri zingine.

Yeye kama mwanasheria nguli nilitegemea awe makini sana na uchaguzi wa maneno atumiayo.
 
Huyo jamaa anaonekana ni mbabaishaji flani hivi!

Nguli gani wa sheria hajui matumizi ya ‘na’ na ‘au’ na implications zake?

Hapo kwenye maelezo yake alipaswa tu kusema kuwa aliteleza kidogo na hakumaanisha kama ilivyopokelewa na watu.

Instead, he’s doubling down on it and blaming others!

Ndo maana baadhi yetu tuliguna na kukuna vichwa vyetu tuliposikia kateuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje.
Wakati Dr. Mahiga alipokuwa balozi wa Tanzania UN, aliletewa scandal alitulize na Kikwete.

Membe alilikoroga, ilionekana watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Tanzania, wengine wenye hadhi ya kibalozi, wanahusishwa na biashara za silaha na waasi wa Congo.

Membe alihojiwa na BBC, akakataa kijinga, katukatu, kama vile anajua nyendo za watumishi wote wa serikali ya Tanzania.

Kumbe BBC wakati wanamuuliza tayari wana ushahidi mpaka wa text messages za wafanyakazi wa serikali ya Tanzania.

Kesi akapelekewa Mzee Mahiga aitulize.

Nikawa namsikia anahojiwa na BBC. Kawanzia mbali, anawaeleza historia ya Tanzania kama msuluhishi wa migogoro, akaeleza tuna wakimbizi wengi, akawaeleza kwamba hatuna cha kufaidi ikiwa jirani zetu watapata maafa ya vita, tuna wanajeshi wengi wanalinda amani. Akaulizwa swali la mtegoi, anajua kwamba serikali ya Tanzania inahusika kuuza silaha?

Akajibu kwamba, serikali ya Tanzania haihusiki, ila hawezi kutoa jibu la uhakika kama watu ambao ni wafanyakazi wa serikali wanahusika wao binafsi kama wao si kwa niaba ya serikali, akasema wanaanzisha uchunguzi wa kimataifa kuchunguza na matokeo yatatangazwa.

Sikuisikia hiyo habari tena.

Nilisikia tu Balozi wa Tanzania Burundi karudishwa nyumbani.

Dr. Mahiga kukubali kwamba hawezi kujua kila kitu kuhusu wafanyakazi wa serikali wote sehemu zote muda wote, an unrealistic expectation, kuli defuse issue, ikatoka kwenye habari za serikali ya Tanzania inahusika, kwend kwenye inawezekana wafanyakazi wa serikali ya Tanzania wanahusika kama watu binafsi, uchunguzi unaendelea.

Mtu kama Kabudi anayejifanya anajua kila kitu, ni vigumu sana kukubali kakosea, au hajui kila kitu.

Na hiyo ni weakness, si strength.

Nasikitika sana wamemtoa Dr. Mahiga hapo foreign relations.
 
prof. hakukosea kabisa ila tumewazoea mkitengeneza tafsiri zenu mnapomchukia mtu na natambua Prof anachukiwa kwa nguvu na uwezo alionao katika kujenga hoja.

mlipokosea ni kudhani kwamba prof anaweza kuongea kama Sugu au Mbowe, lazima daima ujue kwamba yule mtu anapoongea anaongea mambo mazito na magumu kwa watanzania wengi kuyaelewa haraka
Usiwe mpambe mpaka ujitoe ufahamu na mnao wapamba wanawashangaa, mwenyewe amekiri kuwa alikosea na kusema mahojiano aliyoongea kiswahili ndio yachukuliwe yale ya kiingereza aliongea kitu asichokuwa na uhakika nacho..sasa wewe unatetea nini?
 
Wakati Dr. Mahiga alipokuwa balozi wa Tanzania UN, aliletewa scandal alitulize na Kikwete.

Membe alilikoroga, ilionekana watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Tanzania, wengine wenye hadhi ya kibalozi, wanahusishwa na biashara za silaha na waasi wa Congo.

Membe alihojiwa na BBC, akakataa kijinga, katukatu, kama vile anajua nyendo za watumishi wote wa serikali ya Tanzania.

