Waziri Kigwangalla aagiza kampuni ya Uwindaji ya OBC ya Loliondo kurudi walikotokea kabla ya Januari 2018

Waziri Kigwangalla aagiza kampuni ya Uwindaji ya OBC ya Loliondo kurudi walikotokea kabla ya Januari 2018

Hapa tuwe wazalendo, tu fight for our natural wealth, sio kusema tuone kama wazir ataweza kuwafukuza, tumuunge mkono ndio tutapata mafanikio,
Tupo Tayari kumpa ushirikiano atakaouhitaji!kwa walichokifanya hao waarabu kwa kushirikiana na viongozi wa ccm waliopita hata hawakustahili kutoka wakiwa hai!!
 
hakuna nchi ya afrika yenye maendeleo hata moja chukua mali za watu utalipa , watu watkuacha utafute sabuni yakukogea ndio maana kenya wanatuacha , uwazi kuchukua mali za watu wamepewa na serikali yenu iliyopita wataondoka bure ?
sio manji
 
Nachoshangaa na kinanisikitisha sana ni kuona watu wakipinga jitihada za kumkomboa mtanzania mnyonge, na hao wanaopinga ni vijana watz tena wasomi, then baada ya siku utawasikia wakitaka kugombea nafas za uongoz , na wakipata nyazifa hawana msaada wowote kwa serkal ili kurudisha mali zilizobiafsishwa kwa mikataba mibovu au ardh na viwanda visivyoendelezwa, utaskia wakibwabwaja tu ooohhh sheria ya mkataba itatufungs, ooohh sheria ya mkataba tutalipa pesa nyingi, ivi hiyo sheria ya mikataba inaruhusu mwenyemali aibiwe na kumlinda mwizi/ mnyanyasaji. Tusiwe na mihemko isiyo na tija. Penye ukwel tuitetee tanzania yetu.
 
Hili limekaa vizuri. Mikataba ya kikoloni au kimangungu haina nafasi tena.
Lakini approach iwe tofauti. Wakae nao na kuwaeleza ukweli huo


Nakumbuka ni rais Mwinyi ndiye aliyewapa kibali hawa waarab, watu walilalamika sana juu ya hili. Mwinyi aliiuza sana hii nchi tena kwa kijinga tu.
 
Waziri wa Maliasili asili na utalii Mh. Kigwangala akiwa katika ziara yake wilayani Ngorongoro pamoja na kuagiza kuvifuta vibali vyote vya uwindaji nchi nzima ikiwamo vya kampuni ya ORTELLO BUSINESS CORPORATION (OBC) ya Loliondo, ameagiza kampuni hiyo ya MWARABU kujiandaa kurudi walikotokea, kwasababu hata kama wakibaki mchakato mpya wa ugawaji vitalu vya uwindaji utakapoanza hautawahusu.

Ikumbukwe kampuni ilipewa eneo hilo miaka ya 1990 kwa mkataba wa miaka 99.View attachment 618635
Namuona lazaro nyalandu akihamia chadema kabla ya 2020!
 
Kigwangala awaulize kwanza Chadema wanasemaje kuhusu hii ishu,maana watakuja kumlaumu na kumponda anafukuza wawekezaji!!
Spate ushauri wa shadow minister wa utalii na Mali asili
 
Ivi watz wote tukiziunga mkono jitihada za serkal, tutafanikiwa fasta, bt serkal inatupigania while kunawatu wengine kazi yao ni kupinga na kuupotosha ukweli.
Hili ndilo la msingi zaidi.Uzalendo unatakiwa kuzidi unazi.
 
mwinyi alikuwa rahisi wa wapi Tanzania of course fukuza waarabu wape haki Yao
mwisho bahersa na manji na dewji mtamfukuza sio jipya hilo
 
Hili limekaa vizuri. Mikataba ya kikoloni au kimangungu haina nafasi tena.
Lakini approach iwe tofauti. Wakae nao na kuwaeleza ukweli huo
sidhani kama mwarabu aliingia mkataba wa kilofa. Labda kwa vile ni waarabu na akili za .....You will pay dearly
 
Hao jamaa wamepata eneo hilo kihalali.
Na wanalipa fedha nyingi.
Hili ni eneo la mbuga za wanyama sio la kulima.
Sasa hivi kuwapo kwao kumesaidia sana kuhifadhi wanyama na mazingira.
Ndo maana Mkapa aliwapa na aliwatetea sana kuwa lato lao ni muhimu kuliko lingeachwa kwa poachers na wavamizi.
Wenyewe wanakuja mara chache kwa mwaka.
Kampeni hizi zilianza ki udini ..kwanini apewe mwarabu....angekua mzungu isinge kuwa noma.
Wana vijiji wamepata misaada mingi sana kama shule maji na hospital..
Na wanalipa kodi...
Kuwaondoa haileti faida yoyote ile zaidi ya furaha ya nafsi za uchoyo
 
Back
Top Bottom