Kumbe BBC wakati wanamuuliza tayari wana ushahidi mpaka wa text messages za wafanyakazi wa serikali ya Tanzania.

Kesi akapelekewa Mzee Mahiga aitulize.

Nikawa namsikia anahojiwa na BBC. Kawanzia mbali, anawaeleza historia ya Tanzania kama msuluhishi wa migogoro, akaeleza tuna wakimbizi wengi, akawaeleza kwamba hatuna cha kufaidi ikiwa jirani zetu watapata maafa ya vita, tuna wanajeshi wengi wanalinda amani. Akaulizwa swali la mtegoi, anajua kwamba serikali ya Tanzania inahusika kuuza silaha?

Akajibu kwamba, serikali ya Tanzania haihusiki, ila hawezi kutoa jibu la uhakika kama watu ambao ni wafanyakazi wa serikali wanahusika wao binafsi kama wao si kwa niaba ya serikali, akasema wanaanzisha uchunguzi wa kimataifa kuchunguza na matokeo yatatangazwa.

Sikuisikia hiyo habari tena.

Nilisikia tu Balozi wa Tanzania Burundi karudishwa nyumbani.

Dr. Mahiga kukubali kwamba hawezi kujua kila kitu kuhusu wafanyakazi wa serikali wote sehemu zote muda wote, an unrealistic expectation, kuli defuse issue, ikatoka kwenye habari za serikali ya Tanzania inahusika, kwend kwenye inawezekana wafanyakazi wa serikali ya Tanzania wanahusika kama watu binafsi, uchunguzi unaendelea.

Mtu kama Kabudi anayejifanya anajua kila kitu, ni vigumu sana kukubali kakosea, au hajui kila kitu.

Na hiyo ni weakness, si strength.

Nasikitika sana wamemtoa Dr. Mahiga hapo foreign relations.

Just a simple plausible deniability! To a career diplomat, that’s easy work!
 
Waziri amechemka on camera. Maelezo yake yaliacha mwanya kwa watu kuwa na tafsiri sahihi kuwa Aazory Gwanda amefariki.

Kakosea kwanza kwa kusema hivyo, halafu anaendelea kukosea kwa kushindwa kuomba radhi na kukubali kosa, analaumu tafsiri.
Makonda alifanya hivi hivi kwa Mo Dewji na Mengi (RIP). Asubuhi anasema hivi jioni anasema vingine mchana.

Tatizo anaamini kuwa Watanzania hatujui Kingereza. Hiyo ameamua kutuchanganya ili tuchanganyikiwe.

Anachosahau ni kwamba wanaohoji siyo Watanzania peke yao na si kweli kuwa Watanzania wote hawajui Kingereza.
 
prof. hakukosea kabisa ila tumewazoea mkitengeneza tafsiri zenu mnapomchukia mtu na natambua Prof anachukiwa kwa nguvu na uwezo alionao katika kujenga hoja.

mlipokosea ni kudhani kwamba prof anaweza kuongea kama Sugu au Mbowe, lazima daima ujue kwamba yule mtu anapoongea anaongea mambo mazito na magumu kwa watanzania wengi kuyaelewa haraka
we nae ni mpuuzi kuna alichokiongea hakijaeleweka??, na kama yupo hai kwanini hajapatikana??.Hivi Azory alikuwa na uhasama gani na watu mpka wamteke?acha kutoa matapishi katika uhai wa Binadamu mwenzako tena Baba wa familia na mtegemewa wa familia yake. Idiot
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amekanusha kuwa amethibitisha 'kifo' cha mwanahabari Azory Gwanda.

Msemaji mkuu wa serikali ya Tanzania, Dkt Hassan Abbas amemnukuu Profesa Kabudi kwa kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter akisema: "Nimepokea kwa masikitiko taarifa potofu zinazoendelea kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii ikinukuu kimakosa mahojiano yangu kwenye kipindi cha BBC FOCUS ON AFRICA zikidai kuwa nimethibitisha kwamba mwanahabari Azory Gwanda amefariki dunia."

Lakini Prof Kabudi pia amesema bado haijulikani kama Bw Gwanda yungali hai: "Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki. Vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuchunguza tukio hilo na matukio mengine yaliyotokea katika machafuko ya Kibiti, Pwani yaliyosababisha ama watu kadhaa kupoteza maisha au kupotea."

Kabudi amesema kuwa, kilichotokea ni tafsiri potofu ya kile alishokisema: "Hii sio tafsiri sahihi kuhusu kile nilichokisema. Katika mahojiano hayo nilieleza kuwa tukio lililotokea Kibiti lilikuwa ni la kuhuzunisha na wapo watanzania waliouawa na wengine kupotea. SIKUTHIBITISHA kuwa Azory Gwanda amefariki."
OMG Palamagamba has just admitted on BBC FOCUS ON AFRICA that Azory has “disappeared and died”. How did Palamagamba know that Azory is dead? @CPJAfrica Amnesty https://t.co/EjCrH98MuI
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amekanusha kuwa amethibitisha 'kifo' cha mwanahabari Azory Gwanda.

Msemaji mkuu wa serikali ya Tanzania, Dkt Hassan Abbas amemnukuu Profesa Kabudi kwa kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter akisema: "Nimepokea kwa masikitiko taarifa potofu zinazoendelea kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii ikinukuu kimakosa mahojiano yangu kwenye kipindi cha BBC FOCUS ON AFRICA zikidai kuwa nimethibitisha kwamba mwanahabari Azory Gwanda amefariki dunia."

Lakini Prof Kabudi pia amesema bado haijulikani kama Bw Gwanda yungali hai: "Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki. Vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuchunguza tukio hilo na matukio mengine yaliyotokea katika machafuko ya Kibiti, Pwani yaliyosababisha ama watu kadhaa kupoteza maisha au kupotea."

Kabudi amesema kuwa, kilichotokea ni tafsiri potofu ya kile alishokisema: "Hii sio tafsiri sahihi kuhusu kile nilichokisema. Katika mahojiano hayo nilieleza kuwa tukio lililotokea Kibiti lilikuwa ni la kuhuzunisha na wapo watanzania waliouawa na wengine kupotea. SIKUTHIBITISHA kuwa Azory Gwanda amefariki."
hatumshangai hata Mwakyembe alishasema hatukumuelewa alisema kwenye bunge la katiba alipokuwa anapinga andiko/thethis yake ya Phd juu ya muungano uzuri ni kwamba mambo yakiandikwa hayafutiki.
Huyu nae anasema hatukumuelewa ? labda yeye ndiyo hajielewi ANZORY GWANDA KAUWAWA basi.
1. aKIONGEA kWA JAZIBA huku akipigiwa makofi bwana Magufuli ALIHOJI kwanini wanauwawa wa CCM tu? hapa alimanisha wauaji wale walikuwa wapinzani.
Akiandika humu JINGA LAO alishawahi kuhoji kwann gazeti la mwananchi linakuwa la kwanza kuripoti mauaji ya Rufiji kweli mwandishi AKAUWAWA
AKIONGEA BUNGENI wazir wa mambo ya ndani bwana Lugola alishawahi kusema Gwanda kaenda kutafuta maisha
 
Usiwe mpambe mpaka ujitoe ufahamu na mnao wapamba wanawashangaa, mwenyewe amekiri kuwa alikosea na kusema mahojiano aliyoongea kiswahili ndio yachukuliwe yale ya kiingereza aliongea kitu asichokuwa na uhakika nacho..sasa wewe unatetea nini?
Usiwe mpambe mpaka ujitoe ufahamu na mnao wapamba wanawashangaa, mwenyewe amekiri kuwa alikosea na kusema mahojiano aliyoongea kiswahili ndio yachukuliwe yale ya kiingereza aliongea kitu asichokuwa na uhakika nacho..sasa wewe unatetea nini?
unadhani kila mtu anaweza kupotoshwa kwa ulimwengu huu wa utandawazi? Prof. kasema kwamba mlishindwa kumuelewa na kuanza kumtafsiri vibaya lakini wewe unapotosha eti kakiri kukosea. Prof shikilia hapohapo kuna watu wanataka kupima fikra za kiprofesa kwa uzushi na upotoshaji
 
Back
Top Bottom